Nini kimewakumba Maswahiba wa Lowassa; Yusuph Manji na Rostam Aziz?

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
Wadau, amani iwe kwenu.

Mtakumbuka kuwa, katika kipindi cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015, Waziri Mkuu aliyelazimishwa kujiuzulu kutokana na kashfa za ufisadi wa Richmond, Edward Lowasa, alitengeneza mtandao wa wafanyabiashara ambao ndio waliokuwa wanamfadhili kwenye harakati zake za kisiasa. Maswahiba hao walikuwa wanampa mabilioni ya fedha Edward Lowasa akiwa ndani ya CCM na hata baada ya kuhamia CHADEMA. Hawa ndio walioratibu kauli mbiu ya ULIPO TUPO.

Hata hivyo, baada ya Uchaguzi wa Oktoba 2015, maswahiba hawa inaelekea hesabu zao hazipangiki. Rostam Aziz inadaiwa kuwa amekimbia nchi tangu Septemba 2015 na haijulikani yupo wapi kwa sasa ingawa baadhi ya taarifa zinadai kuwa yupo Uingereza na wengine wakisema yupo Uarabuni na wengine wakisema yupo Marekani. Wengine wanadai kuwa Rostam bado yupo nchini isipokuwa kwa sasa ameamua kujifungia tani kwa vile mambo yake kibiashara yanaenda hovyo. kafulia.

Yusuph Manji, Diwani wa Mbagala Kuu, aliyekuwa Mwenyekiti wa Yanga kabla ya kuachia ngazi hivi majuzi baada ya wazee wa Yanga kushtuka dili la kumkodisha timu kwa miaka 10, inadaiwa kuwa hayupo Tanzania kwa sasa. Manji amelazimika kuondoka nchini kutokana na msuguano ulioibuka ndani ya klabu ya Yanga. Aidha, kabla ya hali hiyo, Yusuph Manji aliamua kujitoa kuongoza Quality Group, kampuni ambayo inadaiwa kutumia mwanya wa Manji kuongoza Yanga kuikopesha timu hiyo mabilioni ya fedha ambapo mpaka sasa timu hiyo inadaiwa Bilioni 5. Baadhi ya wana Yanga wanahoji, inakuwaje mtu ambaye aliahidi kuisaidia Yanga aidai fedha zote hizo? Ina maana kwa miaka yote Manji aliyoongoza yanga, timu haikuwa na mapato yoyote hadi deni limefikia kiasi hicho? Je hilo deni limetokana na nini? Wanachama wengine wameomba TAKUKURU kuchunguza deni hilo.

Kwa ujumla, hawa marafiki wa Lowasa ni dhahiri kwamba walikuwa wanafanya biashara kijanja ujanja na ndio maana walikuwa wanatumia fedha zao hovyo hovyo kufadhili kampeni za fisadi Lowasa.

Kutoweka kwa Manji, Rostam pamoja na akina Karamagi kumeenda sambamba na kufunga mdomo Edward Lowasa. Kwa sasa mwanasiasa huyo hayupo kabisa kwenye ulimwengu wa siasa na hata hizi harakati za CHADEMA za UKUTA Septemba Mosi ameamua kujiweka kando.

Ni wakati sasa wa Lowassa kujitokeza hadharani na kuwaeleza Watanzania nini kimewasibu Maswahiba wake. Maana kule Mbagala Kuu wametapeliwa kwa kumpa Manji Udiwani kwa ahadi hewa. Yanga nao wametapeliwa. Na inawezekana na Lowasa naye katapeliwa.
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Mtakumbuka kuwa, katika kipindi cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015, Waziri Mkuu aliyelazimishwa kujiuzulu kutokana na kashfa za ufisadi wa Richmond, Edward Lowasa, alitengeneza mtandao wa wafanyabiashara ambao ndio waliokuwa wanamfadhili kwenye harakati zake za kisiasa. Maswahiba hao walikuwa wanampa mabilioni ya fedha Edward Lowasa akiwa ndani ya CCM na hata baada ya kuhamia CHADEMA. Hawa ndio walioratibu kauli mbiu ya ULIPO TUPO.

