Nini faida na hasara za nyumba za mawe? Bongo kuna wataalamu wa kujenga kwa mawe namna hii?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,160
12,634
Eti wakuu, bongo kuna wataalamu wa kujenga na mawe namna hii, wakatoa nyumba imara? Pia naomba kujua faida na hasara za nyumba ya mawe. Gharama zake zikoje?

3d2369fb54fd7a3893176f407b320271(1).jpg
0ce8c7e18267c05eb80605159a887645(1).jpg
49e2208d003e9c98f8da10a60c095ccc.jpg
1826-round-stone-barn--1826roundstonenewengbarn184697-frank-j-benz.jpg
97714639-old-small-stone-house-on-the-island-martinique-in-the-caribbean.jpg
f3eca7d5df2785c644d8783faa9badd0.jpg
the-stone-house-by-the-river-hotel-25274968.jpg
brandywine-farmhouses-john-chad-house.jpg
 
Nyumba za mawe ziko imara zaidi kuliko za tufali (ni nadra sana kuwa na ufa kwenye ukuta). Lakini gharama zake ni kubwa kidogo kwenye kunyoosha kuta ili upate usawa kwani simenti inakwenda nyingi.

Zanzibar ziko nyingi tu hasa katika maeneo ya karibu na pwani.

Kabla ya ujenzi wa tofali kushika kasi ujenzi mkuu ulikuwa kwa kutumia mawe. Lakini fundi lazima awe mweledi wa kunyoosha kuta za nyumba bila ya hivyo inakaa upande.
 
Nyumba za mawe ziko imara zaidi kuliko za tufali (ni nadra sana kuwa na ufa kwenye ukuta). Lakini gharama zake ni kubwa kidogo kwenye kunyoosha kuta ili upate usawa kwani simenti inakwenda nyingi.

Zanzibar ziko nyingi tu hasa katika maeneo ya karibu na pwani.

Kabla ya ujenzi wa tofali kushika kasi ujenzi mkuu ulikuwa kwa kutumia mawe. Lakini fundi lazima awe mweledi wa kunyoosha kuta za nyumba bila ya hivyo inakaa upande.
Uhimara wake unapatika kwa ubora wa mjengaji. Hizi zikikosewa katika kuyaunganisha mawe zinaweka ufa mwingi tu na ubaya wa mawe ikitokea ufa mkubwa ni rahisi sana yakalazimisha kuporomoka kutokana ya kuwa jiwe haliwi na kitako nyoofu.
 
Uhimara wake unapatika kwa ubora wa mjengaji. Hizi zikikosewa katika kuyaunganisha mawe zinaweka ufa mwingi tu na ubaya wa mawe ikitokea ufa mkubwa ni rahisi sana yakalazimisha kuporomoka kutokana ya kuwa jiwe haliwi na kitako nyoofu.
Ujenzi wowote unahitaji utaalamu hilo halina shaka. Aidha aina ya mawe yanayotumika kujengea pia kuna utaalamu wake.

Angalia yale majumba ya stone town Unguja mjini, yale ya asili yote yamejengwa kwa mawe na chokaa na yamekaa kwa miaka mingi sana. Sasa hivi baadhi yameanza kuanguka kwa vile hakuna uhudumiaji.
 
Ujenzi wowote unahitaji utaalamu hilo halina shaka. Aidha aina ya mawe yanayotumika kujengea pia kuna utaalamu wake.

Angalia yale majumba ya stone town Unguja mjini, yale ya asili yote yamejengwa kwa mawe na chokaa na yamekaa kwa miaka mingi sana. Sasa hivi baadhi yameanza kuanguka kwa vile hakuna uhudumiaji.
Kuna kitu kama chainsaw kinachonga mawe ukubwa unaotaka na linachongwa jiwe linakuwa kama tofali lakini yote haya kufanyika kuna bei yake.
 
Nyumba za mawe ni nzuri ila ni gharama sana yaan unahitaji expert wa kufanya hiyo kazi (Fundi), pia huhitaji plaster wala rangi ukijenga umemaliza,

Maeneo ambayo mawe yanapatikana kwa urahisi kama Dodoma, Mwanza au Iringa kutakua na uafadhali katika ujenzi, ukijenga Dar jiwe unalitoa Lugoba utajua hujui
 
Nyumba za mawe ni nzuri ila ni gharama sana yaan unahitaji expert wa kufanya hiyo kazi (Fundi), pia huhitaji plaster wala rangi ukijenga umemaliza,

Maeneo ambayo mawe yanapatikana kwa urahisi kama Dodoma, Mwanza au Iringa kutakua na uafadhali katika ujenzi, ukijenga Dar jiwe unalitoa Lugoba utajua hujui
Ukifanya finishing madirisha ya vioo inapendeza sana
 
Uhimara wake unapatika kwa ubora wa mjengaji. Hizi zikikosewa katika kuyaunganisha mawe zinaweka ufa mwingi tu na ubaya wa mawe ikitokea ufa mkubwa ni rahisi sana yakalazimisha kuporomoka kutokana ya kuwa jiwe haliwi na kitako nyoofu.
Hapo kwenye wataalamu naona ndiyo changamoto. Nimefanya utafiti inaonekana kuna mambo mengi sana ya kuzingatia, hasa unapojenga kwenye kona.
 
Kuna kitu kama chainsaw kinachonga mawe ukubwa unaotaka na linachongwa jiwe linakuwa kama tofali lakini yote haya kufanyika kuna bei yake.
Yale wanachonga na kama chainsaw yanakuwa sandstones. Siyo magumu sana. Yanatoa tofali nzuri sana. Bila shaka hata yale ya baharini unaweza kuchonga. Kuna haya ya volcano, granite. Magumu balaa, yapo kama chuma.
 
Eti wakuu, bongo kuna wataalamu wa kujenga na mawe namna hii, wakatoa nyumba imara? Pia naomba kujua faida na hasara za nyumba ya mawe. Gharama zake zikoje?

View attachment 2097396View attachment 2097398View attachment 2097399View attachment 2097400View attachment 2097401View attachment 2097403View attachment 2097404View attachment 2097405
Hapa Rorya kuna secondary imejengwa Kwa mawe tuu inaitwa Waningo sec school. Nasikia na fundi aliyenga bado yupo hai mpaka Leo hii yupo Musoma na bado anajenga nyumba za dizaini hii
 
Back
Top Bottom