Nini kifanyike endapo nyumba yako imeshika moto usiku mkiwa ndani

unapojenga nyumba yako binafsi jaribu kuweka escaping root ya siri ambayo ni wewe, mkeo au yeyote mkubwa ndani ya nyumba ndio mtakuwa mnaijua..

Jitahidi nyumbani kwako kuwa na fire extinguisher kubwa na medium na hakikisha watu wote kuanzia dada wa kazi na watoto wanajua namna ya kutumia, jitahidi kufanya fire drills nyumbani kwako na kuwatrain namna ya kutumia fure extinguisher.

Ukiwa uko vizuri funga fire suppression system ndani, joto likifika degree kadhaa vinafyatuka na kuanza kuuzima huku wazimamoto wanasubiriwa..

Kwa wale wenye madirisha yetu haya ya nondo au hizi grills, jitahidi ndani kuwe na hydraulic jack na ikitokea dharula piga jack dirisha okoa walio ndani kwenye hiyo njia..

Kama unaweza kujilinda na vibaka achana na hii minondo na machuma kwenye madirisha yako weka vioo tu kwenye dharula kinavunjwa tu, milango tuachane na hii mininga na mageti baadala yake tumieni MDF kwenye dharula teke moja unatoka nao tu..

Mungu mwenyezi mwingi wa rehma atuepushe na majanga kama haya na amfanyie wepesi majeruhi apone haraka na awape pumziko jema marehemu.
Safi kaka familia za kibongo hata mtu awe na uwezo wa kifedha kuweka tu hose reel nyumbani mtihani, kuna fire alarm kifupi kuna mengi ngoja niuandae uzi vizuri tuzidi pashana habari
 
Kama hiki ni cheap tu
 

Attachments

  • Screenshot_2020-08-25-17-58-07-785_com.alibaba.aliexpresshd.jpg
    Screenshot_2020-08-25-17-58-07-785_com.alibaba.aliexpresshd.jpg
    102.3 KB · Views: 1
Jenga underground exit way ambayo itakua connected kwenye kila chumba so kikinuka unazama underground unasepa kiulaini kama le professor na crue lake kwenye Series ya Money heist.
 
.... ila vibaka sasa Victoire wanaweza kuhamia kufanya party kila week au mwezi

Tatizo zile nondo kwenye madirisha. Nadhani ni muhimu nyumba iwe na milango mitatu. Moto ukianzia sebleni mnatokea milango mingine. Milango mingine isitokee sebleni.
Pia huu mfumo wa kuweka nondo madirishani inabidi tuache.
Maana ukitokea moto kutoka ni haiwezekani.
 
Moto ukitokea ghafla kwenye harakati za kujinasua unatakiwa ujimwagie maji mwili mzima huku ukiwa umevaa nguo nzito nzito. Sasa namna hii inabidi uwe 'sharp' hata kuwavalisha wengine na kisha kuwamwagia maji walowane chapachapa halafu ndo unatafuta njia ya kutokea utapita kwenye moto bila ya madhara makubwa mwilini.
Kama nguo umechelewa unavaa hata shuka au blanketi au godoro lakini sharti liwe limelowa chapachapa ,viatu pia muhimu.
Hili mmelizungumzia wajumbe wengi lkn mmesahau suala la moshi linakunyima pumzi na kushindwa kuona mbele je ktk hili unafanyeje?
 
Lakini wiring si huwa nyaya zinapita juu kwenye mbao halafu zingine zinapita ndan ya ukuta.kama za kwenye hizi socket za taa pamoja na zile za kuchomeka external cable sijui na vingine ..?
Si ndo hivyo unavyosema ndo ilivyo ,
Yaani kuna nyaya lazima zipite juu kwenye mbao na zingine zipite ukutani .

Ila kama unamaanisha main switch iwe nje kwenye kichumba hiyo ndo itakuwa mbaya zaidi.maana kuutoa umeme kutoka kwenye main switch kwenye hicho kichumba nje kuuweka tena ndani ni balaa .
Na hizo nyaya hapo katkati itabidi ufunge ma nguzo mkuu ama ?
Badala ya darini zinapita sakafuni nyumba nyingi asaiv zinapigwa wiring kwa style hiyo
 
.... ila vibaka sasa Victoire wanaweza kuhamia kufanya party kila week au mwezi
Yote hiyo ni sababu ya umaskini,vijana ni wengi kuliko wazee na halafu watu wanaambiwa waendelee kuzaa katika dimbwi hili la umaskini. Vicious circle.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Ulichoandika ni ukweli mtupu ndiyo maana nyumba zimekuwa na nondo chungu nzima milangoni na madirishani utadhani uko lupango.

Yote hiyo ni sababu ya umaskini,vijana ni wengi kuliko wazee na halafu watu wanaambiwa waendelee kuzaa katika dimbwi hili la umaskini. Vicious circle.
 
