Kingdom Finder
JF-Expert Member
- Jan 25, 2012
- 1,119
- 1,388
Kuna uchaguzi umefanyika Marekani katika Jimbo la Albama na mtu aliyeshinda ni wa Chama cha Democratic.
Mheshimiwa Trump amempongeza kwa ushindi wake pamoja na kwamba ni wa chama kingine. Je haya yanaweza kutokea Tanzania?
Ninatamani kuyaona haya kwenye nchi yangu. Tanzania ni ya waislam na wakristo. Dini zote tunajifunza kupendana lakini mbona tunaona mambo ya kishetani kwenye chaguzi zetu.
Ni lini sisi tutakuwa na roho ya upendo au ndyo tuseme pamoja na dini zetu, ushetani ndiyo ulioko mioyoni mwetu. Tusitegemee kuwa na maendeleo kwa siasa za chuki. Siku tutakapojifunza kupendana na kuheshimiana ndiyo siku tutaona maendeleo katika nchi yetu.
Ninawasihi watanzania tujifunze kupendana, tuondoe ushetani na ubinafsi nafsini mwetu. Kuna mataifa ambayo hata dini hawana lakini wanapendana na wana maendeleo. Sisi shida yetu ni nini?
Mheshimiwa Trump amempongeza kwa ushindi wake pamoja na kwamba ni wa chama kingine. Je haya yanaweza kutokea Tanzania?
Ninatamani kuyaona haya kwenye nchi yangu. Tanzania ni ya waislam na wakristo. Dini zote tunajifunza kupendana lakini mbona tunaona mambo ya kishetani kwenye chaguzi zetu.
Ni lini sisi tutakuwa na roho ya upendo au ndyo tuseme pamoja na dini zetu, ushetani ndiyo ulioko mioyoni mwetu. Tusitegemee kuwa na maendeleo kwa siasa za chuki. Siku tutakapojifunza kupendana na kuheshimiana ndiyo siku tutaona maendeleo katika nchi yetu.
Ninawasihi watanzania tujifunze kupendana, tuondoe ushetani na ubinafsi nafsini mwetu. Kuna mataifa ambayo hata dini hawana lakini wanapendana na wana maendeleo. Sisi shida yetu ni nini?