Nini hasa chanzo cha bei ya vyakula kupanda zaidi ya mara dufu (inflation)? Nini kifanyike kutunusuru na janga hili kubwa?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
Tunaambiwa kuwa mfumuko wa bei (inflation rate) nchini kwetu bado ni mdogo sana, ni chini ya asilimia 5%! Wao wanauita single digit inflation.

Lakini kwa miezi ya hivi karibuni, bei za vyakula muhimu sokoni vimepanda kwa zaidi ya maradufu. Yaani mfumuko wa bei wa vyakula ni zaidi ya asilimia 50%, yaani ni double digit inflation! Vyakula hivi ni pamoja na vile wanavyotumia watu wa kawaida, walala hoi na waamka hoi. Kwa mfano Unga wa mahindi ni sasa hivi ni Sh 2,000 kwa kilo moja kutoka Sh 1,000 kwa kilo mwezi Julai 2022. Mchele (grade A) umepanda kutoka Sh 1,200 kwa kilo hadi Sh 3,500 - 4,000. Maharage kutoka Sh 1,800 hadi Sh 3,000. Karanga kutoka Sh 2,000 hadi Sh 5,000 na kadhalika.

Hili ni janga la kitaifa kwani hadi kufika msimu ujao wa mavuno, hatujui hali itakuwa vipi. Sasa hivi mwananchi wa uchumi wa kawaida, ni vigumu kula zaidi ya mlo mmoja kwa siku. Hizo kampeni za lishe bora ili kuepusha vijana wetu wa kiume kutegemea nguvu za supu ya pweza, hazitaweza kufanikiwa kwa mazingira kama haya.

Ili kupata ufumbuzi wake tunapaswa kujua chanzo chake hasa ni nini:

1. Je, ni vita ya Ukraine?

2. Je, ni ukame wa msimu uliopita ambao tulishuhudia mafuriko maeneo mbali mbali ya nchi na kusababisha uharibifu wa miundombinu hususani barabara zetu?

3. Je, ni akiba yetu ya taifa ya chakula (Strategic National Grain Reserves) imeshindwa kufidia upungufu uliopo wa chakula nchini kama ilivyo jukumu lake?

4. Je, ni hayo mamisafara ya malori ya urefu wa kilomita 7 kila siku yanayofanywa na wafanyabiashara (middle men, not our peasants) kupeleka chakula chetu kwa nchi jirani waliokuwa na uhaba wa chakula uliosababishwa na lockdowns walizojiwekea wakati wa mlipuko wa covid? Kwa nini sisi ambao hatukuji lockdown ndiyo tupate shida?

5. Je, ni kwa sababu ya kupanda kwa bei ya mafuta ya petroli na dizeli iliyosababishwa na sisi kususia kununua mafuta hayo toka Urusi, ili kuwaunga mkono West Europe ambao wao hata hivyo wanaendelea kununua gesi kutoka Urusi? West Europe wanalalama na kuishutumu sana Urusi kwa kuwabania gesi yao hasa kwenye kipindi hiki cha kuelekea winter. Kwa nini na sisi au kama East Africa Union tusiwe na msimamo kama wa Uchina na India wa kununua mafuta haya kutoka Urusi ili kuepukana na balaa hili la kupanda kwa bei ya vyakula. Mseveni na Ruto wameonesha dhamira hii.

6. Je, mfumuko huu wa bei unauhusiano na upandishaji wa mishahara ya watumishi wa umma? Jee itakuwaje pale serikali itakapopandisha mishahara ya taasisi binafsi hivi punde? Awamu iliyopita iliogopa sana kupandisha mishahara hii kwa kuogopa kuleta mfumuko wa bei kama zilivyo kanuni za kiuchumi.

Nini kifanyike kinategemea na majibu ya maswali hayo na mengine mtakayopendekeza.
 
... mavuno msimu uliopita hayakuwa ya kuridhisha; vita vya Ukraine ni imechangia; wakulima wameruhusiwa kuuza mazao yao popote penye bei nzuri hata nje ya nchi.

Hizo ni baadhi ya sababu za mabadiliko ya bei za vyakula.
 
Tatizo tumeshindwa kuimport baadhi ya mazao ya chakula toka huko mabara mengine halafu serikali yetu inachapisha pesa kimya kimya hasa baada ya uchaguzi wa 2020
 
Hali si nzuri,

Juzi kati hapa shirika la UN-WFP lilikuwa linateketeza moto shehena yake ya nafaka kwenye moja ya maghala yake huko Kanda ya ziwa.

