Bhikalamba
JF-Expert Member
- Dec 6, 2015
- 1,697
- 2,346
I like Mchengerwa is very smart , kweli alifaa sana utumishi au angemuweka Tamisemi. Sema tu mama kahofia vimaneno vya hapa na pale eti tu kwa kuwa ni mkwe.
Ashauri yaliyo sawa pale anapoona raisi kayumba sasa kama ni ndio mzee kila jambo wa Kasi gani?KWAIYO wee ulitaka uwe waziri afu upingane na maelekezo ya mteuzi wako?
Hakika mambo ni mengi muda ni mchacheHeshima sana wanajamvi,
Mosi unatakiwa kujua majukumu ya Waziri wa Utumishi na Utawala bora.
Kifupi sana hii wizara pamoja majukumu yake ya kusimamia utumishi lakini pia kuna huu utawala bora.Utawala bora maana yake ni pamoja na kuisimamia TISS & TAKUKURU.Hii ni moja ya Wizara nyeti kweli kweli.TISS imo kila mahali kuanzia uraiani,majeshi yote ya Ulinzi na Usalama & mashirika yote ya umma na sehemu zote nyeti.TISS ina jukumu la kuwatafuta na kuwapachika wale maJAJI wa kuchonga.
Wizara hii tunaweza kusema pasipo shaka ndio utoa DIRA namna ya uendeshaji nchi kuanzia teuzi nyeti mbali mbali.Kifupi kabla haujateuliwa hawa jamaa wanakuwa na record zako zote.
Nafikiri huyu Mwamba kilichomwondoa pale ni mambo mawili.
Moja zipo tuhuma kwamba yeye na Majaliwa waliachiwa mambo yote ya ulinzi na usalama huku Bi Mkubwa akijishughulisha na masuala madogo madogo.Tuhuma hizi zilitolewa na yule Mwamba aliyetandikwa risasi nyingi lakini Mwenyezi Mungu akamnusuru na umauti.Dogo akitumia ukaribu baina yake na Bi Mkubwa (Mama Mkwe) alijikuta akipitiliza na Wazee wa nchi wakashauri ni vyema akaondolewa mara moja.
Waziri wa Utawala Bora ndiye aliyeshauri kesi ya yule Mwamba ipelekwe Mahakamani kwakuwa kuna ushahidi wa kutosha tena usioacha mashaka mashaka.File lilipopelekwa Wizara ya yule Waziri mtoa macho likapata baraka zote.Baada ya kesi kuunguruma Mahakamani mambo ya PGO na kina Kingai yakaonekana hovyo kabisa kesi haina mashiko.Ikabidi muhimili uliojichimbia zaidi kutumia njia ya mkato (MAJAJI MICHONGO) kuepeka aibu.
Majaji Michongo wamejitahidi sana tena sana kuibeba JAMHURI na wengine kupandishwa cheo lakini kila hatua au kadri siku zinavyosonga mbele KESI ya UGAIDI inazidi kukosa uhalali wa kuendelea kuwepo Mahakamani.Mawakili wa Serekali wamepewa msaada wote ikiwemo kusaidiwa na Majaji Michongo lakini wapi !.
Kesi ipo kwasababu inatafutwa njia nyingine ya kujisafisha ikiwemo kutumia watu wapuuzi kama Zitto wamuadae Mwenyekiti aingie mkenge kama Ndugai mambo yaishe.Ni suala la muda tu Mwamba atakuwa huru huku jina lake likizidi kutakaswa na heshima yake ikizidi kupaa.
Kuna uhakika gani kuwa kesi hiyo inabaraka za moja kwa moja kutoka kwa mchengerwa na si wizara nyingine kama za mambo ya ndani na ulinzi na usalamaKesi ya Ugaidi imeichafua sana Serekali ya awamu ya 6 kama Dogo hakuwa na mizizi mirefu au ingekuwa enzi ya yule Mzee wa Chato hakika tungeshamsahau.Waziri mtoa macho hana mizizi halafu si mwenzetu huyu ndio maana kaondolewa mwenye makosa makubwa kahamishwa wizara angeondolewa angeweza kutoa talaka.
Unafikiri wale mabalozi wanaoonekana kila mara kesi inapotajwa wanamfurahisha Bi Mkubwa ?.
Kuna uhakika gani kuwa kesi hiyo inabaraka za moja kwa moja kutoka kwa mchengerwa na si wizara nyingine kama za mambo ya ndani na ulinzi na usalama
Mchengerwa ndie anae mtesa Mbowe. Kesi inayo mchafua Mama KimataifaWizara ambayo ukiiangalia chini ya utendaji madhubuti wa mchengerwa , kero mbalimbali zilikuwa zinapatiwa ufumbuzi bila kuonea wala kukandamiza upande mmoja.
Alishaanza kutengeneza mifumo ambayo kwa vizazi vingi mbele vingenyoosha utendaji kazi wa watumishi na maafisa utumishi na mabosi wa maafisa utumishi.
Kifupi kila mtu angefanya kazi kama taratibu za kazi zinavyo taka.
Sio unaamka tu kwakuwa unamamlaka unasitisha likizo, unalimbikiza stahiki za mtumishi, unamcheleweshea haki zake n.k
Hayo yote Mchengerwa naona alikuwa anayanyoosha ipaswavyo.
Pengine siku moja atarejeshwa wizarani kama ilivyotokea kwa waziri wa afya Mwalimu.
kila la kheri
Mchengerwa kwa kweli alikuwa mtu sahihi pale utumishi sijui ni kwa nini Mhe Rais amemhamisha kwenda wizara nyingine.Wizara ambayo ukiiangalia chini ya utendaji madhubuti wa mchengerwa , kero mbalimbali zilikuwa zinapatiwa ufumbuzi bila kuonea wala kukandamiza upande mmoja.
Alishaanza kutengeneza mifumo ambayo kwa vizazi vingi mbele vingenyoosha utendaji kazi wa watumishi na maafisa utumishi na mabosi wa maafisa utumishi.
Kifupi kila mtu angefanya kazi kama taratibu za kazi zinavyo taka.
Sio unaamka tu kwakuwa unamamlaka unasitisha likizo, unalimbikiza stahiki za mtumishi, unamcheleweshea haki zake n.k
Hayo yote Mchengerwa naona alikuwa anayanyoosha ipaswavyo.
Pengine siku moja atarejeshwa wizarani kama ilivyotokea kwa waziri wa afya Mwalimu.
kila la kheri
Chawa tafuta kaziMama chonde chonde, nakuomba tena kwa kusisitiza sana, mrejeshe Mohammed Mchengerwa Wizara ya Utumishi. Huyo bwana hapo alikuwa smart sana na alijitahidi sana kushughulikia na kutolea ufafanuzi kwa ufasaha kabisa masuala ya kiutumishi.
Huyu kipaza sauti uliyemleta utumishi naomba arudi huko kwenye sera na siasa nyingine. Mhagama ni mpiga mayowe tu na hawezi kujenga hoja, atasababisha uchukiwe bure na watumishi.
Mchengerwa ni smart sana ambaye ameanza vizuri, hupaswi kumkatisha tamaa kwa kupeleka huko.
Yule anatakiwa Utumishi au TAMISEMI. Very smart
Mwisho rekebisha jina la Wizara ya Gwajima hasa pale kwenye Wanawake na Jinsia hapajakaa vizuri maana neno jinsia linatisha sana
Kazi iendelee!!