VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,800
Kwanza, ningejitenga haraka na Matamko yote ambayo yanatolewa kwa ajili yangu kupinga Maamuzi ya Kamati Kuu ya chama changu cha CHADEMA.Sababu yangu ingekuwa moja. Kwamba,nilishaahidi kufuata taratibu za chama kumaliza jambo husika.Nisingekaa kimya hivi.
Pili, 'nisingewatuma' vijana toka Dar na kwingineko kwenda Kigoma na mikoa jirani kuchora picha ya kupinga ziara inayoendelea ya Katibu Mkuu wa CHADEMA,Dr.Wilbrod Slaa. Hii ni kwa sababu mbili. Kwanza, kwakuwa naonekana mkorofi na mpenda misifa kwa haya yanayotukia. Pili, ziara husika ilishapangwa zamani tu. Wala haifanyiki kunipinga mimi wala kuelezea maamuzi ya Kamati Kuu. Vijana hawa 'niliowatuma' wanaharibu kabisa badala ya kunilinda.
Tatu, kwa ziara hiyo ya Dr.Slaa kuchorwa kuwa ina wingu na kumbe ni uwongo mtupu,mimi kama Zitto naonekana kuwa si maarufu kuliko chama. Naonekana kama wakawaida sana na chama kitasonga hata kama nitafukuzwa kabisa. Kigoma imekataa kuongopewa juu yangu. Sasa imejua kuwa taratibu za chama zinafuatwa.
Nne, ningewakoromea wana-CCM wote wanaojipambanua kama wapiganaji wangu. Mimi Zitto si CCM.Mimi ni CHADEMA.Kwanini wanishabikie hivi? Kukaa kimya kwangu bila mkwara wowote kwa 'mamluki' wa CCM hasa wale waliofukuzwa CHADEMA ni kukubali kuwa nahusika nao na yasemwayo ni kweli.
Tano, ningesubiri taratibu za chama zifuatwe ili nijue hatima yangu. Mambo yatakwenda vyema tu kichama.Ningeamini hivyo toka mwanzo hadi mwisho.
Pili, 'nisingewatuma' vijana toka Dar na kwingineko kwenda Kigoma na mikoa jirani kuchora picha ya kupinga ziara inayoendelea ya Katibu Mkuu wa CHADEMA,Dr.Wilbrod Slaa. Hii ni kwa sababu mbili. Kwanza, kwakuwa naonekana mkorofi na mpenda misifa kwa haya yanayotukia. Pili, ziara husika ilishapangwa zamani tu. Wala haifanyiki kunipinga mimi wala kuelezea maamuzi ya Kamati Kuu. Vijana hawa 'niliowatuma' wanaharibu kabisa badala ya kunilinda.
Tatu, kwa ziara hiyo ya Dr.Slaa kuchorwa kuwa ina wingu na kumbe ni uwongo mtupu,mimi kama Zitto naonekana kuwa si maarufu kuliko chama. Naonekana kama wakawaida sana na chama kitasonga hata kama nitafukuzwa kabisa. Kigoma imekataa kuongopewa juu yangu. Sasa imejua kuwa taratibu za chama zinafuatwa.
Nne, ningewakoromea wana-CCM wote wanaojipambanua kama wapiganaji wangu. Mimi Zitto si CCM.Mimi ni CHADEMA.Kwanini wanishabikie hivi? Kukaa kimya kwangu bila mkwara wowote kwa 'mamluki' wa CCM hasa wale waliofukuzwa CHADEMA ni kukubali kuwa nahusika nao na yasemwayo ni kweli.
Tano, ningesubiri taratibu za chama zifuatwe ili nijue hatima yangu. Mambo yatakwenda vyema tu kichama.Ningeamini hivyo toka mwanzo hadi mwisho.