Nini hatma ya Uingereza?

Comred Mbwana Allyamtu

JF-Expert Member
Jun 28, 2016
348
847
NINI HATMA YA UINGEREZA?

Na: Comred Mbwana Allyamtu

Duniani huwezi kuzungumzia kile kinachoitwa "ushawishi wa madola makuu duniani" ukaacha kuitaja Uingereza hii ni kutokana na heshima iliyonayo ya kuwa taifa mama la utamaduni wa kileo yani "world English culture" hivyo ushawishi wake ni mkubwa sana katika dunia ikiwa ni pamoja na bala la ulaya, Amerika,Asia, Africa na katika jumuiya kubwa kama NATO, EU na hata UN. Lengo sio kufanya uchambuzi juu ya nafasi ya Uingereza duniani bali ni kutazama hatma yake kwenye Duru za usoni kwa namna ilvyo amua kwa maamuzi ya democracy.

Uingereza leo imeamua maamuzi magumu sana kwa taifa hilo lenye ushawishi mkubwa sana kwa mataifa yenzake 27 sasa ya umoja wa ulaya (EU). Katika Kambi ya wahafidhina waliotaka kujitoa Umoja wa Ulaya ikiongozwa na kiongozi wa chama cha UK Independence Party (UKIP) comred Nigel Farage wanasema sababu za kupambana dhidi ya kuhakikisha Uingereza inajitoa ni kama zifuatazo....

1- Uingereza inapoteza Uhuru wake kwa EU,wanaona kila kinachofanya ndani ya taifa lao yanaamliwa Brussels na siyo Downing 10 street au House of Common,

2- masuala mengi yanayohusiana na Siasa, usalama, uchumi, na utamaduni yanaongozwa na Sera za Ulaya na siyo Uingereza.

3- hulka ya Uingereza ya kutokuwa na sauti ya turufu kiuchumi dhidi ya taifa la Ujerumani ambalo ndio taifa kuu kiuchumi balani ulaya.

4- kudolola kwa uchumi wa Uingereza juu ya kumezwa kwa kile kinachoitwa "european economic zone" yani uchumi wa ulaya kutegemea soko la ulaya.

5- kumezwa kwa hazi ya Uingereza kama Taifa "mornach super power"

6- migogoro ya kisela (policy) ya muda mrefu.

7-Mtikisiko wa siasa za kihafidhina balani ulaya na uingeleza kwa ujumla.

8- sela ya ulaya kuhusu janga la wakimbizi.
Pamoja na sababu zingine ambazo sijazitaja hapo..

Katika Kambi ambayo ilihakikisha Uingereza inaondoka katika jumuiya ya ulaya iliyojulikana kama Brexit au VoteLeave wanaona kuwa
1- taifa lao linamezwa na kupoteza ushawishi wake kama Taifa.
2- ni Sera ya Ulaya kuhusu wakimbizi.

Hizi hoja kwa naman moja au nyingine inaongezea nguvu za kambi ya VoteLeave kupata ushawishi wa kujitoa ulaya.

Kwa upande mwingne wa shilingi ilikuwa na viongozi wa vyama vikubwa wakiongozwa na Waziri mkuu wa sasa wa Uingereza David Cameroon kutoka Conservative, na wahafidhina wa Labour kama Tony Blair, Gordon Brown,Ed Miliband.
pamoja na kiongozi wa chama cha SNP Nicola Sturgeon, pamoja na kiongozi wa chama cha Kijani Green Party Natalie Bennet wote wameweka tofauti zao wanapiga kampeni pamoja kuhakikisha wanazima hasira ya wataka mabadiliko na kuhakikisha uingeleza inabaki katika umoja wa ulaya (EU).

Katika kundi ambalo Wanaongoza kampeni za upande wa VoteRemain, au StrongerIn, BetterIn nk. Wanataja madhara ya Uingereza kujitoa EU kama ifuatavyo....

1-uchumi kuporomoka.

2-kitisho cha usalama kwa raia ndani ya Uingereza.

3- Uingereza kukosa utengamano ndani ya ulaya.

4- kuyumba kwa soko la Taifa na pato kwa ujumla.

Hata hivyo Viongozi wa mataifa mbalimbali wamewaomba Waingereza kutojitoa ndani ya jumuiya ya ulaya (EU) mfano tu ni pale Ziara ya juzi ya Obama balani Ulaya ilikuwa kujaribu kuunga mkono kambi ya David Cameoon, pia viongozi wengine wakubwa tena wenye ushawishi duniani kama Angel Merkel kansela wa Ujerumani, rais François Hollande wa Ufaransa na Justin Trudeau ni miongoni mwa viongozi waliowasihi Uingereza kutojitoa EU.

Yeye Cameron na baadhi ya wanasiasa wa ngazi za juu za serikali yake wamepiga kampeni ya nguvu kuunga mkono upande wa kubaki umoja ya ulaya (EU) lakini pia hata hivyo ndani ya Chama chake Cha kihafidhina(Conservative) wanasiasa wenye nguvu kama aliyekua Meya wa London Boris Johnson, Gove na Ian Duncan Smith pamoja na wabunge wengine walipiga kampeni ya Kutoka yani voteleave.

Sasa wananchi karibu milioni 40 wamepiga kura na karibu asilimia 51% wameamua kura ya kutoka na Upande wa Cameron umeshindwa
Binafsi niliyategemea haya ya uwezekano wa yeye kujiuzulu au kushinikizwa kung'atuka na ndilo lililotokea baada tu ya matokeo kuwa hadharani.

Hata hivyo kitendo cha Kujiuzulu kwa waziri Mkuu kunaweza kuathiri masoko ya hisa zaidi na pia katika negotiation (mjadala wa makubaliano) utakaofanyika kati ya Uingereza na umoja wa Ulaya kuhusu mkakati salama wa pamoja kutokana na namna ya kushirikiana kwa masharti mapya kulingana na Ibara ya "50" ya Mkataba wa EU wa Lisbon.
Ambayo inatoa muelekeo wa taifa iwapo litajiondoa jumuiya ya ulaya (EU)

Watu wengi wanadhani matokeo ya kura ya leo basi ndio Uingereza imetoka moja kwa moja leo. Na ndio sasa hatashilikiana na ulaya
Hapana kuna miaka kama 2 ya makubaliano na namna bora ya kutoka kwenye jumuiya ya ulaya na namna bora ya kushirikiana Ndani ya masaa au siku chache zijazo mawaziri wa mambo ya nje wa nchi wanachama watakutana Makao makuu ya EU Brussels kujadili jambo hilo kwa upana na kisha baadae Wakuu wa nchi za EU wiki ijayo watakutana na Waziri Mkuu wa Uingereza.

Hata hivyo David Cameron wa Uingereza atapeleka taarifa rasmi ya kuwafahamisha kuwa wananchi wa nchi yake wameamua kujitoa.

Hata Hivyo kwa jinsi mataifa tajiri ndani ya EU walivyoudhika wanaweza kuweka maaharti magumu ya ushirikiano ili kukatisha tamaa nchi nyingine wanachama wasiige mfano wa Uingereza wa kutaka kujitoa.

MATOKEO YA UINGEREZA KUJITOA EU

Matokeo haya ya Uingereza kujitoa yanaweza yakazidi kuzusha mgawanyiko wa Dola ya Uingereza(United Kingdom) ikumbukwe kuwa Uingereza imeundwa na dola zingine nne(4) ambazo ni England,Wales,Scotland na Ireland ya Kaskazini.

Hata hivyo Scotland wao wanataka Dola la Uingereza libaki Umoja wa Ulaya Na ni mwaka juzi tu walipiga kura ya maoni ya kutaka nao kubaki au kujiondoa kwenye muungano wa Uingereza.na ndipo David Cameroni alishida kuikomboa Scotland isijiondoe ndani ya Uingereza kipindi hicho viogozi kama Nigel Farage wa chama cha (UKIP) walikiwa katika jukwaa moja la kitetea Scotland kujitenga.

Sasa kwa vile Uingereza imepiga kura ya kutoka inaweza kuchochea hasira za Scotland kujenga hoja ya kura nyingine ya maoni ili itoke kwenye muungano halafu ibaki Umoja wa Ulaya kwa Uhuru kwa kuwa wao wanaona kama vile Uingereza inawafunika na kuwaminya kuamua mustakabali wao.

Pia sasa Uingereza imeondoa nguvu yake ya kibiashara katika bara la ulaya. Ndio maana mpaka sasa salafu ya Uingereza imepolomoka dhidi ya sarafu ya dola ya MAREKANI.

Hata hivyo usalama wa Taifa hilo la Uingereza sasa iko hatalini zaidi kwakuwa haina utengamano na mataifa mengine makubwa ya ulaya kama ujerumani na Ufaransa ambayo kwao usalama ni ajenda kuu na ya msingi sana.

Pamoja na kuongezeka kwa masikitiko na mataifa kadhaa ambayo yameoneshwa kusikitishwa kwa Uingereza kujiondoa yanaweza kuongeza mbinyo mkari na mkubwa ili kuiadhibu Uingereza na kuyatishia mataifa mengine yasifanye uamuzi kama iliyo fanya Uingereza.

Sasa Uingereza itapitia wakati mgumu sana juu ya maamuzi yake hayo sababu dunia ya sasa haiwezi kwenda bila utengamano wa kimataifa na kijumuia

NINI FUNZO LA DUNIA JUU YA MAAMUZI YA UINGEREZA?