Hata hivyo, baada ya Uchaguzi wa Oktoba 2015, maswahiba hawa inaelekea hesabu zao hazipangiki. Rostam Aziz inadaiwa kuwa amekimbia nchi tangu Septemba 2015 na haijulikani yupo wapi kwa sasa ingawa baadhi ya taarifa zinadai kuwa yupo Uingereza na wengine wakisema yupo Uarabuni na wengine wakisema yupo Marekani. Wengine wanadai kuwa Rostam bado yupo nchini isipokuwa kwa sasa ameamua kujifungia tani kwa vile mambo yake kibiashara yanaenda hovyo. kafulia.

Yusuph Manji, Diwani wa Mbagala Kuu, aliyekuwa Mwenyekiti wa Yanga kabla ya kuachia ngazi hivi majuzi baada ya wazee wa Yanga kushtuka dili la kumkodisha timu kwa miaka 10, inadaiwa kuwa hayupo Tanzania kwa sasa. Manji amelazimika kuondoka nchini kutokana na msuguano ulioibuka ndani ya klabu ya Yanga. Aidha, kabla ya hali hiyo, Yusuph Manji aliamua kujitoa kuongoza Quality Group, kampuni ambayo inadaiwa kutumia mwanya wa Manji kuongoza Yanga kuikopesha timu hiyo mabilioni ya fedha ambapo mpaka sasa timu hiyo inadaiwa Bilioni 5. Baadhi ya wana Yanga wanahoji, inakuwaje mtu ambaye aliahidi kuisaidia Yanga aidai fedha zote hizo? Ina maana kwa miaka yote Manji aliyoongoza yanga, timu haikuwa na mapato yoyote hadi deni limefikia kiasi hicho? Je hilo deni limetokana na nini? Wanachama wengine wameomba TAKUKURU kuchunguza deni hilo.

Kwa ujumla, hawa marafiki wa Lowasa ni dhahiri kwamba walikuwa wanafanya biashara kijanja ujanja na ndio maana walikuwa wanatumia fedha zao hovyo hovyo kufadhili kampeni za fisadi Lowasa.

Kutoweka kwa Manji, Rostam pamoja na akina Karamagi kumeenda sambamba na kufunga mdomo Edward Lowasa. Kwa sasa mwanasiasa huyo hayupo kabisa kwenye ulimwengu wa siasa na hata hizi harakati za CHADEMA kutaka kushika UKUTA Septemba Mosi ameamua kujiweka kando.

Ni wakati sasa wa Lowasa kujitokeza hadharani na kuwaeleza Watanzania nini kimewasibu Maswahiba wake. Maana kule Mbagala Kuu wametapeliwa kwa kumpa Manji Udiwani kwa ahadi hewa. Yanga nao wametapeliwa. Na inawezekana na Lowasa naye katapeliwa.

Kila siku nakuambia mambo usoyajua usikimbilie kubwatuka!! Rostam Aziz alihamishia biashara zake nyingi Kenya!! Rostam aliuza shares vodacom ktk mpango wake wa kuhamishia uwekezaji Kenya na hawezi kufulia kijinga!!!
 
IMG-20160818-WA0025.jpeg
 
Kila siku nakuambia mambo usoyajua usikimbilie kubwatuka!! Rostam Aziz alihamishia biashara zake nyingi Kenya!! Rostam aliuza shares vodacom ktk mpango wake wa kuhamishia uwekezaji Kenya na hawezi kufulia kijinga!!!
Na Yusuph Manji kahamishia biashara zake wapi?
 
hivi KARAMAI mzee wa tics bado anamiliki 35 % za pale ticks au amesha toka
, rostama kufilisika sio rahis mzee lizabon maana ana hisa na matenda mengi ya kifisadi kwenye migodi mingi sana kama buzwagi na buliynku, na pia kwenye vodacom ana superdealer kama SHIVACOM kupitia kwa akina FRED lowasa
 
hivi KARAMAI mzee wa tics bado anamiliki 35 % za pale ticks au amesha toka
, rostama kufilisika sio rahis mzee lizabon maana ana hisa na matenda mengi ya kifisadi kwenye migodi mingi sana kama buzwagi na buliynku, na pia kwenye vodacom ana superdealer kama SHIVACOM kupitia kwa akina FRED lowasa
Mkuu, kufilisika kwa hawa mataikuni si sawa na kufilisika kwa TRUVADA.
 
