Ningekutana na rais Magufuli leo ningemshauri abadilishe noti ya elfu kumi

Chikawe Jr

Member
Jun 6, 2017
23
85
Kuna kanuni inasema ""anayekuringishia vyako alivyokuibia mwambie basi sivitaki tena"" ndio njia pekee ya kujikwamua na maumivu ya muda mrefu yanayotokana na kuibiwa au kudhulumiwa.

Kwa miaka 20, Tanzania imeingia katika Rushwa na UFISADI mkubwa na kusababisha kundi la watu wachache kuwa na NGUVU YA PESA na kutawala mzunguko wa fedha nchini. Hii imethibitika baada ya kikundi kidogo cha watu wenye maslahi ya kudumu ya kinyonyaji kuamua kuzifungia Pesa zao zilizokuwa katika mzunguko na kuzificha ndani(Home made shelves)

Athari kubwa iliyojitokeza baada ya kundi hili lenye nguvu kuficha UKWASI WAO ni pamoja na;-
1) Kupungua kwa fedha katika mzunguko.
2) Kupungua kwa uwezo wa kununua
3) Biashara za kati kufa
4) Kupotea kwa ajira za watu
5) Manung'uniko ya hali ngumu ya kiuchumi kwa watanzania hasa wa hali ya chini

Kwa uelewa wangu mdogo, pesa ni alama ya thamani katika kubadilishana huduma au bidhaa. Hakuna sababu iliyokuu ambayo inaweza kumfanya mtu akaficha pesa isipokuwa kuikomoa serikali na wananchi wake.

Wapo watu wanaosema pesa hizi zimebadilishwa 'interm of dollars' na kufichwa, lakini mimi nasema la hasha, pesa hizi zimefichwa katika hali yake ya Tshs. Kwa nini nasema hivyo, kuna sababu kuu 2 kama ifuatavyo;-
1) Kama ingekuwa zimefichwa interm of dollar, Tanzania tusingekuwa na changamoto ya mzunguko wa fedha hasa ndani kwa sababu Tshs ingekuwepo lakini Dollar ndio ingepotea sokoni.Ikumbukwe hakuna nchi yeyote duniani wanatumia currency yetu isipokuwa sisi wenyewe.

2) Changamoto ya kupungua kwa bidhaa zinazoingia nchini (Import trade) sio mitaji isipokuwa wanunuzi hawana uwezo wa kununua bidhaa sokoni kutokana na kupungua kwa fedha katika mzunguko wa maisha ya kila siku. (Currency flow in Business).

Katika hili tunaweza kujikwamua kwa njia nyingi lakini iliyo kuu ni Kubadilisha NOTI ya Elfu 10.
Kwanini kubadilisha NOTI ya elfu kumi kunaweza kutusaidia ni kwa sababu hakuna namna yoyote iliyobora itakayokuwezesha kumfanya mtu au kikundi cha watu walioficha fedha mafichoni isipokuwa tu watakapoona baada ya muda hazitatumika tena hivyo watalazimika kuziingiza katika mzunguko.

Na hili linaweza kusimamiwa kwa njia mbili
1) Kufanya uhakiki wa mitaji ya mabenki yote nchini
2) Kutoa tangazo la kusudio la kubadili NOTI ya elfu 10 na kuweka muda unaofaa kabla ya kuchukua hatua hiyo.
2) Kuweka viwango maalumu kwa mtu kubadilisha fedha zake katika mabenki ya kawaida na kama atazidi kiwango hicho basi atatakiwa kubadilisha fedha hizo Benki kuu kwa utaratibu maalumu.( Ninaposema utaratibu maalumu ni pamoja na kuhojiwa)

Kwa kufanya hivi tutatoa fursa kwa walioficha fedha kuchagua aidha fedha zao ziishie kuwa makaratasi ambayo hayatumiki tena au wayalete katika mzunguko na kuongeza uwekezaji.

Jambo hili lina tija kubwa kama litafanywa kitaalamu lakini nachelea kusema inawezekana wanaokushauri USIBADILI NOTI NAO WAMEFICHA MAJUMBANI MWAO.

Kama tunaweka mambo sawa basi hata ili linaweza kutusaidia

Nahitaji kuona hoja za wachumi hapa. Nini maoni yako?
Chikawe jr.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo unachosema hakina mantiki yoyote kweny uchumi ....
Gharama ya kubadilisha hiyo NOTE ya 10000 ni kubwa kuliko walizo ficha kama ni kweli ..... hiyo hela ni bora SERIKALI ilipe madeni ya ndani na hela itafika MITAAN....

Na haingii akilini mtu mwenye akili timamu akaweka hela ndani tena hela yenyew Shilling.... na wafanya biashara wakubwa mara nyingi wanakonection ambayo ni kubwa huwez kuitrack hata ufanye nini .

Zimwi likujualo......
 
Kama utamlipa yule yule aliyekusudia kuficha ni kujidhoofisha zaidi.

Ninachosema kina mantiki kubwa sana katika uchumi na mifano hai ipo hata MAREKANI walishatumia mbinu hii kujinasua katika mdororo wa uchumi na kuiongezea nguvu serikali ya kusimamia fedha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inatakiwa ifutwe kabisa...sio kubadiriswa....inachangia kushusha thamani ya pesa yetu...10000.5000..zote ziondoke.....ndio uchumi utakua umekua kweli.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo unachosema hakina mantiki yoyote kweny uchumi ....
Gharama ya kubadilisha hiyo NOTE ya 10000 ni kubwa kuliko walizo ficha kama ni kweli ..... hiyo hela ni bora SERIKALI ilipe madeni ya ndani na hela itafika MITAAN....

Na haingii akilini mtu mwenye akili timamu akaweka hela ndani tena hela yenyew Shilling.... na wafanya biashara wakubwa mara nyingi wanakonection ambayo ni kubwa huwez kuitrack hata ufanye nini .

Zimwi likujualo......
Jamaa nazani ni mwanafunzi sasa nazani atakuwa ameanza kusoma somo la Influation

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfichaji wa pesa ni serikali. Refer withdrawal ya pesa zake katika taasisi binafsi za kibenki na kwenda kuzisweka BOT.

Yet amelipa cash baadhi ya huduma na manunuzi ambayo bado hayajaanza kutoa mzunguko mzuri wa pesa. Hapa refer ununuzi wa ndege na ujenzi wa reli.

Bado hapohapo serikali inalipa baadhi ya watumishi wa umma mara mbilimbili katika baadhi ya nafasi.

Kwa haya yote bado tuu anatafutwa aliyeficha pesa.?
 
Kiasi cha fedha kilichotolewa na serikali ni Bilion 500 tu na ambayo haifiki hata 1/4 ya fedha zilizokuwepo kwenye mzunguko. Pia mabenki yanaombwa kukopa kwa riba ya 9% lakini hayakopi kuna shida naiona hapa

Aidha kuna kikundi kinahujumu jitihada za serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
watu wa leo sio wa miaka ya 70 na 80,,hakuna mtu anayeficha hela kwa local currency,,,,enzi za hela kutelekzwa kwenye magunia zilishapita,,
 
Hiyo unachosema hakina mantiki yoyote kweny uchumi ....
Gharama ya kubadilisha hiyo NOTE ya 10000 ni kubwa kuliko walizo ficha kama ni kweli ..... hiyo hela ni bora SERIKALI ilipe madeni ya ndani na hela itafika MITAAN....

Na haingii akilini mtu mwenye akili timamu akaweka hela ndani tena hela yenyew Shilling.... na wafanya biashara wakubwa mara nyingi wanakonection ambayo ni kubwa huwez kuitrack hata ufanye nini .

Zimwi likujualo......
Huyo jamaa atakuwa na PhD ya chemical economics from callomedge university

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbona tayari wameshaibadilisha ingawa ni sehemu chache ila watu hawajashtukia!

SONY Xperia Z5 Premium
 
mi mambo haya siyajui sana but kama nimeficha hela kwa akil zangu mkibadili nazileta naficha tena ha ha ha
 
Hahaaah yaani kwa akili hizi ungekuwa raisi ndo tungezidi kuwa maskini...kwa hiyo kwa akili zako mtu hata akiamua kuficha pesa ataficha hizi za madafu ambazo kila siku zinashuka thamani...watu wanaficha dollar wewe...alafu acha kulialia kila cku kama raisi wako
 
Azingatie sheria pamoja na mikataba ya kisheria za wakandarasi/wawekezaji n.k sio kwenda kwa hisia tuu pasipokuja madhara yake.
Watu walisha kubaliana miaka ndenda miaka rudi huwezi kuingilia makubaliano tumeliwa tumeliwa tuu. Better formulate other rules and policies...
 
Katiba ya nchi ibadilishwe na kil kipengele cha kinga Rais kitolewe plz hiki kimetufikisha hapa.
 
Kwa uchumi wa sasa ni ngumu sana kukomoa watu walioficha pesa......maana naweza peleka zote kwenye vikoba tofauti tofauti na nikakopa upya, au nikanda nunua dola then naweka maskani natumia mdogo mdogo

SONY Xperia Z5 Premium
 
Back
Top Bottom