Nini kinaendelea huko Tarime kati ya Polisi na wananchi?

eden kimario

JF-Expert Member
Jun 13, 2015
10,227
16,178
Kunasemekana huko Tarime kwa mbunge Heche kuna mapambano kati ya police na Raia ambao wanapinga ACACIA kuendelea na shughuli zao wakidai ni wezi kwa mujibu wa Rais Magufuli na hawahitaji shughuli zozote kuendelea mgodini hapo.

Sasa ni vita kati ya Raia na mabomu ya polisi
caab453b8d722e59a82099235210eb88.jpg


Idadi kubwa ya watu wamekusanyika leo katika mgodi wa North Mara kwa siku ya pili mfululizo nchini Tanzania kushinikiza walipwe fidia kutokana na kile wanachodai kufanyiwa madhira mabaya kutokana na operesheni za mgodi huo katika eneo la Nyamongo, wilaya ya Tarime nchini Tanzania. Hali hiyo inatokana na kile kinachoolezwa ripoti mbili za madini za hivi karibuni nchini humo kutaja kampuni tanzu inayosimamia mgodi huo ya Acacia kutosajiliwa.

Mwandishi wa DW Swahili Sudi Mnette amezungumza na Chacha Heche ambaye ni Mwananchi na mjumbe wa kamati iliyoundwa na aliyekuwa waziri wa nishati na madini wa Tanzania Profesa Sospeter Muhongo kufuatilia matatizo ya wananchi na mgodi kwa muda mrefu.

 
Kunasemekana huko tarime kwa mbunge heche kuna mapambano kati y'a police n'a Raia ambao wanapinga ACACIA kuendelea n'a shuhuli zao wakidai ni wezi kwa mujibu wa Rais magufuli n'a hawaitaji shuhuli zozote kuendelea mgodini hapo
Sasa ni vita kati y'a Raia n'a mabomu y'a police
caab453b8d722e59a82099235210eb88.jpg
Wanawachukia bure Acacacia, kwanini wasimpige vita mtu aliye wakaribisha hawa watu kutuibia? Acacia ana mwenyeji wake waliekubaliana kisheria namna ya kuchuma rasilimali zetu au wanatumia ule msemo kwamba aliyekamatwa na ngozi ndiye mwizi wa mbuzi?
 
Wanawachukia bure Acacacia, kwanini wasimpige vita mtu aliye wakaribisha hawa watu kutuibia? Acacia ana mwenyeji wake waliekubaliana kisheria namna ya kuchuma rasilimali zetu au wanatumia ule msemo kwamba aliyekamatwa na ngozi ndiye mwizi wa mbuzi?
Watani zangu hawa washaathiriwa na bangi, we waache
 
nilihisi kutokea kwa jambo km hili sehemu fulani....na leo limetokea!
kama utani lakini nchi inachafuka hii kutokana na kukosa busara za wanaotuongoza; viongozi wanakazana kuwaita watu wezi, kule mbunge anatangaza kuhamasisha raia wakavamie migodi......jamii zetu zina mkusanyiko wa watu wenye uelewa malengo mbalimbali,.....wengine wanasubiri kwa hamu kauli kama hizo ili watende waliyoyadhamiria....matokeo ndo hayo!!!!
 
Wanawachukia bure Acacacia, kwanini wasimpige vita mtu aliye wakaribisha hawa watu kutuibia? Acacia ana mwenyeji wake waliekubaliana kisheria namna ya kuchuma rasilimali zetu au wanatumia ule msemo kwamba aliyekamatwa na ngozi ndiye mwizi wa mbuzi?

mkuu kama ni mwizi ameingia nyumbani kwako lazima udili nae haijalishi ameletwa na mtoto wako au lah, mwenyewe atamtaja huko ameingiaje hapa.
 
Hao polisi watakua hawakubaliani na kauli ya raisi ama inakuaje?
Maana sielewi haya mambo
Police look very it's not to that extent
 
Wananchi wameamua kwenda kutafta za matumizi. Si mbaya we used to live our lives through mines, baada ya wazungu kuja na kujenga kuta maisha yamekuwa magumu mno. Zameni ndani kwenye kinu mchukue kidogo halafu mtoke
 
ACACIA haijasajiliwa Tanzania, ACACIA imewaibia watanzania hii ni kwa mujibu wa Serikali ya Tanzania..Pia serikali imetuaminisha huu umasikini wetu chanzo ni ACACIA...

Sasa mnataka wananchi wafanye nini kama sio kukamata mwizi na kumyang'anya mali anazomiliki??

Heko wananyamongo, komaeni mpaka muingie hapo plant na kule pit mjipimie dhahabu maana ACACIA haipo kihalali..
 
Back
Top Bottom