Hapa ndio tunaona sasa kuwa alieleta nadharia ya demokrasia Hakuwa na maana mbaya, alitaka kuwakumbusha watu kuwa Demokrasia ni maamuzi ya wengi tu, yawe yana maana au hayana. Na ndio maana kuna msemo huu ambao juzi nilijalibu kueleza kwenye makala yangu ya "Democrasia ni pamoja na kuvumilia ujinga" yani nilisema

Mwl Nyerere au Mwanasiasa gani wa kikazi cha karne ya jana aliwahi kusema "Demokrasia inaweza kupeleka hata chizi Ikulu"

Funzo lake kubwa hapo ni kuwa democrasia ni fimbo ambayo inaweza kuzaa matunda ama mazuri ua mabaya (ulilolitaka na lile usilo litaka)

Labda huelewi, katika democracy hakuna mwenye uhalali wa jambo isipokuwa wengi ndio washindi na ukipinga mawazo ya wengi hata kama ni ya kipumbavu unapingana na demokrasia kwa sababu una kataa ya wengi.

Kwa hiyo, jukumu la la dunia kuheshimu katika demokrasia ni funzo muhimu kwa dunia nzima.

Mfano Uingereza iliweza kuiba kura ili kukidhi matakwa ya watawala ila iliamua kupisha sauti ya wengi isikike bila hata kujali madhara yake japo kuwa hiyo ina madhara makubwa kwa upande mwingine mfano ni kwa Uingereza yenyewe kuamua kijitila moto yenyewe.

Vile vile, ndio maana wasomi wengi duniani hasa wa Uchina wanasema demokrasia inayohubiriwa na Magharibi haifai katika nchi zenye watu wengi wajinga (large number of ignorant citizens) na idadi kubwa ya wenye mihemuko ya kihafidhina ( aggresive of consevatism) kwa sababu ujinga au mihemuko yao inaweza kuamua kupeleka hata chizi Ikulu na hakuna wa kuwapinga kwa sababu wameshaamua na wengi wanapewa.

Aidha, demokrasia katika nchi zenye wajinga wengi na wenye mihemuko mingi sio tu inapeleka wajinga wengi katika vyombo vya maamuzi kama Bunge au ikiru au kuamua mambo mengi ya kitaifa kama hayo ya Uingereza bali inapeleka pia wajinga wachache katika vyombo hivyo.

Nini kitatokea, ikiwa wajinga wengi au wahafidhina wenye misimamo ya mihemuko ni huidhinisha ya kijinga na ya maana kwa wakati tofauti huku wakiyaacha ya msingi kwa mstakabali mpana.

Pamoja na hayo yoyete bado funzo kubwa kwa uamuzi huu wa Uingereza ni lazima viongozi popote duniani waheshimu sauti za wengi

MWISHO

Najuwa jambo hili ni matakwa kwa Uingereza lakin sio uamuzi wenye busara jambo ambalo wahafidhina wa Uingereza wameamua kuikomoa jumuiya ya ulaya kwa uamuzi huu lakini ni maamuzi yenye madhala kwa watu wake.

Pia najua tunatakiwa kujifunza kutoka Uingereza kuheshimu sauti ya watu (democracy) hasa kwa mataifa ya afrika hususani hapa kwetu nyumbani Tanzania.

Japokuwa democracy nayo inachangamoto zake mingi tu Mifano ni hai, madai ya demokrasia hiyo ya wengi ndio umeitia kitanzi mataifa ya Libya, Yemen, Syria na kadhalika.

Nchi ya wajinga wengi na wahafidhina wenye misimamo ya mikari demokrasia ya wengi ni hatari mnooooo sasa wachache wanaohubiri demokrasia sasa hivi lazima wajue katika hii lakile ambalo dunia inakiitaa " mtikisiko wa kidipromasia yaa anga la Uingereza" wengi ndio wamepewa wao kwaiyo haifai kuwalaumu hata kidogo hao wengi.


MY TAKE

Ni kwa sababu hiyo hakuna nchi yoyote duniani iliyopiga hatua kwa kuanza na Demokrasia, haipo kabisa. Demokrasia ni zao la maendeleo yaliyotokana na mifumo ya nje ya Demokrasia. (The theory of democracy)

Ndimi:
Comred Mbwana Allyamtu

+255679555526
+255765026057
mbwanaallyamtu990@gmail.com IMG]https://www.jamiiforums.com/mobile-gallery/43598285107c2b6bf05032f371285186.jpg[/IMG]
 
Wewe ni mchambuzi mahiri, makala yako ni nzuri, yenye lugha rahisi yenye kueleweka.
Vitu muhimu nilivyopata kutoka kwenye hii makala ni kwamba
1. Demokrasia ni hatari kwa taifa lenye wajinga (au watu wenye mihemko) wengi
2. Demokrasia ni hatua ya baadaye kwenye maendeleo, yaani huwezi kufanya taifa liendelee kwa kutumia demokrasia katika hatua za mwanzo (yaani likiwa kwenye umaskini wa aina yoyote)
3. Demokrasia si mfumo sahihi kwa kila jamii (au taifa), demokrasia haifai katika baadhi ya jamii (mataifa) hata kama jamii hizo zimeendelea
 
Back
Top Bottom