Nini asili ya jina Tanganyika na Nani alilitunga jina hili?

Silipendi kabisa hili jina. Hili jina limekaa kikoloni koloni. Lililetwa na Wakoloni. Je kuna umuhimu gani kuturudisha kwenye Jina la ukoloni? Kwa nini tusibuni jina lingine tu?
 
Hili Tanganyika lililetwa na wajerumani kwa hiyo lazima kutakua na maelezo chanzo cha jina hili. Nilivyosikia kabla ni kuwa jina ni mjumuisho wa mji wa Tanga na Nyika iliozunguka kuliko upeo wa macho - sijui kama ni kweli.
 
Neno Tanganyika nalipenda sana..in fact liko so attached na sisi watu wa bara kuliko hata neno Tanzania..niko proud kuitwa Mtanganyika kuliko mtanzania..na sikubaliani kuwa asili ya hili neno ni wazungu...wazungu watatamukaje neno Tanganyika...Lake victoria from its name ni kweli limetokana ma wazungu lakini sio Tanganyika.
 
Kuna mijadala mingi imepita humu JF juu ya ujio wa Tanganyika kufuatia Rasmi ya pili ya katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 2013,lakini katika mijadala yote sijaona ikitoa tafsiri na asili ya hili neno Tanganyika zaidi ya baadhi ya members kusema kuwa asili ya neno Tanganyika ni Tanga bila ya kusema maana ya neno lenyewe.Hata hivyo nimeshawahi kusoma mahali kuwa asili ya neno Tanganyika ni Kigoma, (Lake Tanganyika),na neno hili limetokana na aina flani ya samaki (electric eels) anayeitwa NTANGA na samaki huyu huwa anatoa umeme na anapatikana ziwa Tanganyika hence neno Tanganyika.Kuna wengine wakisema kuwa neno hili asili yake ni Kigoma hukohuko likiwa na maana ya makutano ya watu yaliyokuwa yakifanyika ziwani hence Tanganyika yaani kuchanganyika.
Sisi wengine watu wa bara na kwa lugha ya kwetu neno NYIKA hata hivyo lina maana pori ,sasa lilivyokuja kuunganishwa na Tanga hapa ndo kitendawili kingine. Naomba wadau wenye kujua maana na asili ya hili neno watuelimishe tafadhali.


Tanga means first
Nyika means counrty

TangaNyika means First country
 
[QUOTEmkada8254809]Kabla ya kuja waingereza hakuna nchi iliyoitwa Tanganyika pamoja na Rwanda/urundi ilikua 'D Ost Afric
 
Kwa kisambaa na kibondei (makabila ya Tanga) mnyika ni mtu wakuja(asie mwenyeji). Na hili neno lilitumika zaidi kwa waliotoka bara kuja kulima mkonge. Tanga ni lile kama shuka hivi linalotumika kwenye madau(mitumbwi) kusafirisha chombo kwa msaada wa upepo. Pia tanga ina maana ya shughuli za msiba. Mfano, kuinua Tanga ni kumaliza msiba... Ni mtazamo wangu, malizieni.
 
Hili Tanganyika lililetwa na wajerumani kwa hiyo lazima kutakua na maelezo chanzo cha jina hili. Nilivyosikia kabla ni kuwa jina ni mjumuisho wa mji wa Tanga na Nyika iliozunguka kuliko upeo wa macho - sijui kama ni kweli.
TANGA .......ILIKUWA NDIO NJIA YAO YA KUINGILIA KATIKA ENEO HILI LA ARDHI, AMBALO LIMETAWANYIKA MPAKA KIGOMA, SASA BAADA YA MAENEO MENGINE YOTE KUPEWA MAJINA LIKAWA LINATAMBULISHWA KWA KI SIRI (PENGINE KWA SASABU WANAZOZIJUA WAO......(LABDA MALI ZILIZOMO N.K.)........1.UTAMBULISHO WA KWANZA ULIKUWA NI KWAMBA KIPANDE HICHO CHA ARDHI KIMEZUNGUKWA NA MAZIWA (LAKES).....2.LAND MARK ZAO ZILIKUWA BAADA YA KUINGIA TANGA......KWA UPANDE WA KASKAZINI WALIKUBALI MWISHO WAKE UWE NI MLIMA KILIMANARO NA KUANZIA HAPO UNAENDELEA MBELE MPAKA UKUTE ZIWA LINGINE KUBWA(VICTORIA).3.PIA WALIKUBALIANA BAADA YA KUINGIA TANGA KWA UPANDE WA KUSINI UKIAMBA AMBAA NA BAHARI MWISHO WAKE UWE NI MTO MKUBWA (RUVUMA),TENA UKIUFUATA MWISHO WAKE UTAKUTA ZIWA (NYASA/MALAWI).....HIVYO BASI UPANDE WA KASKAZINI WALIPATA LAND MARK MBILI KWANZA MLIMA PILI ZIWA...NA UPANDE WA KUSINI WALIPATA LAND MARK MBILI KWANZA MTO THEN ZIWA....SASA KIPANDE CHA KATI CHOOTE KIKAITWA NYIKA...NYIKA .....NA MWISHO WA NYIKA HIYO...PIA KUNA ZIWA..NDIO KISA NA MAANA YA ZIWA HILO KUITWA TANGANYIKA......NASIKITIKA DOCUMENT HIZI HAZIKUMFIKIA MWL.JK.NYERERE MANAKE HATA YEYE ALIKUWA ANATAFUTA ASILI YA NENO TANGANYIKA...........to be continued......
 
