Nini faida ya mirungi na hasara zake?

dibbo

Member
Feb 18, 2011
30
1
Wana jf naomba mnipe faida na hasara za mirungi aka gomba

MADHARA YA KIAFYA;

1. Mtumiaji wa mirungi yupo
katika hatari ya kupata
vidonda vya tumbo.
- Kupungukiwa msukumo wa
kufanya tendo la ndoa (low sex drive) na pia kuwahi kumaliza haraka na kutoweza kudumu kwenye tendo la ndoa kwa muda mrefu.

2. Ukosefu wa haja kubwa (constipation)

3. Utumiaji wa muda mrefu
husababisha ini kushindwa
kufanya kazi, pia meno kubadilika rangi, kudhoofika, fizi kuuma na harufu mbaya
mdomoni.

4. Upungufu wa usingizi.

5. Humpelekea mlaji
kutawaliwa nayo. (addiction)

6. Madhara ambayo bado
kinamama walaji Mirungi
hawajagundua ni kwamba
mtoto anayezaliwa na mama
mlaji Mirungi mara nyingi
hukataa kunyonya titi la mama
yake kwa sababu ladha ya
maziwa inabadilika kwa ajili ya
utumiaji wa madawa (pesticides) unaotumiwa na
wakulima wa Mirungi kama
inavyoeleza utafiti uliofanyika
na Chuo Kikuu Cha Aden
(Aden University).

7. Utafiti mwengine kule
Ethiopia unatueleza ya kuwa
mtoto wa mama mwenye kula
Mirungi kwa wingi huwa hana
uzito wa kawaida wakati wa
kuzaliwa.

8. Ukosefu wa hamu ya kula
chakula.

9. Magonjwa ya vidonda vya tumbo (ulcers).

10. Kupatwa na ugonjwa wa futuru/futuri/bawasiri/baasili - nyama inayoota kwenye utupu wa nyuma.

11. Walaji wengi huvuta na sigara, hata yule aliyekuwa havuti kabla ya kuanza kula Mirungi, hujikuta akizama kwenye uvutaji, na madhara huwa maradufu.

source;

polisijamiimafia: MIRUNGI NA MADHARA YAKE
 
Hasara zake nikua ukishakula ulevi wake unakupa hisia kua wewe unamiliki magorofa yote pale Dar es Salaam! Hyo ni noooma mazee!
 
Ina stem (ulevi fulani hivi) ambao unaupata kwa muda ila hasara ni nyingi zaidi...

1. ule utomvu unaomeza unaenda kuganda kwenye utumbo (ndio maana huwa inatakiwa ukimaliza kula unywe maziwa fresh
2.Ukienda haja kubwa inatanguliwa na ute unaoteleza kama kamasi......
3.Inakufanya uridhike na maisha hata kama wewe ni masikini....
 
Hupoteza hamu ya tendo la ndoa,hapo sijui kama ni faida ama hasara
 
Hasara mojawapo ni kupigwa mashine hadi unasahau kufuli gesti, nakumbuka kuna jamaa mmoja ni rafiki yangu alikula mirungi kwa bahati mbaya, yaani sian hamu.
 
Kama haina madhara mbona inapigwa marufuku sehemu nyingi?
 
Hasara!~ Ufujaji wa pesa
Madhara~ Kukosa hamu ya kula na tendo la ndoa, wendawazimu.
Izara~ Kuota ndoto za alinacha.
Ufukara~ Kufilisika.
Himar~ Kuwa na akili mfano wa punda.
Ufala~ Kuhangaika unapo pata arosto.
Kali ni pale aakhir gaat unapohisi kuwashwa sehmu za haja kubwa, na hii hakuna mlaji atakae kiri.
 
mfano mzuri nchi ya yemen.yemen ilikuwa nchi yenye wasomi hodari wa safari za meli wafanya biashara wazuri lkn tangu waanze kutumia mirungi miaka 300 iliyopita imeifanya nchi iwe katika hali ya sasa.
 
Mmm! Mmenikumbusha huku Kondoa, warangi wanakula km mbuzi akulavyo majani. @ siku kesi polisi haziishi na ni kesi zinazoongoza
 
Kama kweli unataka kujua madhara ya mirungi chukua kidogo niletee hapa Kituo cha Kilwa polisi maana ndo kuna mtambo ambao utatupa jibu la uhakika mi na weye au!?
 
Hapa nilipo nagonga shamba rungu yani nifull handas, tatizo walio wengi wanasaga gomba bila ya kula,ukitaka usigonge mzigo kunywa chai navihandazi vyako alafu mchana usile alafu ugonge gomba, kuhusu tatizo kweny haja kubwa sina hakika ila nadhani litakua nikwawale wanao geuza gomba ndo msosi,kula chakula kwanza ushibe alafu saga gomba ila iwe shamba rungu,au ngarito utagonga mzigo upendavyo,
 
Kuna mirungi aina nyingi kuna rungu korombo chakasi miruingi yenyemadhala ni chakasi na mirungi inayo pandiwa mbolea. Madhara mengne sijaona zaidi yaufujaji wapesa na yenyewe ya tegemeana uliyo jcondition. Wewe mimi ni mwaka wa kumi nasaga gomba nanina to......mb demuwangu mpaka anajuta kuzaliwa
 
MADHARA YA KIAFYA;

1. Mtumiaji wa mirungi yupo
katika hatari ya kupata
vidonda vya tumbo.
- Kupungukiwa msukumo wa
kufanya tendo la ndoa (low sex drive) na pia kuwahi kumaliza haraka na kutoweza kudumu kwenye tendo la ndoa kwa muda mrefu.

2. Ukosefu wa haja kubwa (constipation)

3. Utumiaji wa muda mrefu
husababisha ini kushindwa
kufanya kazi, pia meno kubadilika rangi, kudhoofika, fizi kuuma na harufu mbaya
mdomoni.

4. Upungufu wa usingizi.

5. Humpelekea mlaji
kutawaliwa nayo. (addiction)

6. Madhara ambayo bado
kinamama walaji Mirungi
hawajagundua ni kwamba
mtoto anayezaliwa na mama
mlaji Mirungi mara nyingi
hukataa kunyonya titi la mama
yake kwa sababu ladha ya
maziwa inabadilika kwa ajili ya
utumiaji wa madawa (pesticides) unaotumiwa na
wakulima wa Mirungi kama
inavyoeleza utafiti uliofanyika
na Chuo Kikuu Cha Aden
(Aden University).

7. Utafiti mwengine kule
Ethiopia unatueleza ya kuwa
mtoto wa mama mwenye kula
Mirungi kwa wingi huwa hana
uzito wa kawaida wakati wa
kuzaliwa.

8. Ukosefu wa hamu ya kula
chakula.

9. Magonjwa ya vidonda vya tumbo (ulcers).

10. Kupatwa na ugonjwa wa futuru/futuri/bawasiri/baasili - nyama inayoota kwenye utupu wa nyuma.

11. Walaji wengi huvuta na sigara, hata yule aliyekuwa havuti kabla ya kuanza kula Mirungi, hujikuta akizama kwenye uvutaji, na madhara huwa maradufu.

source;

polisijamiimafia: MIRUNGI NA MADHARA YAKE
 
hawa wote kwa kudurusu walioandika ni vitu walivyosoma. mimi hutumia tena sana na nimewahi kua inapokuzwa huku kenya Meru.
mirungi huongeza concentration ndio maana hutumiwa sana na madereva wa masafa marefu kutokana na uwezo wake wa kupunguza usingizi na uchovu
mirungi hufanya mtu kuwa na mipango makini haswa wakati handas imepanda ila pia katika hali hii pia unaeza kua na mipango isio wezekana kwa kawaida lakini hii ndio raha yake.
hupunguza stress si kama pombe au bangi hii mawzo huwa timamu na mtu mtulivu ila pia unaeza kupiga stori sana.
ukila unahitaji maji kwa wingi unapomaliza maana usipofanya hivyo utatizika ukienda haja kubwa kwa sababu kinyesi hua kigumu sio kama ulivyo elezwa hapo awali.
haipunguzi tija ya kufanya mapenzi ila uume huchelewa kupata damu na kusimama wima na ikisimama anayeshughulikiwa atapenda maana hakuna kuanguka ni mshike mshike.ndio sababu eneo la tharaka nithi kenya inapokuzwa kuna idadi kubwa ya watu.kwa maelezo zaidi nitafute pm
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom