Ningekuwa na uwezo ningecharaza bakora viongozi wote wa CHADEMA Taifa

Hapana, huu ni ujumbe tu wa hadharani kwa viongozi wote - nilio na simu zao na wale ambao sina. Kwamba, waachane na mambo ya siasa za vyama vichanga waelewe wako vitani na kosa moja lina gharama kubwa. Haiwezekani, kila baada ya masaa watu wanakuja kushindana nani anajua zaidi mambo ya chama na nani hajui halafu wakafikiria wanakitendea chama hisani. Hivi, Pentagon mnafikiri wote wanapendana? Hivi mnajua misuguano ya 'ego' ambayo iko kati ya Marines, Army na Navy? Lakini inapokuja vita huwezi kujua kuna tofauti! Wote wanaenda vitani wakipigania chini ya bendera ya Marekani!

Kwanini nitumie mfano wa mbali - tulipoenda vitani dhidi ya Uganda siyo wote walioenda kupigana walikuwa ni JWTZ! Wengine walikuwa recruited kutoka polisi, JKT, Magereza na hata mgambo! Wengine walitoka Zanzibar - haijalishi kama walikuwa hawaupendi Muungano! - lakini wote hawa walipigana na wengine kufa chini ya bendera ya Tanzania.

Hii ni changamoto ya Mwenyekiti mwenyewe kuweza kuhakikisha wapiganaji wake wana focus ya vita - a.k.a Arumeru Mashariki. Nimekaa na kusoma toka wiki ianze na kuona jinsi mada mbalimbali za kuiharibu chadema wakati wa vita zikitokea na watu wanafikiria ni mijadala ya kawaida tu. Well, kweli kabisa kwa vile sina uwezo tu ila ningekuwa na uwezo...

Ndio maana siwezi kuwa mwanasiasa.

Mwanakijiji writes and writes and writes but wapi bana! Watu wameweka gundi masikioni! Ruzuku bana!
 
Haya yote uliyoyaeleza MM nimeyakubali, lakini najua timu ya wataalamu wa CDM itawanasa tu hawa majeruhi wa BAVICHA wanaoleta mambo yao ya kiuanafunzi hapa, lakini ujumbe umefika
 
Nasubiri kuona uchaguzi wa mwaka 2015 ambao utakuwa wa muungano wa vyama vingi dhidi ya ccm.........''Kidume'' kipo pembeni kinaratibu mambo.........atakua nani Mkulu wa nchi...Prof Lipumba au EL?.......''Presure inapanda presure inashuka''.....
Angalizo kwa mulio karibu na ''Kidume'', kumbukeni ''kidume hana urafiki wa kweli anawagombanisha kwa maslahi ya nchi yake tu.
 
I hope so, I sure do.
Hakuna aliyesema CDM HQ kuna matatizo, na sidhani kama kuna tatizo kuubwa la kufanya watu wawe na wasiwasi hadi kuamua kuchapana viboko. Mapungufu yalianzia kwenye thread ya Tuntemeke na wenzake. Hakukuwa na Mnyika wala Zitto walioonyesha nguvu ya pamoja kama Chama kuwasaidia Slaa na Mkewe ambao reputation yao ilikuwa inagaragazwa vibaya sana. Na Mzee Mwanakijiji utaelewa haya mambo kuwa once one tempers with Slaa's reputation he/she tempers with CDM's reoutation as well.

Udhaifu ulianzia pale. Lakini tukumbuke kuwa Slaa ana watu wanaompenda na kumtakia mema yeye na familia yake kila saa na kila wakati. Ana watu wanaoumia wakiona kiongozi wao anasulubiwa kipropaganda isivyo halali tena kwa hoja za uongo. Watu hao miongoni mwao ni mimi. Na kujibu zile hoja nzito ilihitaji kukusanya ushahidi/utafiti. Utafiti ukaja kutaja watu ambao ni source ya mgogoro huu wa mtandaoni.

