Kuna habari nimezisikia kutoka kwa watu mbali mbali kwamba mtu anapokufa, akazikwa zile siku tatu yaani siku alipozikwa unahesabua ya kwanza unaongeza siku zingine mbili anakuwa bado yupo duniani anatembea tembea, na anamfuata yule mtu aliyekuwa anampenda sana au wanaelewana kama ni mchana anaingia ndani anamwangalia hasemi kitu, na wanasema mtu huyo uso wake huwa unan'gaa sana huwezi kumuona vizuri, anaondoka siku ya pili anarudi usiku anakuita kwa jina akijua umesikia anakwambia njoo nje ukikataa anakwambia nimekuja kukuchukua ukikataa anakwambia basi, endapo utakubali mnaondoka mnaongea mkifika njiani anakwambia au rudi tu ukirudi kesho yake unakufa. Sasa kwa wale ambao wanajua mila hizi na sio waoga na kwao ni kitu cha kawaida akisikia anaitwa anamwambia njoo ndani anakaa wanaanza kuongea anampa maagizo fulani ambayo hakumwambia na mambo mengine anaaga anaondoka anamwambia hutaniona tena duniani nimekuja kukuaga.
Ila aliyeniambia anasema hizi mila zipo sana kwa kabila la Wapare wale wazee wa siku nyingi wanajua na wanaona ni kitu cha kawaida mi nilishidwa kuelewa na mtu akifa asipokuja huwa wanuliza mbona fulani hajaja kuaga, au wanamuuliza yule aliyekuwa rafiki yake fulani ameshakuja kukuaga?
Naombeni kama kuna mtu mewahi kusikia hiki kitu au anajua atuelezee zaidi.
Ila aliyeniambia anasema hizi mila zipo sana kwa kabila la Wapare wale wazee wa siku nyingi wanajua na wanaona ni kitu cha kawaida mi nilishidwa kuelewa na mtu akifa asipokuja huwa wanuliza mbona fulani hajaja kuaga, au wanamuuliza yule aliyekuwa rafiki yake fulani ameshakuja kukuaga?
Naombeni kama kuna mtu mewahi kusikia hiki kitu au anajua atuelezee zaidi.