... Maswahiba hao walikuwa wanampa mabilioni ya fedha Edward Lowasa akiwa ndani ya CCM na hata baada ya kuhamia CHADEMA.
Aisee! Ina maana mgombea udiwani wa CCM alikuwa anatoa ufadhili wa hela kwa mgombea wa CHADEMA?
 
Lizaboni, amechanganyikiwa kama walivyo wanaCCM wenzake , akilala anamuwaza Lowassa tu.......Manji ni Diwani wa CCM so kama ni tapeli basi anawakilisha utapeli wa CCM ........
Sijachanganyikiwa. Mimi ni msema kweli
 
Wadau, amani iwe kwenu.

Mtakumbuka kuwa, katika kipindi cha kuelekea uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015, Waziri Mkuu aliyelazimishwa kujiuzulu kutokana na kashfa za ufisadi wa Richmond, Edward Lowasa, alitengeneza mtandao wa wafanyabiashara ambao ndio waliokuwa wanamfadhili kwenye harakati zake za kisiasa. Maswahiba hao walikuwa wanampa mabilioni ya fedha Edward Lowasa akiwa ndani ya CCM na hata baada ya kuhamia CHADEMA. Hawa ndio walioratibu kauli mbiu ya ULIPO TUPO.

Hata hivyo, baada ya Uchaguzi wa Oktoba 2015, maswahiba hawa inaelekea hesabu zao hazipangiki. Rostam Aziz inadaiwa kuwa amekimbia nchi tangu Septemba 2015 na haijulikani yupo wapi kwa sasa ingawa baadhi ya taarifa zinadai kuwa yupo Uingereza na wengine wakisema yupo Uarabuni na wengine wakisema yupo Marekani. Wengine wanadai kuwa Rostam bado yupo nchini isipokuwa kwa sasa ameamua kujifungia tani kwa vile mambo yake kibiashara yanaenda hovyo. kafulia.

Yusuph Manji, Diwani wa Mbagala Kuu, aliyekuwa Mwenyekiti wa Yanga kabla ya kuachia ngazi hivi majuzi baada ya wazee wa Yanga kushtuka dili la kumkodisha timu kwa miaka 10, inadaiwa kuwa hayupo Tanzania kwa sasa. Manji amelazimika kuondoka nchini kutokana na msuguano ulioibuka ndani ya klabu ya Yanga. Aidha, kabla ya hali hiyo, Yusuph Manji aliamua kujitoa kuongoza Quality Group, kampuni ambayo inadaiwa kutumia mwanya wa Manji kuongoza Yanga kuikopesha timu hiyo mabilioni ya fedha ambapo mpaka sasa timu hiyo inadaiwa Bilioni 5. Baadhi ya wana Yanga wanahoji, inakuwaje mtu ambaye aliahidi kuisaidia Yanga aidai fedha zote hizo? Ina maana kwa miaka yote Manji aliyoongoza yanga, timu haikuwa na mapato yoyote hadi deni limefikia kiasi hicho? Je hilo deni limetokana na nini? Wanachama wengine wameomba TAKUKURU kuchunguza deni hilo.

Kwa ujumla, hawa marafiki wa Lowasa ni dhahiri kwamba walikuwa wanafanya biashara kijanja ujanja na ndio maana walikuwa wanatumia fedha zao hovyo hovyo kufadhili kampeni za fisadi Lowasa.

Kutoweka kwa Manji, Rostam pamoja na akina Karamagi kumeenda sambamba na kufunga mdomo Edward Lowasa. Kwa sasa mwanasiasa huyo hayupo kabisa kwenye ulimwengu wa siasa na hata hizi harakati za CHADEMA kutaka kushika UKUTA Septemba Mosi ameamua kujiweka kando.

Ni wakati sasa wa Lowasa kujitokeza hadharani na kuwaeleza Watanzania nini kimewasibu Maswahiba wake. Maana kule Mbagala Kuu wametapeliwa kwa kumpa Manji Udiwani kwa ahadi hewa. Yanga nao wametapeliwa. Na inawezekana na Lowasa naye katapeliwa.
mkuu hivi bado hujapata ukuu wa wilaya tu?au bado unaendelea na kazi yako ile ya ujumbe wa nyumba kumi
 
Back
Top Bottom