Tangu nitoe hoja kuhusu Mwigamba HAKUNA, narudia tena, HAKUNA kiongozi wa juu yeyote aliyekanusha wala kukubali zile hoja isipokuwa Mwalimu wangu Mkumbo ambaye na yeye nadhani ameingia mitini baada ya kukandamiziwa sehemu ndogo ya ushahidi na kuona asije akaharibu reputation yake. Kama lengo ni kuacha kampeni za Arumeru ziishe kwanza, bado viongozi wetu hawa hawapaswi kunyamaza. Kwa uzito wa tuhuma zilivyo alipaswa apatikane mtu reliable, akanushe na kama atazidiwa na members angepatikana kiongozi mwingine naye akanushe na mwisho hoja za Tuntemeke zingeishia hewani na watu tusingelazimika kufanya utafiti. Leo hii ile thread ya Tunte inakaribia kutengeneza page ya sabini, nani mbali ya Slaa na Josephine waliojitokewa walau kupinga au kukubali zile allegations?
Kwa hiyo, ubovu na madhara ya hapa tulipofikia umesababishwa na viongozi wenyewe. Labda wame-under estimate impactt ya kina Tuntemeke kumwaga tuhuma humu.
 
Inaonekana anti-virus ya Chadema haikamati spywares na trojans vizuri. Kuna haja ya kui-update or kui-replace ili iwe imara na up to date. Inawezekana hizo spywares na trojans bado hazijaidhuru system lakini kama hawata update anti-virus yao na kufanya security scanning mara kwa mara kuna uwezekano baadhi ya mafolder na mafaili yakawa infected na possibly system nzima ika-crash.

Pia internet connection yao iko slow sana. Inabidi watafute provider na modern ambavyo viko fasta zaidi katika ku-connect na internet. Pia wahakikishe wana strong firewall inayoweza kukabiliana na kutolewa au kuingizwa vitu kwenye system bila permission. Pia kuwa na popup blocker nayo ni muhimu sana kuzuia interference hasa pale system inapo-deal na suala muhimu kama kampeni za Arumeru Mashariki.

nimeipenda hii
 
  • Thanks
Reactions: EMT
Nimeshangazwa na 'like' ya John Mnyika kwenye uzi wa MM, ina maana yeye(Mnyika) yupo tayari kucharazwa viboko(kama MM angekuwa na uwezo huo) au yeye Mnyika hayumo kwenye list ya wachapwa viboko ila yupo tayari kuwaona viongozi wenzake wakiadhibiwa?

MM unaonesha umechukizwa sana na migogoro, na utendaji mbovu wa chama, lakini kwa nini usiitakie mema nchi badala ya chama? Hivi vyama leo vipo na kesho havipo lakini nchi ipo tu kwa uongozi wowote ule. Pia viongozi wa leo sio wa jana wala sio wa kesho. Kama CCM wanavyopenda kusema kuwa wanapokezana vijiti, inaashiria kubadilishana uongozi, lakini hatubadilishi nchi.

Nchi yetu ilikuwepo , ipo, na itaendelea kuwepo. Nadhani kuna haja ya kuonea uchungu nchi yetu na sio vyama.
 
Nimeshangazwa na 'like' ya John Mnyika kwenye uzi wa MM, ina maana yeye(Mnyika) yupo tayari kucharazwa viboko(kama MM angekuwa na uwezo huo) au yeye Mnyika hayumo kwenye list ya wachapwa viboko ila yupo tayari kuwaona viongozi wenzake wakiadhibiwa?

MM unaonesha umechukizwa sana na migogoro, na utendaji mbovu wa chama, lakini kwa nini usiitakie mema nchi badala ya chama? Hivi vyama leo vipo na kesho havipo lakini nchi ipo tu kwa uongozi wowote ule. Pia viongozi wa leo sio wa jana wala sio wa kesho. Kama CCM wanavyopenda kusema kuwa wanapokezana vijiti, inaashiria kubadilishana uongozi, lakini hatubadilishi nchi.

Nchi yetu ilikuwepo , ipo, na itaendelea kuwepo. Nadhani kuna haja ya kuonea uchungu nchi yetu na sio vyama.

kuza upeo wako mkuu. MMkJ hana maana ya kuwachapa fimbo. Anatoa busara zake. Hata mi nita-like nikitumia PC
 
Hakuna aliyesema CDM HQ kuna matatizo, na sidhani kama kuna tatizo kuubwa la kufanya watu wawe na wasiwasi hadi kuamua kuchapana viboko. Mapungufu yalianzia kwenye thread ya Tuntemeke na wenzake. Hakukuwa na Mnyika wala Zitto walioonyesha nguvu ya pamoja kama Chama kuwasaidia Slaa na Mkewe ambao reputation yao ilikuwa inagaragazwa vibaya sana. Na Mzee Mwanakijiji utaelewa haya mambo kuwa once one tempers with Slaa's reputation he/she tempers with CDM's reoutation as well.