Siku hizi kuna design ya madirisha ya nondo au flat bars ya kufungua kwa ndani na show yake haina tofauti na lile fixed. Madirisha ya vyumba kadhaa yanaweza kuwa ya kufungua nusu hiyo nondo
 
Tatizo zile nondo kwenye madirisha. Nadhani ni muhimu nyumba iwe na milango mitatu. Moto ukianzia sebleni mnatokea milango mingine. Milango mingine isitokee sebleni.
Pia huu mfumo wa kuweka nondo madirishani inabidi tuache.
Maana ukitokea moto kutoka ni haiwezekani.
Wengi wanaweka nondo madirishani sababu ya kuhofia wizi hasa huku kwetu uswahilini,
Maana licha ya kuweka ndondo lakini bado watu wanaibiwa hivi hivi, Kidukulilo aliwahi kuleta uzi akasema kuweka nondo ni uoga wa maisha lakini kiukweli ndio hali halisi ya jamii yetu kubwa,
Kiusalama si nzuri kwa majanga ya moto yanapotokea
 
Tatizo zile nondo kwenye madirisha. Nadhani ni muhimu nyumba iwe na milango mitatu. Moto ukianzia sebleni mnatokea milango mingine. Milango mingine isitokee sebleni.
Pia huu mfumo wa kuweka nondo madirishani inabidi tuache.
Maana ukitokea moto kutoka ni haiwezekani.
Tunaweka Nondo kwa sababu ya wezi
 
Nenda kwenye maplastic unayoifadhia maji kajimwagie yote afu wakati moto unapambana kukausha maji uliyojimwagia we unapita kininja katikati ya moto
Ila kama hii mbinu ya kininja vile?. Ongezea hapo hapo vaa kabisa manguo mazito mazito,ikiwezekana jifunge blanket,halafu jitumbukize kwenye jaba la maji au jifungulie bomba,ukiwa unejifunga hilo blanket au koti,ikulowanishe tepetepe,halafu toka
 
Mimi nadhani ni muoga sana, chumbani kwangu tuliacha nafasi ndogo ya mtu kupita tukaweka mlango usio na komeo na tukapaka rangi vizuri hata ukiwa nje huwezi jua kama pale ni mlango ambao likitokea lolote mtu anapiga teke unafunguka.

Vyumba vyote nimetoa funguo na nimewaambia watoto likitokea lolote wakimbilie chumbani kwangu.

Mwisho wa yote tusisahau Muomba Mungu atuepushe maana kama ilipangwa ufe kwa moto haijalishi umechukua tahadhari gani utakufa tu
Kibaya zaidi msipokuwepo home mlango wa chumban mnafunga.. sasa sijui majanga yanatokea mkiwepo tuu???
 
Kitu kingine ni kuweka mlango wa dharura kwenye dirisha. Unaweka kamlango kadogo kwenye grili labda la chumba cha baba na mama na unalifunga na kakufuli kadogo ambako kakipigwa hata nyundo kanaachia.Watu wote wambiwe ikitokea dharura wakimbilie kwenye hicho chumba.
kuna nyumba nilipanga kulikuwa na hako kadirisha bhana..WEZI waliniibia mara 2 kwa kupitia kwenye hiko kidirisha..cjui walijuaje WASHENZI wale...ilibidi nimwambie baba mwenye nyumba aniruhusu niuchomelee tu hako kamlngo ka dirishan
 
Jenga underground exit way ambayo itakua connected kwenye kila chumba so kikinuka unazama underground unasepa kiulaini kama le professor na crue lake kwenye Series ya Money heist.
Huu ushauri unawafaa akina Mo sio sisi akina Mwamedi.
 
Tatizo zile nondo kwenye madirisha. Nadhani ni muhimu nyumba iwe na milango mitatu. Moto ukianzia sebuleni mnatokea milango mingine. Milango mingine isitokee sebleni

Pia huu mfumo wa kuweka nondo madirishani inabidi tuache.
Maana ukitokea moto kutoka ni haiwezekani.

Tuna shida mbili tunazojaribu kukabiliana nazo: risk ya moto na ya intrusion ya vibaka. Solution muafaka inabidi izingatie hizi risks mbili. Probability ya kutembelewa na vibaka ni karibu 100%. Probability ya nyumba kushika moto, under normal circumstances, is far less than 100%.

Kwa sababu ya uhalisia huu, homeowners lazima wataweka nondo kuifanya intrusion ya vibaka kuwa ngumu, huku wakikubali kubeba kiasi fulani cha risk ya kushindwa kutoka pindi nyumba zikishika moto. Ili kupunguza hiyo risk ya kuteketea kwa moto ukiwa ndani, umuhimu wa kuwa na more than one exit door na vifaa vya kusaidia kudhibiti moto unakuwa bayana!
 

Similar Discussions

22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom