Nini kifanyike kwa Upinzani tunapojiandaa na Uchaguzi wa 2025

Consultant

JF-Expert Member
Jun 15, 2008
11,401
20,661
Uchaguzi huu umekwisha na Upinzani unapaswa kucheza karata zake vizuri ili kuepusha majanga mengine mwaka 2025. Kelele za kutaka uchaguzi urudiwe hazitozaa matunda sasa ambapo hata maandamano tu ya kupinga Mbowe kupewa kesi nzito yamefail.

Nini kifanyike
1. Wale Wapinzani wawili walioachiwa majimbo waachwe waingie Bungeni wakapiganie haki. Hii haitakuwa kubariki wizi uliofanyika.

2. Viti maalumu kutoka CHADEMA nao waende bungeni. Haki itendeke kwenye kuteua nani aende ili kuepuka kukipasua Chama zaidi.

3. Agenda kuu Bungeni kila mpinzani anaposimama iwe ni kudai KATIBA MPYA/marekebisho makubwa ya Katiba pamoja na kuifumua NEC.

4. Wapinzani waliopo nje ya Bunge watumie platforms zote kuimba wimbo mmoja: KATIBA mpya na NEC iliyo huru.

5. Ikitokea akafa Mbunge, Upinzani uwe umeshadeclare mapema kutokushiriki marudio yoyote ya Uchaguzi kwa NEC hii ya sasa.

6. Warsha mbalimbali ziandaliwe na kuibua mijadara ya umuhimu wa Katiba mpya/muundo wa NEC iliyo huru. Wanaweza kualikwa wadau mbalimbali hasa wale development parners (a.k.a mabeberu) ambao wana mchango mkubwa kwenye bajeti ya Serikali na hivyo wakikohoa kidogo tu Jiwe anaweza kuwasikia na kutii.

7. Wapinzani wajipange na kufungua matawi mpaka kwenye ngazi za kata. Mafunzo yaanze kutolewa mapema ili by 2025 kuwe kuna misingi imara na hata iwe rahisi kupata mawakala bora kuliko ilivyokuwa mwaka huu.

Kususa haitakuwa strategy nzuri. Sanasana itawapa nafasi CCM kujiandaa vizuri mwaka 2025 na wao wakaja na system ya “kura za mapema” kama ilivyokuwa Zanzibar mwaka huu ili waibe kiulaini na kufunga hesabu mapema.
 
Kinachotakiwa ni kuwa na dhamira ya dhati ya kutetea maslahi ya watanzania.

Kwa hizi siasa za kilaghai za Mbowe, hakuna aina ya maandalizi mengine itakayozaa matunda...

Hii ni point muhimu sana, Mbowe na Lissu wana siasa za kilaghai ambazo hazina uhalisia wala kugusa maisha ya mwananchi wa kawaida, Zitto na Dr Slaa wapo vizuri na ndio walioweza kupandisha upinzani mbele ya umma, kama Mbowe na Lissu wanataka kuendelea na siasa wabaki nyuma wawaaachie vijana kina Mnyika na Zitto wafanye siasa za hoja.
 
Huwa najiuliza kwa nini CCM wengi wanawashauri chadema kutosusia bunge? Na maalim akubali kuwa makamo wa rais? Wanaogopa nini?
Sababu mojawapo ni kwamba kususia mara nyingi huwa hakuzai matunda chanya na mifano hai tunayo hapa hapa Tanzania.

CUF walisusia huko Zanzibar. Sioni cha zaidi walichogain zaidi. Mimi sioni kama ni sawa kususia bunge then kuhamia JF na Twitter kutoa povu
 
Hata Kama Wapizani wakaunza orgaization hadi kwenye mabalozi wa Nyumba Kumi na Wakaungana wote ikifika 2025 kama Mfumo ni huu huu wajue Hata Kura Moja ya Urais Hawataipata. Ni Hivi Hauwezi Itofautisha CCM na Serikali/Dola. Hata wasipofanya campagn wakaingia Kuanzia Kusambaza Masaduku ya Kura, Uhesabuji wa Kura na Kutanganza Mshindi Wataendelea kushinda tena kwa Kishindo kama kauili yao. Solution sio Tume Huru ya Uchaguzi bali ni Upatikanaji wa Katiba Mpya...,
 
Uchaguzi huu umekwisha na Upinzani unapaswa kucheza karata zake vizuri ili kuepusha majanga mengine mwaka 2025. Kelele za kutaka uchaguzi urudiwe hazitozaa matunda sasa ambapo hata maandamano tu ya kupinga Mbowe kupewa kesi nzito yamefail.

Nini kifanyike

1. Wale Wapinzani wawili walioachiwa majimbo waachwe waingie Bungeni wakapiganie haki. Hii haitakuwa kubariki wizi uliofanyika.

2. Viti maalumu kutoka CHADEMA nao waende bungeni. Haki itendeke kwenye kuteua nani aende ili kuepuka kukipasua Chama zaidi.

3. Agenda kuu Bungeni kila mpinzani anaposimama iwe ni kudai KATIBA MPYA/marekebisho makubwa ya Katiba pamoja na kuifumua NEC.

4. Wapinzani waliopo nje ya Bunge watumie platforms zote kuimba wimbo mmoja: KATIBA mpya na NEC iliyo huru.

5. Ikitokea akafa Mbunge, Upinzani uwe umeshadeclare mapema kutokushiriki marudio yoyote ya Uchaguzi kwa NEC hii ya sasa.

6. Warsha mbalimbali ziandaliwe na kuibua mijadara ya umuhimu wa Katiba mpya/muundo wa NEC iliyo huru. Wanaweza kualikwa wadau mbalimbali hasa wale development parners (a.k.a mabeberu) ambao wana mchango mkubwa kwenye bajeti ya Serikali na hivyo wakikohoa kidogo tu Jiwe anaweza kuwasikia na kutii.

7. Wapinzani wajipange na kufungua matawi mpaka kwenye ngazi za kata. Mafunzo yaanzs kutolewa mapema ili by 2025 kuwe kuna misingi imara na hata iwe rahisi kupata mawakala bora kuliko ilivyokuwa mwaka huu.

Kususa haitakuwa strategy nzuri. Sanasana itawapa nafasi CCM kujiandaa vizuri mwaka 2025 na wao wakaja na system ya “kura za mapema” kama ilivyokuwa Zanzibar mwaka huu ili waibe kiulaini na kufunga hesabu mapema.
Izo pesa za kufungua matawi kisha wayalinde watatoa wapi wakatai hawana pesa?
Walipokuwa na pesa mliwashauri waka kataa sasa iweje leo ambapo hawana pesa.
 
Haya
Mapambano ya kupigania uhuru ni kila siku hayasubiri mwaka fulani.
mambo mnayaongea mkiwa wapi, mbona barabarani hatuwaoni?
Tunataka mtoke mgongeshwe mpungue humu JF ili wabaki watu wenye kusimamia maneno yao.
 
Wanaccm naona mnashinda kuwapa ushauri wapinzani. Kwa nini msishauriane jinsi ya kuongeza kura za Magu zifike 107% kama Ivory Cost kabisa na wabunge mhakikishe wapinzani wanapata 0%

Mkuu wapinzani wangekuwa -7% kabisa ili Magu ajulikane kuwa ni baba lao!
 
Ushauri mzuri sana mkuu ulio utoa.

Mimi naenda mbali zaidi ya hapa sio tuu mwaka wa 2025 bali 2035.
Yaani wajiandae kwa miaka kumi toka sasa na pia hata kuzidi.

Hii ya kukurupuka kwa miaka 2 mitatu tokea 2005 mpaka leo hii haijawahi kuwaletea matokeo chanya.

Hizi siasa za kiuanarakati hazijazaa matunda yoyote zaidi ya kuwaumiza na kuwaketea maumivu makali.

Misemo inasema usiangalie ulipoangukia bali angalia ulipotelezea kisha ukaanguka.

Kwa kipindi hiki upinzani umeanguka sana tena zaidi ya sana. Wanachopaswa kufanya ni kutafuta wapi wanakosea! Kuibiwa kura nalo ni makosa makubwa sana sana tena sana, kwa nini uibiwe kura? Jiulize kisha upate jibu nifanye nini nisiibiwe kura.

Kwa nini mhasimu wangu kapata kura? Hata hio moja unatakiwa ujiulize kwa nini??

Kisha kupata jibu na kulifanyia kazi...

Ila wajue tuu tuliopo kwenye hii mitandao ya kijamii ni wachache mno kuliko uma ulio nje ya utatawazi je wamewafikia???

Wafanyeje ili wawafikie ilihali utawala uliopo hauwapi wepesi wa kuwafikia. Wakiisha kupata majibu hayo haitakua ngumu sana kuzungumza lugha iliotofauti na sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Izo pesa za kufungua matawi kisha wayalinde watatoa wapi wakatai hawana pesa?
Walipokuwa na pesa mliwashauri waka kataa sasa iweje leo ambapo hawana pesa.
Inabidi wakazitafute huko nje sasa. Kwa sasa wana kisingizio kizuri na inaweza kuwa rahisi kupata ‘pesa za huruma’

Yale mawazo kwamba siasa sio majengo na kwamba CHADEMA ipo mioyoni mwa watu yanapaswa kuangaliwa upya
 
Hata Kama Wapizani wakaunza orgaization hadi kwenye mabalozi wa Nyumba Kumi na Wakaungana wote ikifika 2025 kama Mfumo ni huu huu wajue Hata Kura Moja ya Urais Hawataipata. Ni Hivi Hauwezi Itofautisha CCM na Serikali/Dola na Ushin d w
Umeongea point ya muhimu sana..................

Ikiwa mfumo Wa utawala utabaki kama ulivyo, hata kama atatokea kiongozi Wa upinzani, akapendwa na watanzania wote na CCM ikachukiwa na kutopewa kura na mtanzania yeyote..............

Bado tu CCM atapewa ushindi, dawa ni moja tu kwa sasa, tutumie nguvu zetu zote na wakati wetu wote katika kudai KATIBA MPYA na TUME HURU YA UCHAGUZI
 
Siasa wanazofanya wapinzani ndio zinazowafanya warudi nyuma hatua kumi huo Ushauri wako hawawezi kuchukua Hata kidogo kifupi Ni chama ambacho akipendi Ushauri wao wanaamini chama Chao Ni kisafi na kinaongozwa na Mungu,Wanachama wake Ni malaika na ndio maana akijawahi kujirekebisha au kujitathimini na ndio maana walishindwa uchaguzi wanajifichia kwenye kichaka Cha kuibiwa kura.CCM pamoja na kuwa Ni chama tawala lakini kina tabia ya kujitathimini na kufanyia kazi mapungufu yao Sasa CHADEMA ambacho hata madaraka akina lakini wanajiona malaika hiv unazani kitakuwa kina maisha marefu?
 
Kabla ya kuwashauri Wapinzani mshaurini kwanza Jiwe atenganishe ccm na vyombo vya dola arudishe mikononi mwa wanachama.
 
Back
Top Bottom