Udhaifu ulianzia pale. Lakini tukumbuke kuwa Slaa ana watu wanaompenda na kumtakia mema yeye na familia yake kila saa na kila wakati. Ana watu wanaoumia wakiona kiongozi wao anasulubiwa kipropaganda isivyo halali tena kwa hoja za uongo. Watu hao miongoni mwao ni mimi. Na kujibu zile hoja nzito ilihitaji kukusanya ushahidi/utafiti. Utafiti ukaja kutaja watu ambao ni source ya mgogoro huu wa mtandaoni.

Tangu nitoe hoja kuhusu Mwigamba HAKUNA, narudia tena, HAKUNA kiongozi wa juu yeyote aliyekanusha wala kukubali zile hoja isipokuwa Mwalimu wangu Mkumbo ambaye na yeye nadhani ameingia mitini baada ya kukandamiziwa sehemu ndogo ya ushahidi na kuona asije akaharibu reputation yake. Kama lengo ni kuacha kampeni za Arumeru ziishe kwanza, bado viongozi wetu hawa hawapaswi kunyamaza. Kwa uzito wa tuhuma zilivyo alipaswa apatikane mtu reliable, akanushe na kama atazidiwa na members angepatikana kiongozi mwingine naye akanushe na mwisho hoja za Tuntemeke zingeishia hewani na watu tusingelazimika kufanya utafiti. Leo hii ile thread ya Tunte inakaribia kutengeneza page ya sabini, nani mbali ya Slaa na Josephine waliojitokewa walau kupinga au kukubali zile allegations?
Kwa hiyo, ubovu na madhara ya hapa tulipofikia umesababishwa na viongozi wenyewe. Labda wame-under estimate impactt ya kina Tuntemeke kumwaga tuhuma humu.
Kweli kabisa mkuu! Kuna tuhuma angeweza kujibu Dr Slaa lakini zingine viongozi wengine walipaswa kujibu.mfano mambo yanayotaka udhibitisho wa vikao halali ni vizuri wengine wangekuja kujibu na mwisho Dr Slaa angehitimisha kuweka mambo sawa! binafsi ingawa nilikuwa nimebanwa lakini niliumia kuona heshima ya Mzee wetu ikichezewa na hakuna anayejibu! Ndio maana wengine tulijitahidi kujibu yale yaliyo wazi! Viongozi wawe makini pale heshima ya mtu kama Dr Slaa inapochezewa namna hii! Kwasasa ndiye jemedari wa vita ya ukombozi!
 
hii ni strategy ya ccm kuwatoa cdm kwenye concentration ya uchaguzi wa arumeru,nafikiri slaa kashasoma uzi wa tuntemeke na atautolea ufafanuzi baada ya uchaguzi like he always does.. hivi mwigamba kapewa condition na ccm ya kumfutia kesi yake ya uchochezi kwa ku-snitch mambo ya cdm?maana naona watu wanamlink na ***** uliomwagwa na tunte!!!duh,kweli vita ya ukombozi inataka watu wenye moyo.
 
KWA NINI UTAMANI KUCHAPA WATU VIBOKO? Mzee Mwanakijiji wazo ni zuri sana lakini tamanio ulilonalo la kuwacharaza viboko kama wasiposikia lina element ya udikteta.

Tamanio zuri ni kuwafanya wakusikilize kwa mazungumzo ama ushauri lakini bila kucharazana viboko - adhabu tuwaachie Mahakama na Magereza. Naamini kuna njia bora na yenye matokeo mazuri kuliko hiyo ya kucharaza viboko - hivyo usichoke lakini bila viboko.
Kama Mzee Kifimbo alivyopenda kufanya, just Imagine mtu atamanie kukucharaza viboko ati MM HUSIKII - si utaona si MUUNGWANA.
 
Hivi hawajasikia yaliyomkuta yule "rogue soldier" wa US kule Afghanistan? Badala ya kupigana na Taleban kaenda kuwaua watu 16 wasio na hatia? Unafikiria jeshi lingemuacha huko huko? No, wamemchukua na kumrudisha US na kumsweka kwenye gereza lenye ulinzi mkali. Huwezi ukiwa vitani ugeuze silaha kwa wenzako au watu wasio maadui haalafu ukaendelea. Kama kuna "mhuni" mmoja kama ulivyosema itanishangaza kama CDM haina intelligence capabilities ya kumjua na kumuondoa kabisa. Haya ya kuvumiliana na kuoneana huruma ndio mwanzo wa kuvurugana. Its war out there!

Pal,

Kuna mhuni mmoja kungwi na vibaka kama wanne, tatizo CDM intelligence bado haijaelewa approach yao ya sasa is suicidal!!! and wakimuondoa ndio balaa zaidi kwani walimfikisha waliwato

dawa tu ni kuangalia namna ya kupunguza huu ujinga unaoendelea.... na ujumbe tu kwa huyo kungwi, aondoke kwa amani, anachofanya, chaweza hata kumcost dearly, dunia ya leo iko desperate sana, na watu si wazuri kihivyo
 
Kweli kabisa!! Kama kuna vitu vinanitibua sasa hivi - na sijachangia sana - ni haya malumbano, vijembe, uchimvi na mashambulizi ya "wao kwa wao". Vitani kunakuwa na "friendly fire" lakini hii siyo "friendly fire" tunachoshuhudia ni silaha zimegeuzwa toka kwa CCM na kuelekezwa kwa CDM wenyewe ndani kwa ndani. Badala ya wapiganaji wote kusimama kupigana na kusonga mbele, muda mwingine unatumiwa kupigana wenyewe, kujeruhiana na kutafuta muda kugangana.

Sasa hivi CCM hawagombani! Wana tofauti kubwa zaidi kuliko zilizoko ndani ya CDM lakini wanajua kabisa kuwa mkiwa vitani akili, mikakati, silaha zenu zote zinaelekezwa kwa adui! Lakini, kwa vyovyote vile inaonekana CDM itajikuta inatumia muda mwingi zaidi kujitetea na kujibu hoja za wao kwa wao ndani ya Chama badala ya kutulia kupanga mikakati ya kushinda! Na hapa ndipo unapoona mkakati wa Wassira kwa mfano na wengine tuliowaona siku hizi chache, wote wanajitahidi kuwapa CDM sababu ya kugongana wao kwa wao kiasi kwamba wakishawatupia hoja CDM wanabaki kujibizana na kutafutana badala ya kupigana na adui!

Ndio maana ninasema ningekuwa na uwezo - bahati mbaya sina - ningehakikisha watu wanaoitwa wapiganaji wanakuwa na akili ya kivita (war mentality). When you are fighting in a war your collective mentality is shaped in such a way that you are absolutely focused on defeating the enemy! You don't spend your time to start worrying about your generals!

Binafsi ningewaita hawa wote wanaotajwa pamoja - ningejaribu kuwaweka pamoja waseme tofauti zao ni nini - halafu kama bado hawataki kusikilizana na kurudisha akili zao kwwenye vita ningewacharaza bakora kama "Mzee Kifimbo"! Halafu ningewaondoa kabisa kwenye mambo ya kampeni! Mwenyekiti yuko wapi?

C'mmon now! mnataka kushinda au kushindana? CDM Taifa safisheni migongano yenu hatutaki mtafute kisingizio cha kutofanya vizuri au kuendeleza malumbano baada ya uchaguzi. Hakuna mtu mwenye uwezo wakuonesha uongozi na kutuliza hivi vita vya wenyewe kwa wenyewe? Waacheni CCM wawashambulie kwani ni haki yao; na nyinyi msiwaonee huruma!

Hivi huu muda wa kuandika na kuchunguzana na kujibizana wakati mko vitani mnautoa wapi? Sijaona mtu kaandika kitu cha maana kuelezea kushindwa kwa sera za CCM Arumeru Mashariki? Sijaona mtu akikosoa kushindwa kwa sera hizo wakati wa Mkapa - zaidi ya watu kutumia muda kufurahia majibu ya Vincent Nyerere!; Vincent Nyerere angemchambua Mkapa na kushindwa kwa sera zake ingekuwa bora zaidi kuliko kugombania jina; hilo angemuachia Madaraka! grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr!

Nitafafanua zaidi katika "Arumeru East Contest: CHADEMA'S own Battle for Fallujah"


  1. CHADEMA hakuna malumbano ya wenyewe kwa wenyewe, isipokuwa kuna jamii ya watu mamluki wanaotumiwa na magamba kutaka kuonyesha ndani ya chadema kuna vita ya wenyewe kwa wenyewe
  2. What we see ni kwamba they all focused kwenye uchaguzi wa Arumeru
  3. Jambo la msingi kuwa they are going foward as a team, with the same standard and the same product
 
umenena vema ni wakati wa kuwa na single focus kwenye critical issues kama ya uchaguzi wa Arumeru mashariki. CDM please settle down you petty issues
 
Kweli MMM, ni vizuri uiandae vyema bakora yako....

