Nini faida ya Marais wastaafu wa Tanzania kwa nchi yetu?

Chief Kabikula

JF-Expert Member
Jan 1, 2019
7,567
9,026
Tanzania mpaka sasa tuna marais wastaafu watatu ukiacha Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyetangulia mbele za haki.

Hawa marais wastaafu ni wazoefu na wajuzi sana wa mambo kupitia uzoefu wa kuongoza nchi kwa miaka kumi kila mmoja.

Swali huo uzoefu, maarifa na ujuzi wao umesaidia vipi nchi hii. Baba wa taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Alipokabidhi kijiti kwa rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi hakusita kumkosoa waziwazi pale alipoona mzee Mwinyi anaenda ndivyo sivyo, aliwahi kutamka huwezi kuongoza nchi kwa kushauriwa na mke wako maana hatujui kesho atakushauri nini.

Hilo lilikuwa ni dongo kwa rais Ali Hassan Mwinyi wakati, mpaka Mwalimu Nyerere akaandika kitabu cha uongozi wetu na Hatima ya Tanzania, yote hiyo ilikuwa na lengo moja tu kukosoa utawala kwa manufaa ya nchi.

Wakati wa utawala wa awamu ya tatu ya mzee Benjamin William Mkapa Mwalimu Nyerere hakukaa kimya, alipoona mambo yanaenda ndivyo sivyo alikemea, wakati wa sera za ubinafsishaji, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alimkosoa vikali mzee Mkapa kwa kubinafsisha mali za umma hasa NBC BANK pamoja na uwekezaji wa wageni katika madini wakati huo.

Hiyo yote aliifanya baba wa taifa katika lengo la kuisaidia nchi alitimiza wajibu wake kwa nchi yake.

Leo tuna marais wastaafu watatu ujuzi, maarifa na uzoefu wa kukaa ikulu miaka kumi wapo kimya licha ya kila dalili kuonyesha kuwa uongozi wa sasa umekengeuka na utaleta sintofahamu kama tahadhari hazitochukuliwa.Faida ya hawa viongozi wastaafu nini kwa nchi hii?
 
No alama ya amani aka kuonesha dunia utofauti uliopo kati ya maeneo mengi ya Africa (upinduaji was katiba) na hapa kwetu kwamba watu wanaachiana madaraka bila kinyongo bila hiyana kama katiba inavyoelekeza!
 
No alama ya amani aka kuonesha dunia utofauti uliopo kati ya maeneo mengi ya Africa (upinduaji was katiba) na hapa kwetu kwamba watu wanaachiana madaraka bila kinyongo bila hiyana kama katiba inavyoelekeza!
Marais Wastaafu wana majukumu makubwa sana sio hilo tu wanapaswa kwenda mbali zaidi ya hapo.
 
Tuwaache wastafu wapumzike

Tuendelee kumuunga mkono mh Rais katika juhudi zake za kuipeleka Tanzania Katika uchumi wa kati
 
NYERERE alikuwa "msafi", ndo maana aliweza kukosoa Bila hofu. Hawa wa Sasa baadhi yao hawajiamini maana wanategemea fadhila za mkulu kuzuia madudu yao kufukuliwa, na alishaonya mapema kuwa yeyote asiwashwe washwe. Kwa mazingira hayo kila mmoja anaangalia maslahi yake.. wananchi watajijua
 
IMG_20191112_194800.jpg

Hali kama hii wastaafu wanakaaje kimya?
 
IMG_20190823_193421.jpg

Marais wastaafu hawajaona tu dereva wa basi Jiwe anaelekea kupindua abiria, basi linaelekea shimoni.
 
NYERERE alikuwa "msafi", ndo maana aliweza kukosoa Bila hofu. Hawa wa Sasa baadhi yao hawajiamini maana wanategemea fadhila za mkulu kuzuia madudu yao kufukuliwa, na alishaonya mapema kuwa yeyote asiwashwe washwe. Kwa mazingira hayo kila mmoja anaangalia maslahi yake.. wananchi watajijua
Si wanakinga hawa hawashtakiwi kwa makosa waliyofanya wakiwa madarakani?
 
Faida ya hawa viongozi wastaafu nini kwa nchi hii?

Kula pensheni, kulindwa na kuhudumiwa na serikali iliyopo madarakani.

Unataka waanze kumkosoa raisi aliyekuwepo madarakani ili wakose hizo "privileges" zilizohalalishwa??!.

Kila mmoja na zama zake, unapomaliza zama zako acha mwingine naye awe huru kufanya yake kupitia vyombo vyake vya ushauri na utendaji. Kama atahitaji ushauri hilo ni suala jingine na hapo ndipo hao wastaafu wanapotakiwa kushauri.
 
Kula pensheni, kulindwa na kuhudumiwa na serikali iliyopo madarakani.

Unataka waanze kumkosoa raisi aliyekuwepo madarakani ili wakose hizo "privileges" zilizohalalishwa??!.

Kila mmoja na zama zake, unapomaliza zama zako acha mwingine naye awe huru kufanya yake kupitia vyombo vyake vya ushauri na utendaji. Kama atahitaji ushauri hilo ni suala jingine na hapo ndipo hao wastaafu wanapotakiwa kushauri.
Hakuna mtu anateyekataa awe huru kufanya yake, lakini sio mpaka ya kijinga, ya kipuuzi, yasiyo na maslahi kwa nchi na Watanzania.
 
Chief Kabikula,

Nyerere pamoja na madhaifu ya utawala wake hakujimbikizia mali kwa njia za ufisadi. ndio maana hakuogopa kukemea viogozi. hawa maraisi baada yake wote wanaogopa kukemea kwasababu wanagopa madhambi ya ufisadi waliyo yafanya ambayo jiwe anayatumia ku blackmail. yaani wanajuwa wakimkosawa jiwe ataanika ufisadi wao.
 
Hakuna mtu anateyekataa awe huru kufanya yake, lakini sio mpaka ya kijinga, ya kipuuzi, yasiyo na maslahi kwa nchi na Watanzania.
hayo masilahi ya nchi ni yapi kama wanachi wanalala njaa na kufa kwa kukosa elimu na huduma za afya? au masilahi ya taifa ni raisi kutembelea private jet ?
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom