Nini cha kufanya mara tu baada ya kuingiliana kimwili na muathirika wa UKIMWI?

Alexander The Great

JF-Expert Member
Aug 28, 2018
4,502
23,582
Habari Wana Kijiji,

Kwa muda tunapost thread nyingi ni za kuomba msaada/umbea/habari na kupeana ushauri. Leo nimeamua kuja na thread hii ya kufundisha/kukumbusha/kuelimisha na kutahadharisha.

Ukimwi (H.I.V) kwa maisha ya sasa si HUKUMU YA KIFO TENA kama ilivyokua hapo awali. Gonjwa hili limeshaua mamilioni ya watu hapo mwanzoni, tofauti na sasa unaweza kuishi miaka mingi sana hata kama ni muathirika, japo bado linaendelea kupoteza maisha ya watu wengi sana duniani.

NOTE THAT: Nikumbushe tu, chukua tahadhari kwani gonjwa hili bado lipo na linaangamiza watoto/vijana na wazee wa kila jinsia kila siku ipitayo.

Nirudi kwenye mada husika.

"POST EXPOSURE PROPHYLAXIS au kwa kifupi PEP" ni njia ya dharura sawa na njia ya kutumia ARV au ART.

Hii PEP ni dose ya dawa kama ilivyo ARV au ART ambayo mtu hutumia mara tu baada ya kukutana kimwili na muathirika wa ukimwi au kujichoma na kitu chenye ncha kali ambacho kimetumiwa na muathirika huyo.

Lengo la dawa za PEP ni kuzuia mtu asiathirike na gonjwa hili la ukimwi mara tu baada ya kugundua au kuhisi anaweza kuwa amepokea vinasaba vya damu iliokwisha athirika na ukimwi kutoka kwa muahirika. Dose hii ya dawa inapaswa mtu kuanza kutumia mara tu baada ya kuhisi anaweza akawa amepokea vinasaba hivyo vya damu iliokwisha athirika kwa muda usiozidi masaa 72 (Yani mtu aanze kutumia dose kabla ya masaa 72 hayajapita), au lasivyo dawa hazitofanya kazi.

PEP ni dose ya dawa ya kuzuia maambukizi ya ukwimi kwa dharura mara tu mtu anapokua amefanya mapenzi au kupokea vinasaba vya damu na mtu alie athirika (Yasizidi masaa 72). Sio kwaajili ya mtu aliekwisha athirika tayari.

Wana kijiji, tujilinde, ukimwi upo na unauwa kama hatutoji kinga.
 
Nimesikia mitaani kuwa kuna kifaa ambacho linaweza kutumika kujipima mwenyewe ukiwa nyumbani.
Naomba kufahamishwa:
i) Ni kweli kipo?
ii) Ubora na uthabiti wake.
iii)Kinapatikana/kinauzwa wapi?
 
Nimesikia mitaani kuwa kuna kifaa ambacho linaweza kutumika kujipima mwenyewe ukiwa nyumbani.
Naomba kufahamishwa:
i) Ni kweli kipo?
ii) Ubora na uthabiti wake.
iii)Kinapatikana/kinauzwa wapi?
Vipo vifaa vya kujipimia ukimwi (na vya malaria) nyumbani, ila hawaruhusu kujipimia nyumbani. Na kuvipata ni tabu labda uwe na rafiki mwenye pharmacy au daktari.

Wanataka mtu apimwe hospital ili kama akikutwa positive apewe ushauri nasaha hapo hapo na wataalamu.
 
Vipo vifaa vya kujipimia ukimwi (na vya malaria) nyumbani, ila hawaruhusu kujipimia nyumbani. Na kuvipata ni tabu labda uwe na rafiki mwenye pharmacy au daktari.

Wanataka mtu apimwe hospital ili kama akikutwa positive apewe ushauri nasaha hapo hapo na wataalamu.
Nashukuru sana.

Naomba kufahamu uthabiti/ubora wake.

Vinatoa matokeo yanayoaminika?
 
Nashukuru sana.

Naomba kufahamu uthabiti/ubora wake.

Vinatoa matokeo yanayoaminika?
Vinatoa majibu ya kuaminika, na wanashauri upime mara mbili, ya kwanza ya kujua hali na ya pili kuthibitisha majibu ya mwanzo. Vipimo kinakua cha plastic kidogo kama cha kupimia malaria, kina sinado yake ndogo ya kujitoboa kidole kama unapima malaria.
 
Vipi izo dawa zinapatikana wapi?
Sio dawa za kwenda na kupata kirahisi mkuu,nadhani sera ya afya haijaruhusu watu kupewa Kama sio kesi maalum kama vile kubakwa,wahudumu wa afya wanapojikuta wamejitoboa kwa vifaa hatarishi kazini nk.
Lakini Ukienda tu umueleze Umefanya ngono na mtu unayedhani ana maambukizi lazima uzinguliwe japo unaweza kusaidika
 
Vipo vifaa vya kujipimia ukimwi (na vya malaria) nyumbani, ila hawaruhusu kujipimia nyumbani. Na kuvipata ni tabu labda uwe na rafiki mwenye pharmacy au daktari.

Wanataka mtu apimwe hospital ili kama akikutwa positive apewe ushauri nasaha hapo hapo na wataalamu.

Kwa sasa tuna sheria inayoruhusu watu kujipima VVU nyumbani na vitenganishi kuuzwa madukani.
 
Back
Top Bottom