Natamani Ben (wa JF) aje hapa, maana kuna fukuto nimelipata sijalielewa.

Na naomba ukianza kuwachapa uwaulize na maswali ya wanatutaka nini watz!

JouneGwalu,

Unatamani Ben yupi wa JF aje hapa? Kama ni mimi,nipo mkuu.....Ni fukuto gani umelipata?nitakuelewesha...............!

kwa bahati mbaya network inasumbua niko kanda ya ziwa ndani vijini Geita huku.Watanzania wanateseka kutokana na sera mbovu za CCM katika uwekezaji.Leo hii tumezalisha wakimbizi.Hawana wa kuwasemea zaidi ya kutegemea wanaharakati na chama kinachosubiri muda kiishinikize serikali kwa njia Rasmi na isiyo rasmi wapate haki yao.Pichani ni wahanga wa sera mbovu za uwekezaji za CCM zilizozalisha wakimbizi kutoka maeneo yaliyochukuliwa na mgodi wa geita gold mine(GGM).Tujue jukumu kubwa tulilo nalo la kukomboa taifa kutoka katika makucha haya mabaya ya CCM,chadema tujiimarishe tubebe jukumu hili bila kuelemewa


View attachment 49710View attachment 49711View attachment 49712



Kweli kabisa!! Kama kuna vitu vinanitibua sasa hivi - na sijachangia sana - ni haya malumbano, vijembe, uchimvi na mashambulizi ya "wao kwa wao". Vitani kunakuwa na "friendly fire" lakini hii siyo "friendly fire" tunachoshuhudia ni silaha zimegeuzwa toka kwa CCM na kuelekezwa kwa CDM wenyewe ndani kwa ndani. Badala ya wapiganaji wote kusimama kupigana na kusonga mbele, muda mwingine unatumiwa kupigana wenyewe, kujeruhiana na kutafuta muda kugangana.

Sasa hivi CCM hawagombani! Wana tofauti kubwa zaidi kuliko zilizoko ndani ya CDM lakini wanajua kabisa kuwa mkiwa vitani akili, mikakati, silaha zenu zote zinaelekezwa kwa adui! Lakini, kwa vyovyote vile inaonekana CDM itajikuta inatumia muda mwingi zaidi kujitetea na kujibu hoja za wao kwa wao ndani ya Chama badala ya kutulia kupanga mikakati ya kushinda! Na hapa ndipo unapoona mkakati wa Wassira kwa mfano na wengine tuliowaona siku hizi chache, wote wanajitahidi kuwapa CDM sababu ya kugongana wao kwa wao kiasi kwamba wakishawatupia hoja CDM wanabaki kujibizana na kutafutana badala ya kupigana na adui!

Ndio maana ninasema ningekuwa na uwezo - bahati mbaya sina - ningehakikisha watu wanaoitwa wapiganaji wanakuwa na akili ya kivita (war mentality). When you are fighting in a war your collective mentality is shaped in such a way that you are absolutely focused on defeating the enemy! You don't spend your time to start worrying about your generals!

Binafsi ningewaita hawa wote wanaotajwa pamoja - ningejaribu kuwaweka pamoja waseme tofauti zao ni nini - halafu kama bado hawataki kusikilizana na kurudisha akili zao kwwenye vita ningewacharaza bakora kama "Mzee Kifimbo"! Halafu ningewaondoa kabisa kwenye mambo ya kampeni! Mwenyekiti yuko wapi?

C'mmon now! mnataka kushinda au kushindana? CDM Taifa safisheni migongano yenu hatutaki mtafute kisingizio cha kutofanya vizuri au kuendeleza malumbano baada ya uchaguzi. Hakuna mtu mwenye uwezo wakuonesha uongozi na kutuliza hivi vita vya wenyewe kwa wenyewe? Waacheni CCM wawashambulie kwani ni haki yao; na nyinyi msiwaonee huruma!

Hivi huu muda wa kuandika na kuchunguzana na kujibizana wakati mko vitani mnautoa wapi? Sijaona mtu kaandika kitu cha maana kuelezea kushindwa kwa sera za CCM Arumeru Mashariki? Sijaona mtu akikosoa kushindwa kwa sera hizo wakati wa Mkapa - zaidi ya watu kutumia muda kufurahia majibu ya Vincent Nyerere!; Vincent Nyerere angemchambua Mkapa na kushindwa kwa sera zake ingekuwa bora zaidi kuliko kugombania jina; hilo angemuachia Madaraka! grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr!

Nitafafanua zaidi katika "Arumeru East Contest: CHADEMA'S own Battle for Fallujah"

Kupishana kwa hoja ndani ya taasisi ni jambo la kawaida (namaanisha kwa hoja na sio mipasho ya kijinga). Ukiwa na kampuni au taasisi halafu kukakosekana conflict basi ujue taasisi hiyo ni mfu.Kwa wale waliosoma Management wanalijua hili. Changamoto inakuwa ni kwa jinsi gani ya kubalance conflict ili iwe healthy kwa taasisi husika ama chama cha siasa.Ukishindwa ku-control conflict basi tatizo linaanzia hapo.Conflict is necessary,human beings are social animals so ni lazima kuwe na selfish interests lakini zile selfish interest ziki-overshadow collective interest ndiyo tatizo litaibuka litakaloumiza Taasisi.

Mwanakijiji,Umeandika post nzuri.Ni kweli migogoro imekuwa kikwazo kikubwa katika demokrasia yetu.Chama cha NCCR-Mageuzi kilichangia kupitia migogoro yake kudumaza demokrasia.Kwa hiyo ushauri aliyoutoa mwanakijiji,ni work up call kwa chama.Ni lazima tuimarishe mshikamano ndani ya chama kama kweli tunataka kufanikiwa katika vita hii,we must put our house in order.

Pia,kuhusu vijana wanaoingia mtandaoni kwa majina ya kuficha na kuanika au kuchafua chama hili ni changamoto.Pia ni changamoto kwa wale wasiokubali kukosolewa.vyama vya siasa vimeundwa na vinaongozwa na watu kwa hiyo ni lazima kuwe na mapungufu madogo na makubwa.Kitakachotuokoa kwa level ambayo tumefikia,ni spidi ya kurekebisha mapungufu na tusonge mbele.

Tatizo lililoko kwa vyama vyote Tanzania ni kutokujikita kwenye itikadi.Kwa bahati mbaya tuliingizwa mkenge kwenye mfumo huu wa demokrasia ya magharibi bila kutoa darasa la kutosha kuhusu itikadi.Hata elimu ya uraia shule ya msingi na sekondari imekuwa ya kutoa definition ya Ideology tu.Ndiyo maana hata siasa za hovyo zinashabikiwa,ndiyo maana majungu yanageuka kuwa sera.Mfumo huu tuliouiga vibaya unakaribia kutufanya tugeuke kuwa taifa la watu wa matukio na kutumia vigezo vya sura.Tunageuka taifa la ki-facebook.Kwa hiyo ni jukumu la vyama vya siasa sasa kurudi katika hoja ya issue fulani based on Ideology

Katika mikakati ya kivita,chadema imefikia hatua ambayo ni muhimu sana.Terrain/Situational Positioning,we should now look at the three general areas of resistance (distance, dangers, and barriers).Hapo kwenye danger ni kuzuia mifumo yetu kuingiliwa na pia tuepuke disruption from within.We need harmony.Tusipokuwa makini tunaweza kujikita sasa tuko katika diffencive side badala ya kuwa kwenye offensive side.So far katika kila move chadema imefanya strategic positioning nzuri,kwa wapenda mabadiliko wote tuungane katika kutoa sapoti.Ushauri ambao ni sensitive zaidi unaweza kupelekwa moja moja kwenye chama ili kuepusha kuwafaidisha mahasimu wetu(Adui yako vitani mwombee njaa hutashitakiwa kwa uhalifu wa kivita) kwa njia iliyo rasmi au isiyo rasmi.

Na pia vijana wa chadema tulikoko mitandaoni,tuache majungu.Tukubali kukosoana kwa staha.Mkandara mara nyingi amekuwa akitukanwa kwa sababu katoa ushauri ambao baadhi ya vijana (kwa sababu ya ulimbukeni wa siasa tu) ambao walijita wanachadema hawakuufurahia.Hii ni tabia chafu na ya hovyo

Na pia Mwanakijiji na wakuu wengine,baadhi ya vijana hapa msiwachukulie serious kwani wengine ni wanatumiwa na wapinzani wa chadema kisiasa kwa kujitangaza wanachadema huku wakitukana watu ili ionekana chadema ni chama cha wahuni au chama cha watu wasio na ustaarabu wa kisiasa.Chadema imekomaa,iko juu ya siasa za majungu.Chadema iko at par na siasa za hoja.Changamoto ndogo zinazojitokeza ni za kufanyia kazi tu ili zisigeuke kuwa tatizo kama inanvyoonekana sasa

Changamoto tuliyo nayo ni kuigeuza fan base kuwa loyal base.Hawa vijana wanaoandika andika mambo fulani aidha yawe na ukweli ama yawe ya uongo ni kwamba inaonyesha tatizo kwa kuwa wangekuwa loyal kwa chama wasingetumia hii Approach(nimefanya assumption,suppose kama ni wanachadema kweli halafu wanachoandika kikawa na ukweli),ukikipenda chama hutakitukana na hutakidhoofisha kwa hali yoyote ile (sitetei kuficha uovu),utakilinda na utatumia njia ya staha katika kushinikiza marekebisho au mabadiliko fulani bila ku-harm interest za chama..CCM wapo hapa walipo kwa sababu chini ya Mwalimu Nyerere tangu enzi za TANU inaonekana aliigeuza fan base kuwa loyal base kwa chama.Ndiyo maana unaona wazee wa sasa pamoja na kwamba baadhi wanaishabikia chadema lakini unawakuta loyality yao kwa CCM inawazuia kufanya maamuzi fulani.(kwa CCM loyal base yao ni maafa kwa taifa na vizazi vijavyo).Sasa chadema tuigeuze hii fan base tuliyo nayo kubwa igeuke kuwa loyal base(huu ni mjadala wa siku nyingine)

Kwa wanachadema wote,vita yetu ni dhidi ya CCM.Turudi kwenye kanuni ya vita tusitoke nje ya mikakati na hesabu yetu.We should review our plans daily.Turudi kwenye chati,tuangalie roadmap. Plans & Calculations.Let us explore the five fundamental factors (the Way, seasons, terrain, leadership, and management) and other elements that determine the outcomes of political engagements. By thinking, assessing and comparing these points, a commander can calculate his chances of victory. Habitual deviation from these calculations(kugombana wenyewe na majungu yasiyo na tija bila hoja zinazofo-focus katika mass interest) will ensure failure via improper action.

Tujiimarishe tubebe jukumu la kuwapigania hawa watanzania
 
Nadhani lesson kubwa ni kwamba hao vijana bora wapewe nafasi ya kuongea ndani ya chama ili wasije kumwaga mchele huku barabarani. Kuza demokrasia kwenye vyama sio kukusanyana ndugu kibao kama ambavyo Chadema imefanya.
 
Nadhani lesson kubwa ni kwamba hao vijana bora wapewe nafasi ya kuongea ndani ya chama ili wasije kumwaga mchele huku barabarani. Kuza demokrasia kwenye vyama sio kukusanyana ndugu kibao kama ambavyo Chadema imefanya.

watu wa namna hiyo hawastahili kupewa nafasi yoyote maana yake ni kuwa wanaonesha traits za ufuasi na siyo uongozi. you do not accommodate mediocrity
 
  1. CHADEMA hakuna malumbano ya wenyewe kwa wenyewe, isipokuwa kuna jamii ya watu mamluki wanaotumiwa na magamba kutaka kuonyesha ndani ya chadema kuna vita ya wenyewe kwa wenyewe
  2. What we see ni kwamba they all focused kwenye uchaguzi wa Arumeru
  3. Jambo la msingi kuwa they are going foward as a team, with the same standard and the same product
Hata mimi ningesema hivi hivi, haya ni maneno yanayotakiwa kusemwa na kiongozi yeyote hasa wakati wa vita.
 
Kweli MMM, ni vizuri uiandae vyema bakora yako....

Natamani Ben (wa JF) aje hapa, maana kuna fukuto nimelipata sijalielewa.

Na naomba ukianza kuwachapa uwaulize na maswali ya wanatutaka nini watz!
Huyo jamaa dhambi ya usaliti wa chama itamfuata popote atakapojificha.
 
Back
Top Bottom