Kuna mijadala mingi imepita humu JF juu ya ujio wa Tanganyika kufuatia Rasmi ya pili ya katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 2013,lakini katika mijadala yote sijaona ikitoa tafsiri na asili ya hili neno Tanganyika zaidi ya baadhi ya members kusema kuwa asili ya neno Tanganyika ni Tanga bila ya kusema maana ya neno lenyewe.Hata hivyo nimeshawahi kusoma mahali kuwa asili ya neno Tanganyika ni Kigoma, (Lake Tanganyika),na neno hili limetokana na aina flani ya samaki (electric eels) anayeitwa NTANGA na samaki huyu huwa anatoa umeme na anapatikana ziwa Tanganyika hence neno Tanganyika.Kuna wengine wakisema kuwa neno hili asili yake ni Kigoma hukohuko likiwa na maana ya makutano ya watu yaliyokuwa yakifanyika ziwani hence Tanganyika yaani kuchanganyika.
Sisi wengine watu wa bara na kwa lugha ya kwetu neno NYIKA hata hivyo lina maana pori ,sasa lilivyokuja kuunganishwa na Tanga hapa ndo kitendawili kingine. Naomba wadau wenye kujua maana na asili ya hili neno watuelimishe tafadhali.

Pitia hapa JAIZMELALEO: WASIFU 360: MOHAMMED IQBAL DAR MBUNIFU WA JINA TANZANIA panaweza pakawa na jibu
 
Tanganyika asili yake ni Kigoma, ilikuwa hivi,
Wazungu wavumbuzi kina Livingstone walipifika ujiji walilakiwa na wenyeji, katika mapokezi yale walikuwa wakisema TSANGANIGWA (SANGANIGWA) =>Means KARIBU, kwa kiha,. Basi wajerumani wale katika matamshi walishindwa kutamka Tsanganigwa, wakawa wanatamka Tanganyika....!
 
Kwa kisambaa na kibondei (makabila ya Tanga) mnyika ni mtu wakuja(asie mwenyeji). Na hili neno lilitumika zaidi kwa waliotoka bara kuja kulima mkonge. Tanga ni lile kama shuka hivi linalotumika kwenye madau(mitumbwi) kusafirisha chombo kwa msaada wa upepo. Pia tanga ina maana ya shughuli za msiba. Mfano, kuinua Tanga ni kumaliza msiba... Ni mtazamo wangu, malizieni.

Unaweza ukawa uko sahihi basi kwa logic kuwa waliokuwa wanakwenda Tanga (wanyika, wakuja Tanga) kwa shughuli za mkonge ndiyo walikuwa wanaitwa Watanganyika!
 
Mm nahc maana yake kua ni "Tambara pori" hahahaaaa.. Watanganyika mjue hivyo nyinyi ni watu wa tambara pori.. njoni ZANZIBAR tuwatafutie jina jamanii.. tumekupeni Dar-es-salam zuri tu lkn ni la mji.. njoni tukupeni la nchi sasa msione tabu..!
 
Katika muendelezo wangu wa kutafuta kiini cha la Matatizo yetu, leo hii najikita ktk kuelezea kuhusu Jina la Tanganyika yaani asili yake na ni nini mana yake, kwa wale ambao bado hawafahamu...

Tanganyika ni Muunganiko wa maneno mawili yaani Tanga na Nyika. Maneno haya yaliunganishwa pamoja na kuunda neno Moja Tanganyika, na hili lilifanywa na Wajerumani waliokuwa wakitawala Nchi yetu kipindi hicho!

Wajerumani walikuja na jina hilo baada ya kuanza kutawala Nchi yetu ambayo Mpaka wake kwa Upande wa Kusini ni Mto Ruvuma na Magharibi ni Ziwa kubwa lilokuja kupewa Jina la Tanganyika (na Wajerumani).

Kumbuka Wajerumani walivyofika walikaa kwanza Pwani ambapo walijenga Bandari ya Dar na pamoja na Tanga, sasa Eneo la nchi yao au yetu lilikuwa linatoka Tanga mpaka kwenye Ziwa (baadae Tangayika), na mji wa Tanga peke yake ndio uliokuwa umepimwa yaani Mipango Miji lkn kutoka Tanga mpaka kwenye Ziwa kulikuwa na Misitu mizito yaani Nyika au kwa kifupi kulikuwa hakujapimwa hivyo wakaamua kuliita lile Ziwa Tanga-nyika yaani kati ya Tanga na Nyika au misitu minene.

Baada ya Waingereza kuja walitaka kubadilisha jina la Nchi iliyokuwa inaitwa Ujerumani ya Afrika Mashariki, kulikuwa na majina manne ambayo waliyapendekeza nayo ni New Maryland, Windsorland na Victoria, lakini pia Majina ya Kilimanjaro na Tabora yalipendekezwa na mwishowe Gavana aliyekuwa anajulikana kwa jina la Alfred Milner akaamua kuchukua jina Ziwa ambalo lilibatizwa Tanganyika na Wajerumani kama jina la Nchi yao!

Nafikiri ndio moja ya sababu ya Mlm.Nyerere kulikataa jina la Tanganyika baada ya Uhuru kwani kwake yeye bado lilikuwa ni jina la Mkoloni kama vile ilivyokuwa Ghana- Gold coast, au Zimbabwe na Zambia- Rhodesia, Malawi -Nyasa land na Hata Afrika Kusini au South Africa kuna kipindi ANC walikuwa hawalitaki kwamba ni jina la Kizungu na walitaka kutumia Azania badala yake!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom