mngony
JF-Expert Member
- Jul 27, 2012
- 5,193
- 6,381
Kama tunakumbuka vizuri, ripoti ya kwanza ya CAG Assad baada ya kuingia kwa awamu ya 5 pamoja na ubadhirifu mwingine ilionesha ufisadi wa kiasi cha pesa 1.5 Trilioni ambacho hakikuoneka wapi kilienda.
Baada ya ripoti hiyo, CAG alishambuliwa sana na serikali na Chama wakiwemo mawaziri, Spika, makada na wafuasi wa Chama na Rais aliyekuwa madarakani.
Ufisadi huo ulikuwa hata ukijumlisha ufisadi na kashfa za Meremeta, Kagoda, Ununuzi wa Radar, Buzwagi na RICHMOND hazikufika kiasi cha 1.5 T. Na huo ndio ulikuwa mwaka wake wa kwanza tu wa Bajeti.
Ni vile tu vyombo vya habari viliminywa na kutishiwa huku matukio ya watu kutekwa, kupotea yakishamiri bila yeyote kusema au kuwajibika. Kulikuwa na hofu kubwa sana.
Ripoti ile haikupewa nafasi kuwasilishwa kwa Rais wala bungeni haikujadiliwa. Rais hakuwahi kuizungumzia hata kidogo kanakwamba 1.5 T ni kiasi kidogo.
Baada ya kelele kuwa nyingi za wapinzani na wananchi kuhusu 1.5 T ziko wapi ndio akaibuka Polepole makao makuu madogo 'akipiga' hesabu kutuonesha ilipo 1.5 T.
Misukosuko ilimfuata Prof Assad mpaka kutolewa katika nafasi yake. Kuna kipindi hadi kulizuka tetesi za kutekwa kwake.
Wenye akili tukajua hakukuwa na dhamira ya kweli kupambana na wizi na ufisadi bali ilikuwa ni hadaa na danganya toto huku viongozi wakijinadi kwa Uzalendo.
Sasa leo wale wapenzi na wakereketwa wa mtu mmoja badala ya Taifa mnashangazwa nini na ripoti huru ya CAG wa sasa? Ambayo hazifiki 1.5 T.
Kipi kinachowashangaza mpaka mnaleta chuki kwa CAG, spika na hata Rais Samia. Lazima tuelezane ukweli ili tusonge mbele, hizo ndege mlitaka hasara ifike ngapi? Yani hakuna mipango, madeni yanaongezeka tu, ndege haziruki kwenda nje na hasara kila siku bado mnataka tuendelee kisa tu ndio mradi wake pekee huku watumishi hawapandishiwi madaraja na kuongezewa mishahara kwa miaka mitano sasa na wastaafu mlikuwa mkiwazungusha na uhakiki mpaka leo.
Si alikuwa akisema msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Sasa kwa nini mnataka CAG asiseme ukweli? Wapinzani wamekuwa wakisema mara kadhaa kuhusu baadhi ya mambo mkawaita wahaini, wasiopenda nchi yao, wanatumiwa na mabeberu. Tulieni
Baada ya ripoti hiyo, CAG alishambuliwa sana na serikali na Chama wakiwemo mawaziri, Spika, makada na wafuasi wa Chama na Rais aliyekuwa madarakani.
Ufisadi huo ulikuwa hata ukijumlisha ufisadi na kashfa za Meremeta, Kagoda, Ununuzi wa Radar, Buzwagi na RICHMOND hazikufika kiasi cha 1.5 T. Na huo ndio ulikuwa mwaka wake wa kwanza tu wa Bajeti.
Ni vile tu vyombo vya habari viliminywa na kutishiwa huku matukio ya watu kutekwa, kupotea yakishamiri bila yeyote kusema au kuwajibika. Kulikuwa na hofu kubwa sana.
Ripoti ile haikupewa nafasi kuwasilishwa kwa Rais wala bungeni haikujadiliwa. Rais hakuwahi kuizungumzia hata kidogo kanakwamba 1.5 T ni kiasi kidogo.
Baada ya kelele kuwa nyingi za wapinzani na wananchi kuhusu 1.5 T ziko wapi ndio akaibuka Polepole makao makuu madogo 'akipiga' hesabu kutuonesha ilipo 1.5 T.
Misukosuko ilimfuata Prof Assad mpaka kutolewa katika nafasi yake. Kuna kipindi hadi kulizuka tetesi za kutekwa kwake.
Wenye akili tukajua hakukuwa na dhamira ya kweli kupambana na wizi na ufisadi bali ilikuwa ni hadaa na danganya toto huku viongozi wakijinadi kwa Uzalendo.
Sasa leo wale wapenzi na wakereketwa wa mtu mmoja badala ya Taifa mnashangazwa nini na ripoti huru ya CAG wa sasa? Ambayo hazifiki 1.5 T.
Kipi kinachowashangaza mpaka mnaleta chuki kwa CAG, spika na hata Rais Samia. Lazima tuelezane ukweli ili tusonge mbele, hizo ndege mlitaka hasara ifike ngapi? Yani hakuna mipango, madeni yanaongezeka tu, ndege haziruki kwenda nje na hasara kila siku bado mnataka tuendelee kisa tu ndio mradi wake pekee huku watumishi hawapandishiwi madaraja na kuongezewa mishahara kwa miaka mitano sasa na wastaafu mlikuwa mkiwazungusha na uhakiki mpaka leo.
Si alikuwa akisema msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Sasa kwa nini mnataka CAG asiseme ukweli? Wapinzani wamekuwa wakisema mara kadhaa kuhusu baadhi ya mambo mkawaita wahaini, wasiopenda nchi yao, wanatumiwa na mabeberu. Tulieni