Nini hukumu ya mtu anayeshindwa kurudi kwao kushiriki katika shughuli za kifamilia kama sherehe au misiba?

BabaMorgan

JF-Expert Member
Dec 18, 2017
4,045
10,476
Katika hali ya utafutaji imesababisha watu kutoka katika mikoa yao ya asili na kwenda mikoa ya mbali au hata nchi tofauti na walikozaliwa na kama ilivyo kwenye kutafuta wapo waliofanikisha kupata huku wengine wakiwa bado wanatafuta.

Kwa mtu ambaye yupo mbali na kwao panapotokea msiba au sherehe nyumbani kwa kawaida anatarajiwa na analazimika kushiriki kwa kuwepo eneo la tukio kwenye sherehe sio tatizo kwa kuwa linakuwa tukio lilopangwa lakini kwenye msiba inakuwa ni changamoto kwa kuzingatia wengi wetu hatuna mazoea ya kuweka akiba kwa ajili ya matukio ya dharura sasa hapa mtu ujikuta akiwa na majukumu mawili mosi ni kuchangia gharama za mazishi pili ni kushiriki kwa kuwepo.

Inapotokea mtu kushindwa kushiriki kwenye sherehe au msiba kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake katika tamaduni na Mila za kabila nini hukumu yake?
 
Mkoa gani huo?
km Kilimanjaro sasa hivi yatatoweka
watu kila siku wanafariki na wanazikwa huko mashambani sasa unakuta misiba 5 wiki moja utahudhuriaje misiba yote? hata iwe kwa miezi mitatu
haya huko mashambani kila kona nyumba hazina watu kabisa nje makaburi hata kupangisha walimu au manesi hawataki
Na mikoa mingine sasa waelimike popote mtu azikwe kupunguza hizo sintofahamu za miaka ya giza, eti lazima uwepo angalau kwa sura wakati Corona haitaki mikusanyiko
 
Katika hali ya utafutaji imesababisha watu kutoka katika mikoa yao ya asili na kwenda mikoa ya mbali au hata nchi tofauti na walikozaliwa na kama ilivyo kwenye kutafuta wapo waliofanikisha kupata huku wengine wakiwa bado wanatafuta.

Kwa mtu ambaye yupo mbali na kwao panapotokea msiba au sherehe nyumbani kwa kawaida anatarajiwa na analazimika kushiriki kwa kuwepo eneo la tukio kwenye sherehe sio tatizo kwa kuwa linakuwa tukio lilopangwa lakini kwenye msiba inakuwa ni changamoto kwa kuzingatia wengi wetu hatuna mazoea ya kuweka akiba kwa ajili ya matukio ya dharura sasa hapa mtu ujikuta akiwa na majukumu mawili mosi ni kuchangia gharama za mazishi pili ni kushiriki kwa kuwepo.

Inapotokea mtu kushindwa kushiriki kwenye sherehe au msiba kwa sababu zilizo nje ya uwezo wake katika tamaduni na Mila za kabila nini hukumu yake?

Ndo maana hashiriki kwa sababu ya Hii mitazamo yenu
 
km Kilimanjaro sasa hivi yatatoweka
watu kila siku wanafariki na wanazikwa huko mashambani sasa unakuta misiba 5 wiki moja utahudhuriaje misiba yote? hata iwe kwa miezi mitatu
haya huko mashambani kila kona nyumba hazina watu kabisa nje makaburi hata kupangisha walimu au manesi hawataki
Na mikoa mingine sasa waelimike popote mtu azikwe kupunguza hizo sintofahamu za miaka ya giza, eti lazima uwepo angalau kwa sura wakati Corona haitaki mikusanyiko
Fikra za walio wengi kutoshiriki ni kama umeamua kujitenga na upelekea mtu kupewa tuhumu za ushirikina kama kuhusika na msiba.
 
km Kilimanjaro sasa hivi yatatoweka
watu kila siku wanafariki na wanazikwa huko mashambani sasa unakuta misiba 5 wiki moja utahudhuriaje misiba yote? hata iwe kwa miezi mitatu
haya huko mashambani kila kona nyumba hazina watu kabisa nje makaburi hata kupangisha walimu au manesi hawataki
Na mikoa mingine sasa waelimike popote mtu azikwe kupunguza hizo sintofahamu za miaka ya giza, eti lazima uwepo angalau kwa sura wakati Corona haitaki mikusanyiko
Huku nilipo uongozi ulipiga marufuku mtu kuzikwa nyumbani ni kosa la jinai mazishi yote yanafanyika makabulini palipotengwa na serikali
 
Imagine upo South Africa huna hata kipande cha passport huna hata mia mbovu msiba unatokea kigoma ama kagera si watakutafutia lawama za bure tu aisee
 
wengine sababu zao za kutokurudi nyumbani zinajulikana na taifa zima mfano Mange Kimambi
 
Back
Top Bottom