Raia wakavamia kuzima moto ili wajichotee chakula ikawa tafrani.

Serikali iachie maghala yake ku-neutralize bei si walitamba kununua si mahindi tu bali nafaka karibu zote.
 
Baadhi ya wadau tumeanza kulalamikia jambo hili, lakini katika hali ya kushangaza! Serikali imeweka pamba masikioni. Sisi tulioko huku mtaani tunaona namna hali ilivyo mbaya kwa wananchi wa kawaida!

Serikali inatakiwa kuja na suluhu ya kupunguza huu mfumuko wa bei kwenye bidhaa za chakula! Yaani hii hali isipo dhibitiwa kwa wakati, basi kuna kila dalili ya kuja kutokea njaa kali ya funga funga miezi kadhaa ijayo.
 
Tatizo ni kwamba, serikali haisemi ukweli kuhusu kiwango halisi cha mfumuko wa bei.

Haiwezekani kabisa bidhaa zote ziwe zinapanda bei kwa kiwango kikubwa hivi halafu wanatudanganya kwamba mfumo ni asilimia sijui nne na pointi kadhaa au tano, huu ni uongo mtupu.

Kiwango halisi cha mfumuko wa bei katika nchi hii kwa sasa sio chini ya asilimia 30 lkn kwa kuwa kote ni siasa ndio inatawala basi ndio tunadanganywa hivyo.
 
Hivi ni wakati gani serikali hutakiwa kutoa chakula toka kwenye akiba yake ili kufidia upungufu uliopo unaosababisha bei ya vyakula kupanda?

Naona huu ndio wakati mzuri wa serikali kufanya hivyo, inaonekana kama vile bado wamezubaa hawaoni wala kusikia haya malalamiko ya wananchi toka kila upande wa nchi, au wana hofu wasije kutoa sasa halafu mbele ya safari hali ije kuwa mbaya zaidi...

Kwa upande wangu, huu upandaji holela wa bei za vyakula vyetu ukiondoa sababu ya upungufu wa mvua, naona Rais wetu alikosea pakubwa pale aliposema vita ya Urusi na Ukraine itasababisha bei ya bidhaa kupanda, ni kama aliwapa jamaa kisingizio cha kutuumiza, akajisahau kama yeye ni kama mlezi wa wananchi anaowaongoza.
 
Tatizo ni kwamba, serikali haisemi ukweli kuhusu kiwango halisi cha mfumuko wa bei.

Haiwezekani kabisa bidhaa zote ziwe zinapanda bei kwa kiwango kikubwa hivi halafu wanatudanganya kwamba mfumo ni asilimia sijui nne na pointi kadhaa au tano, huu ni uongo mtupu.

Kiwango halisi cha mfumuko wa bei katika nchi hii kwa sasa sio chini ya asilimia 30 lkn kwa kuwa kote ni siasa ndio inatawala basi ndio tunadanganywa hivyo.
Si mlidai serikali ya jpm ilikuwa inapika data kwa hiyo na hii ya mama hamyaamini tu
 
Tunaambiwa kuwa mfumuko wa bei (inflation rate) nchini kwetu bado ni mdogo sana, ni chini ya asilimia 5%! Wao wanauita single digit inflation.

Lakini kwa miezi ya hivi karibuni, bei za vyakula muhimu sokoni vimepanda kwa zaidi ya maradufu. Yaani mfumuko wa bei wa vyakula ni zaidi ya asilimia 50%, yaani ni double digit inflation! Vyakula hivi ni pamoja na vile wanavyotumia watu wa kawaida, walala hoi na waamka hoi. Kwa mfano Unga wa mahindi ni sasa hivi ni Sh 2,000 kwa kilo moja kutoka Sh 1,000 kwa kilo mwezi Julai 2022. Mchele (grade A) umepanda kutoka Sh 1,200 kwa kilo hadi Sh 3,500 - 4,000. Maharage kutoka Sh 1,800 hadi Sh 3,000. Karanga kutoka Sh 2,000 hadi Sh 5,000 na kadhalika.

Hili ni janga la kitaifa kwani hadi kufika msimu ujao wa mavuno, hatujui hali itakuwa vipi. Sasa hivi mwananchi wa uchumi wa kawaida, ni vigumu kula zaidi ya mlo mmoja kwa siku. Hizo kampeni za lishe bora ili kuepusha vijana wetu wa kiume kutegemea nguvu za supu ya pweza, hazitaweza kufanikiwa kwa mazingira kama haya.

Ili kupata ufumbuzi wake tunapaswa kujua chanzo chake hasa ni nini:

1. Je, ni vita ya Ukraine?

2. Je, ni ukame wa msimu uliopita ambao tulishuhudia mafuriko maeneo mbali mbali ya nchi na kusababisha uharibifu wa miundombinu hususani barabara zetu?

3. Je, ni akiba yetu ya taifa ya chakula (Strategic National Grain Reserves) imeshindwa kufidia upungufu uliopo wa chakula nchini kama ilivyo jukumu lake?

4. Je, ni hayo mamisafara ya malori ya urefu wa kilomita 7 kila siku yanayofanywa na wafanyabiashara (middle men, not our peasants) kupeleka chakula chetu kwa nchi jirani waliokuwa na uhaba wa chakula uliosababishwa na lockdowns walizojiwekea wakati wa mlipuko wa covid? Kwa nini sisi ambao hatukuji lockdown ndiyo tupate shida?

5. Je, ni kwa sababu ya kupanda kwa bei ya mafuta ya petroli na dizeli iliyosababishwa na sisi kususia kununua mafuta hayo toka Urusi, ili kuwaunga mkono West Europe ambao wao hata hivyo wanaendelea kununua gesi kutoka Urusi? West Europe wanalalama na kuishutumu sana Urusi kwa kuwabania gesi yao hasa kwenye kipindi hiki cha kuelekea winter. Kwa nini na sisi au kama East Africa Union tusiwe na msimamo kama wa Uchina na India wa kununua mafuta haya kutoka Urusi ili kuepukana na balaa hili la kupanda kwa bei ya vyakula. Mseveni na Ruto wameonesha dhamira hii.

6. Je, mfumuko huu wa bei unauhusiano na upandishaji wa mishahara ya watumishi wa umma? Jee itakuwaje pale serikali itakapopandisha mishahara ya taasisi binafsi hivi punde? Awamu iliyopita iliogopa sana kupandisha mishahara hii kwa kuogopa kuleta mfumuko wa bei kama zilivyo kanuni za kiuchumi.

Nini kifanyike kinategemea na majibu ya maswali hayo na mengine mtakayopendekeza.
Sasa wewe ulitaka bei ya mkulima iwe chini?
 
Mtoa mada mbona huongelei ishu ya mbolea kupanda kutoka elfu hamsini kwa mfuko wa kg 50 kabla ya corona mpaka mara tatu ya bei ambayo ni laki na nusu kwa mfuko wa kg 50 hivi sasa ?
 
Kwahiyo hiyo Inflation rate ni asilimia ngapi?

Mara ya mwisho naona, BOT waliweka 3.5% ingawa bei za kitaa zilishapaa kwa zaidi ya 30%

Kwani wese limetoka bei gani mpaka tulipo sasa? Vyakula vya ndani ya nchi navyo vinaathiriwa na vita ya huko? Maana kama mvua imenyesha, jua halikuwaaaaaaka.

NINI CHANZO CHA INFLATION HALISI?
NA AWAMU HII PIA WANAPIKA DATA?
 
Hivi ni wakati gani serikali hutakiwa kutoa chakula toka kwenye akiba yake ili kufidia upungufu uliopo unaosababisha bei ya vyakula kupanda?

Naona huu ndio wakati mzuri wa serikali kufanya hivyo, inaonekana kama vile bado wamezubaa hawaoni wala kusikia haya malalamiko ya wananchi toka kila upande wa nchi, au wana hofu wasije kutoa sasa halafu mbele ya safari hali ije kuwa mbaya zaidi...

Kwa upande wangu, huu upandaji holela wa bei za vyakula vyetu ukiondoa sababu ya upungufu wa mvua, naona Rais wetu alikosea pakubwa pale aliposema vita ya Urusi na Ukraine itasababisha bei ya bidhaa kupanda, ni kama aliwapa jamaa kisingizio cha kutuumiza, akajisahau kama yeye ni kama mlezi wa wananchi anaowaongoza.
Hamna Rais mule mkuu nawashangaa Sana mnaodhan mama n competent she is incompetent

Hajui kuchagua maneno wapi ya kuongea nayap ya kuacha



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom