Nini hutokea baada ya kufa?

Joyceline

JF-Expert Member
Jan 9, 2009
1,010
166
Kuna habari nimezisikia kutoka kwa watu mbali mbali kwamba mtu anapokufa, akazikwa zile siku tatu yaani siku alipozikwa unahesabua ya kwanza unaongeza siku zingine mbili anakuwa bado yupo duniani anatembea tembea, na anamfuata yule mtu aliyekuwa anampenda sana au wanaelewana kama ni mchana anaingia ndani anamwangalia hasemi kitu, na wanasema mtu huyo uso wake huwa unan'gaa sana huwezi kumuona vizuri, anaondoka siku ya pili anarudi usiku anakuita kwa jina akijua umesikia anakwambia njoo nje ukikataa anakwambia nimekuja kukuchukua ukikataa anakwambia basi, endapo utakubali mnaondoka mnaongea mkifika njiani anakwambia au rudi tu ukirudi kesho yake unakufa. Sasa kwa wale ambao wanajua mila hizi na sio waoga na kwao ni kitu cha kawaida akisikia anaitwa anamwambia njoo ndani anakaa wanaanza kuongea anampa maagizo fulani ambayo hakumwambia na mambo mengine anaaga anaondoka anamwambia hutaniona tena duniani nimekuja kukuaga.
Ila aliyeniambia anasema hizi mila zipo sana kwa kabila la Wapare wale wazee wa siku nyingi wanajua na wanaona ni kitu cha kawaida mi nilishidwa kuelewa na mtu akifa asipokuja huwa wanuliza mbona fulani hajaja kuaga, au wanamuuliza yule aliyekuwa rafiki yake fulani ameshakuja kukuaga?

Naombeni kama kuna mtu mewahi kusikia hiki kitu au anajua atuelezee zaidi.
 
Kilambi nadhani hujanielewa, second chance ni tofauti na hii story yangu, second chance ni roho ya mtu aliyekufa inaingia kwa mtu mwingine anaanza kuishi tena. Lakini hii ni tofauti nimesema marehemu ndani ya siku tatu anakuja kuaga wapendwa wake au mpendwa wake then basi anakuwa amekufa moja kwa moja kama watu wengine hataonekana tena anaonekana ndani ya hizo siku tatu za mwanzo tu. nadhani umenilewa.
 
mimi sijawahi kusikia stori za namna hiyo ila mtu bwana akiisha kufa huwa amekufa,roho yake hutengana na mwili kabisa na kwenda mahali ambapo mwenyezi ajuaaye mambo na siri za binadamu amemuandalia kutokana na vile huyo jamaa alivyoishi hapa duniani,akisubiri ile hukumu yamwisho,aidha kwenda kukaa kwenye pepo ya mungu au jehanamu ya moto.

hili suala la kutembe tembea kwa huyo aliyekufa si kweli,inawezkana ni roho za mizimu au mapepo zinazofaya kazi ya kuwatembelea ndugu au rafiki za huyo marehemu aidha zinatafuta mahali pa kuingia na kukaa au kuvuruga amani katika ukoo au jamii ile.
 
Imani yangu ni kwamba mtu akishakufa hana mawasiliano tena na duniani. Hiyo roho yake yaweza kwenda sehemu ambayo wanadamu hatuijui na hatunauhakika nayo may be peponi (hypothetical/belief).
 
mtu akifa ndiyo mwisho wa mchezo, consciousness inaisha na entropy level inaenda zero.

Ni vigumu kuwa na hakika lakini kwa yanayojulikana sasa hili ndilo linaloonekana kutokea.
 
Hata mimi naamini baada ya kufa mawasiliano na duniani yanakatika. Lakini hiki chanzo changu cha habari kiliniambia vitu vya kushangaza nilimtolea mifano, biblia inavyosema kuhusu wafu yeye akasisitiza kikwao hicho kitu kipo na kinaendelea kutokea mpaka vizazi vya sasa hivi, nikasema au ni mzimu wa marehemu huwa unarudi au? yani alinielezea vitu vingi nikashangaa. ndo maana nikauliza kama kuna mtu amewahi kusikia hizi habari
 
Mnapoambiwa ponda mali kufa kufa kwaja ,mnzania nini ,si mnaona mafisadi wanavyokomba ,wanajua wakifa ndio imetoka ,na haya mambo ya mapenzi na nini yote haya ,alizianeni hapa hapa duniani ukiwa hai ,usiingie na tamaa ya kwenda peponi ni moto mtindo mmoja ,yaani embu jipime ujione ka unaingia peponi ,uone kama utaenda kweny kundi la kula uhondo ,yaani wewe hapa unatakiwa uwe mtu wa kuvuruga tu ,unaponda kikweli ila kama mswalihina basi iwe hivyo.

Hiyo huyo mdada mada yake inaulizia kuhusu maghost na mila flani flani ambazo amezisikia kuwepo hapa Tanzania aidha naweza kusema hakuna kitu hicho,ila inakuwa ni njozi na njozi zinatafsirika ,kivyakevyake na zinakuwa na ukweli kwa kiasi fulani na zoko njozi za kuchoka hizi hazina maana yeyote ni kukuliwaza usingizini tu.
 
...anamfuata yule mtu aliyekuwa anampenda sana ...siku ya pili anarudi usiku anakuita kwa jina akijua umesikia anakwambia njoo nje ukikataa anakwambia nimekuja kukuchukua ukikataa anakwambia basi, endapo utakubali mnaondoka mnaongea mkifika njiani anakwambia au rudi tu ukirudi kesho yake unakufa. ...anampa maagizo fulani ambayo hakumwambia na mambo mengine ...hizi mila zipo sana ...wale wazee wa siku nyingi wanajua ...fulani hajaja kuaga, au wanamuuliza yule aliyekuwa rafiki yake fulani ameshakuja kukuaga?...

Dada yangu Joyceline, haya mambo ni mambo ya Hadithi za kusadikika. Myth. Hayana ukweli hata kidogo, nimambo ya imani za kijadi, katika kuendeleza dhulma na unyang'ani katika koo husika.

Kwanza nikufahamishe jambo moja, si kabila na koo za kipare tu zenye tabia hizi. Hata hizo nchi zilizo endelea kuna jamii zenye kuamini jambo hilo la maiti kurudi tena na ikiwezekana kuondoka na mmoja wa wanadungu, hususani yule anaye mpenda sana. Ngano za kale (Myth) ambazo watu wengi siku hizi wanazifuata bila kujuwa kuwa ni urithi wa kipagani, ni huu uvaaji wa nguo nyeusi msibani.

Wapagani wa kale waliamini kuwa ukivaa nguo nyeusi kwenye msiba basi maiti ya mtu yule haitakuona itakapo rudi duniani. (kwa mtindo huo ulio ueleza hapo juu). Imani hii ikapelekea watu wengi kuvaa nguo nyeusi wakiamini kuwa hawata onekana pale maiti itakapo kuja kutaka kuambatana nayo. Hii ni sawa na kusema kuwa paka mweusi ni nuksi, au ukisikia sauti ya bundi ni uchuro, nk, nk.

Tukirejea kwenye suala la maiti kuja kutoa maagizo fulani fulani, hii ni aina ya dhurma, ninasema dhurma kwa sababu suala la maiti au mfu kuja kutoa maagizo mara nyingi huyo mfu umtokea mzee wa ukoo au mtu ambaye anajuwa kabisa akisema hata pingwa. Na mara nyingi maagizo hayo uhusiana na mambo ya urithi katika njia ya kuwadhurumu wenye haki ya kurithi.
Unavyo fikiria mzee wa koo fulani au huyo anaye semekana kuwa ni kipenzi chake akisema kuwa mfu fulani kanijia na kanifahamisha jinsi kadhaa wa kadhaa, ni nani wa kupinga...!? na kama ni kweli wafu huja kutoa maagizo kwa nini wasije au wasitokee kwenye kikao cha mazishi na kwanini wasubiri mpaka wazikwe? Na kama ni kweli kwa nini wasitokee wakaonekana na wana ndugu wote. Kwa nini hawe mzee fulani au mtu moja fulani tu!? Huu ni utapeli uliochanganyika na wizi.

Aliye kufa amekufa dadangu, yatakayo kumbukwa ni yale matendo yake aliyoyafanya hapa duniani tu basi.

Ukisikia siku nyingine wazee wakidai fulani hajaja kuaga ujuwe wamesahaulika kwenye ulaji (Urithi wa mali). Lakini wakipewa chochote kitu kutoka kwa wafiwa, hutasikia hayo maneno ya mfu hajaja kuaga.
 
Dada yangu Joyceline, haya mambo ni mambo ya Hadithi za kusadikika. Myth. Hayana ukweli hata kidogo, nimambo ya imani za kijadi, katika kuendeleza dhulma na unyang'ani katika koo husika.

Kwanza nikufahamishe jambo moja, si kabila na koo za kipare tu zenye tabia hizi. Hata hizo nchi zilizo endelea kuna jamii zenye kuamini jambo hilo la maiti kurudi tena na ikiwezekana kuondoka na mmoja wa wanadungu, hususani yule anaye mpenda sana. Ngano za kale (Myth) ambazo watu wengi siku hizi wanazifuata bila kujuwa kuwa ni urithi wa kipagani, ni huu uvaaji wa nguo nyeusi msibani.

Wapagani wa kale waliamini kuwa ukivaa nguo nyeusi kwenye msiba basi maiti ya mtu yule haitakuona itakapo rudi duniani. (kwa mtindo huo ulio ueleza hapo juu). Imani hii ikapelekea watu wengi kuvaa nguo nyeusi wakiamini kuwa hawata onekana pale maiti itakapo kuja kutaka kuambatana nayo. Hii ni sawa na kusema kuwa paka mweusi ni nuksi, au ukisikia sauti ya bundi ni uchuro, nk, nk.

Tukirejea kwenye suala la maiti kuja kutoa maagizo fulani fulani, hii ni aina ya dhurma, ninasema dhurma kwa sababu suala la maiti au mfu kuja kutoa maagizo mara nyingi huyo mfu umtokea mzee wa ukoo au mtu ambaye anajuwa kabisa akisema hata pingwa. Na mara nyingi maagizo hayo uhusiana na mambo ya urithi katika njia ya kuwadhurumu wenye haki ya kurithi.
Unavyo fikiria mzee wa koo fulani au huyo anaye semekana kuwa ni kipenzi chake akisema kuwa mfu fulani kanijia na kanifahamisha jinsi kadhaa wa kadhaa, ni nani wa kupinga...!? na kama ni kweli wafu huja kutoa maagizo kwa nini wasije au wasitokee kwenye kikao cha mazishi na kwanini wasubiri mpaka wazikwe? Na kama ni kweli kwa nini wasitokee wakaonekana na wana ndugu wote. Kwa nini hawe mzee fulani au mtu moja fulani tu!? Huu ni utapeli uliochanganyika na wizi.

Aliye kufa amekufa dadangu, yatakayo kumbukwa ni yale matendo yake aliyoyafanya hapa duniani tu basi.

Ukisikia siku nyingine wazee wakidai fulani hajaja kuaga ujuwe wamesahaulika kwenye ulaji (Urithi wa mali). Lakini wakipewa chochote kitu kutoka kwa wafiwa, hutasikia hayo maneno ya mfu hajaja kuaga.

asante nimekuelewa sana, nilikuwa napata utatanishi.
 
Joyceline,
Acha kutazama na kuamini kipindi cha - Ghost Whispers!..

siyo kwamba naamini , mimi ni mkristo na niko makini na imani yangu sana, kilichopelekea kuandika haya ni hivi,

Last week nililala kwenye msiba nikalala na mfiwa sasa tumelala chini mimi nilikuwa karibu yake,usiku nikasikia anaongea kama anajibishana na mtu, anaitika anasema sawa, nikajua anaota asubuhi nikamwuliza ndo akaanza kunipa hizo habari fulani kaja kuniaga kwamba kuna maagizo alikuwa anapewa.
 
Mpendwa Joyceline,
Kwa imani yangu na nahakikishiwa na maandiko matakatifu kuwa mtu akishakufa ni mwisho wa mchezo. Hayo mengine yanayoweza kutokea ni michezo ya kuigiza tu, na yawezekana ni roho chafu toka kuzimu. Hakuna mawasiliano kati ya mfu na aliye hai. Biblia inasema; 'Kama wanadamu walivyowekewa kufa mara moja, baada ya kufa hukumu' Waebrania 9:27.


Hebrews 9:27 (New International Version)
27Just as man is destined to die once, and after that to face judgment,
[/B][/B]
 
Anachoongea joyceline kinauwezekano kipo, ila sema watanzania wengi tunapenda kuletewa chakula kilichotayari kuliwa kuliko kwenda kuanza kukiandaa shambani as seed mpaka ukipike mwenyewe ndo uanze kula,namaanisha watanzania wavivu wa kufanya tafiti, na ndo maana vitu vikitoka nje ya nchi tunavishangaa sana
 
Kuna habari nimezisikia kutoka kwa watu mbali mbali kwamba mtu anapokufa, akazikwa zile siku tatu yaani siku alipozikwa unahesabua ya kwanza unaongeza siku zingine mbili anakuwa bado yupo duniani anatembea tembea, na anamfuata yule mtu aliyekuwa anampenda sana au wanaelewana kama ni mchana anaingia ndani anamwangalia hasemi kitu, na wanasema mtu huyo uso wake huwa unan'gaa sana huwezi kumuona vizuri, anaondoka siku ya pili anarudi usiku anakuita kwa jina akijua umesikia anakwambia njoo nje ukikataa anakwambia nimekuja kukuchukua ukikataa anakwambia basi, endapo utakubali mnaondoka mnaongea mkifika njiani anakwambia au rudi tu ukirudi kesho yake unakufa. Sasa kwa wale ambao wanajua mila hizi na sio waoga na kwao ni kitu cha kawaida akisikia anaitwa anamwambia njoo ndani anakaa wanaanza kuongea anampa maagizo fulani ambayo hakumwambia na mambo mengine anaaga anaondoka anamwambia hutaniona tena duniani nimekuja kukuaga.
Ila aliyeniambia anasema hizi mila zipo sana kwa kabila la Wapare wale wazee wa siku nyingi wanajua na wanaona ni kitu cha kawaida mi nilishidwa kuelewa na mtu akifa asipokuja huwa wanuliza mbona fulani hajaja kuaga, au wanamuuliza yule aliyekuwa rafiki yake fulani ameshakuja kukuaga?

Naombeni kama kuna mtu mewahi kusikia hiki kitu au anajua atuelezee zaidi.

..Je na wewe unataka ukishaundei uzagaezagae mitaani? siku hizi mgambo wa city wanakamata wazururaji ohoo usije ukashikwa
 
..Je na wewe unataka ukishaundei uzagaezagae mitaani? siku hizi mgambo wa city wanakamata wazururaji ohoo usije ukashikwa

mimi sitaki, lakini hazururi aanaenda kwa mlegwa tu na mlegwa ndo anamuona
 
Mi shetani nimemwona amekaa kama picha iliyoko kwenye negative ,ni kutishana tu.
 
Mimi fikra zangu huwa zinanipelekaga kwingine kuhusu kifo.

Isije tukaja kujilaumu kwanini hatukujiuaga mapema ili tufaidi raha ambazo pengine wenzetu waliofariki wanazipata,regardless matendo yao yalikuaje hapa duniani.

Nafikiri kunamaisha mazuri/bora kwa wote baada ya kufa.
 
Joycline kwa sababu wewe ni mkristo soma sana bible mambo yote yako huko.
Mtu akifa amekufa na hana ushirika tena na walioko duniani, swala la mtu aliyekufa kuja kuaga kwa muda wa siku tatu au zozote hilo halipo kabisa.

Shetani ni mjanja sana na hutumia vitu vingi kuhalalisha uongo wake na kuwapotosha watu. Kimsingi huyo dada alikuwa anaongea naweza kusema na mizimu au pepo kama alivyosema mmoja wetu.

Mara nyingi katika kabila mbalimbali au koo au familia mambo ya mizimu yametawala sana kila jambo linalotokea watu husika wanauliza mizimu, kwa kutambika na kadhalika. Huu ni uomgo mkubwa.

Mizimu au mzimu ni pepo ambalo linavaa sura ya mtu aliyekufa na kuanza kufuatilia watu aliokuwa nao karibu au familia. Kimsingi huyo pepo kazi yake ni kuwafanya watu wa mhusika kuona kwamba wanaongea au wanapata maelekezo fulani toka kwa aliyekufa, mwisho huamini na yale mambo wanayoambiwa na pepo huyo huwa hutokea. Hii yote ni machukizo mbele za Mungu, mtu akifa amekufa na hana mawasiliano tena duniani.

Nakusihi usiamini vitu hivyo hata siku moja hata kama una ndugu yako amekufa akikujia kwa ndoto au vyovyote vile kemea kwa Jina la Yesu hatakuja tena.
 
Back
Top Bottom