Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,197
- 25,516
Alihama CCM na sasa amerejea 'nyumbani'. Alipojiunga na CHADEMA,aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho,Balozi Dr. Wilbrod Slaa alijitokeza na kutoa hotuba ndefu kuhusu kujiweka pembeni na siasa za vyama.
Pamoja na mambo mengine,Balozi Slaa aliweka wazi kutomuunga kwake mkono Lowassa ndani ya CHADEMA/UKAWA kwa kumchambua vilivyo kwenye mkutano wake wa Serena Hotel na hata mahojiano yake kwenye runinga ya StarTV ya jijini Kwanza.
Balozi Slaa aliwataka viongozi na wanachama wa CHADEMA/UKAWA kujiuliza kama Lowassa ni liability au asset.Kwake Balozi Slaa,Lowassa alikuwa liability kwa CHADEMA/UKAWA. Kwake yeye,Lowassa hakufaa na hivyo alijitenga naye.
Sasa Lowassa amerejea CCM anakokuita nyumbani. Kwanini swali la iwapo Lowassa ni liability au asset kwa CCM hivisasa lisiulizwe na kujibiwa na makada wa CCM na hata Balozi Slaa? Wale 'waliomkimbia Lowassa CHADEMA/UKAWA watamkimbia tena huko CCM?
Wakati utajibu hadi kusaza...
Pamoja na mambo mengine,Balozi Slaa aliweka wazi kutomuunga kwake mkono Lowassa ndani ya CHADEMA/UKAWA kwa kumchambua vilivyo kwenye mkutano wake wa Serena Hotel na hata mahojiano yake kwenye runinga ya StarTV ya jijini Kwanza.
Balozi Slaa aliwataka viongozi na wanachama wa CHADEMA/UKAWA kujiuliza kama Lowassa ni liability au asset.Kwake Balozi Slaa,Lowassa alikuwa liability kwa CHADEMA/UKAWA. Kwake yeye,Lowassa hakufaa na hivyo alijitenga naye.
Sasa Lowassa amerejea CCM anakokuita nyumbani. Kwanini swali la iwapo Lowassa ni liability au asset kwa CCM hivisasa lisiulizwe na kujibiwa na makada wa CCM na hata Balozi Slaa? Wale 'waliomkimbia Lowassa CHADEMA/UKAWA watamkimbia tena huko CCM?
Wakati utajibu hadi kusaza...