Ningejiajiri kwenye kilimo ningekua mbali sana

Kwa kuwa lengo lako ni kufunguana macho, usinialike kuangalia mafanikio...nialike sasa nione njia ya kuyafikia mafanikio. Ninatamani sana kuona set up yako ya mabanda ya nguruwe nipate inspiration.
Nitakualika mkuu... Litakua shamba darasa
 
Mkuu hongera sana kwa jitihada zako..... ila nakuomba ulijibu swali lake la msingi huyo bwana
Kwani mnatumia hela ngapi kutafuta kazi? Kuanzia nauli za kwenda kwenye interview mpaka kuhonga sometimes? Kuku na mbuzi ni sh ngapi?
 
Wanabodi,

Ni mwaka wangu wa nane sasa kwenye ajira, nikijiangalia sina mafanikio ninayoota kuwa nayo na nahisi itachukua muda kuyafikia. Katika tafakari zangu nikagundua kama ningejiajiri kwenye kilimo biashara hata just 3 years back ningekua mbali sana. Hivi sasa nimeanza mchakato wa kuingia kwenye kilimo biashara na dalili zinaonekana kuwa nzuri. Kila nikiingia humu nakukuta watu tunapambana kutafuta ajira nasikitika sana kwakuwa miaka kumi ya ajira ni sawa na miwili au mitatu ya kilimobiashara. Kama hamniamini fanyeni utafiti mdogo tu hakika mtabadili mawazo.
Kuajiriwa kunapoteza muda sana labda kwa wachache wanapiga mshahara wa m40+ na wale wanaopewa boom la 10,000/- kwa siku huku wakipewa hela na marupurupu mengine hadi hela ya kunyolea, kukata kucha na kupeleka nguo kwa dobi lakini wengine kujiari hususani kwenye kilimo ndo sehem ya kutokea.
Tatizo watu wanachukulia kilimo kuwa ni ukosefu wa elimu na ni kazi ya masikini bila kujua kipato kinachopatikana shambani ukilima kitaalam au ukajali mimea yako ipasavyo.
 
Hicho kilimo ungekifanya kwa mtaji kutoka wapi? Na sasa hivi unalima kwa pesa kutoka wapi?
Hizi fikra za kwamba unahitaji mamilioni kuanza project ndio zinawarudisha nyuma...nimeeleza vizuri kwamba si lazima uanze kama mi ninavyoanza..hela kidogo zinazotumika kutafuta kazi kwenye agribusiness si hella ndogo..nauli zinazotumika kwenda kwenye mainterview na hata kuhonga sometimes ni kitu.. Sikulazimishi uamini ninachoamini lakini take your time kujifunza utaelewa
 
Kuajiriwa kunapoteza muda sana labda kwa wachache wanapiga mshahara wa m40+ na wale wanaopewa boom la 10,000/- kwa siku huku wakipewa hela na marupurupu mengine hadi hela ya kunyolea, kukata kucha na kupeleka nguo kwa dobi lakini wengine kujiari hususani kwenye kilimo ndo sehem ya kutokea.
Tatizo watu wanachukulia kilimo kuwa ni ukosefu wa elimu na ni kazi ya masikini bila kujua kipato kinachopatikana shambani ukilima kitaalam au ukajali mimea yako ipasavyo.
Thiis is high level of understanding mkuu big up...kilimobiashara mtu anazalisha mwaka mzima tena mazao ambayo sokoni hayaharibiki haraka so unaweza hata kuexport.. Kuna miradi ya nyuki ynavuna hata zaidi ya mara tatu kwa mwaka. Tatizo watu wakiskia kilimo wanajua ni kile cha kusubiri mvua za masika
 
Mkuu...nimefanya utafiti ndio maana nimesema miaka mitatu au miwili...tena hata hivyo ni mingi... kiufupi tayari ninashamba la ekari 20 ambalo nimeshajemga mabanda 15 kwa ufugaji wa nguruwe, mabanda ya kuku, mbuzi. Kilimo cha mbogamboga na matunda ambapo nimetuma sample ya udongo kituo cha utafiti ili nijue virutubisho vinavyopungua ambapo mwishoni mwa mwaka huu nitaweka greenhouse. Nimemnunulia fundi vifaa vya mizinga ya nyuki ambapo mpaka sasa tumetengeneza mizinga 23 bado kuipaka rangi na kuipanga kwenye bee house lengo ni kuweka mizinga mia mbili ila awamu hii ya kwanza ni mizinga 100
Haya ndo mambo mkuu. Na hapa ndo umuhim wa kujenga kijijini unapoonekana maadam kuna njia za kulink na main road. Huku unafanya kitu utakacho kilimo, ufugaji kama huo kwa kadri utakavyo. Umeme sola zinapiga kazi, maji unachimba kisima chako; network siku hizi hadi vijijini halotel wameokoa jahazi tunastream tu video huku tukifanya matembezi madogo kwenye mashamba.
Kilimo kina raha yake ndo maana JK hajawaacha ng'ombe wake.
 
Wanabodi,

Ni mwaka wangu wa nane sasa kwenye ajira, nikijiangalia sina mafanikio ninayoota kuwa nayo na nahisi itachukua muda kuyafikia. Katika tafakari zangu nikagundua kama ningejiajiri kwenye kilimo biashara hata just 3 years back ningekua mbali sana. Hivi sasa nimeanza mchakato wa kuingia kwenye kilimo biashara na dalili zinaonekana kuwa nzuri. Kila nikiingia humu nakukuta watu tunapambana kutafuta ajira nasikitika sana kwakuwa miaka kumi ya ajira ni sawa na miwili au mitatu ya kilimobiashara. Kama hamniamini fanyeni utafiti mdogo tu hakika mtabadili mawazo.
Mkuu umedumu sana kwenye ajira .. pole sana.

Ebu fikiria kuhusu hii .. ni ndogo lakini ina faida kubwa kupita kiasi ...
Jaribu kilimo cha Nyanya chungu .. kwanza changamoto zake ni ndogo sana ..
Ukianza kuvuna ,, kwenye matuta 3 unaweza kupata ndoo 3 za nyanya chungu kila siku. Ndoo moja inauzwa Tshs. 12,000/= x 3 x 30 = 1,080,000.00 Kwa mwezi.
Zao hili unavuna kwa mwaka mzima na ni bila kuweka kwenye green house.
 
Mtaji wa kwanza na muhimu ni akili na utayari wa kuamua. Mtaji wa pili ni nguvu yaani afya njema. Hivi vikiunganishwa unapata mtaji wa fedha.
Kilimo kinalipa sana ukitumia hayo mambo mawili.
 
Thiis is high level of understanding mkuu big up...kilimobiashara mtu anazalisha mwaka mzima tena mazao ambayo sokoni hayaharibiki haraka so unaweza hata kuexport.. Kuna miradi ya nyuki ynavuna hata zaidi ya mara tatu kwa mwaka. Tatizo watu wakiskia kilimo wanajua ni kile cha kusubiri mvua za masika
Ni kweli kabisa mkuu. Kwenye nyuki nimeiona hiyo nilikuwa Shinyanga kwa wazungu fukani hivi wa shirika nimekuta wamefuga nyuki wa kutosha sehem ambayo sikutarajia nikawa nafikiria sana juu ya ufugaji wake na ninadhani nitaifanyia kazi ili niweke mizinga katika himaya yangu na nipate asali safi na pia niuze niachane na kununua asali kwa bei ghali kila nipitapoa Dodoma-Singida.
Kilimo ni kila kitu, ukachanganya na biashara ya mazao unaishi kama mfalme hakuna shida, hakuna njaa kwako. Matunda, maziwa yanakuwepo tena mtu anachukua toka shambani anakula.
 
Ni kweli kabisa mkuu. Kwenye nyuki nimeiona hiyo nilikuwa Shinyanga kwa wazungu fukani hivi wa shirika nimekuta wamefuga nyuki wa kutosha sehem ambayo sikutarajia nikawa nafikiria sana juu ya ufugaji wake na ninadhani nitaifanyia kazi ili niweke mizinga katika himaya yangu na nipate asali safi na pia niuze niachane na kununua asali kwa bei ghali kila nipitapoa Dodoma-Singida.
Kilimo ni kila kitu, ukachanganya na biashara ya mazao unaishi kama mfalme hakuna shida, hakuna njaa kwako. Matunda, maziwa yanakuwepo tena mtu anachukua toka shambani anakula.
Yap Mkuu wewe ni kama vile tayari umejua nilichopanga... nitajenga ghala kubwa la mazao badae kwa hiyo mazao kama mahindi na mpunga nanunua tu kwa wakulima yanakaa humo. Na hili nililiandika kwenye diary yangu mwanzoni mwa mwaka huu kama moja ya malengo ya baadae. Mi ntakua nalima mazao mengine tu kipindi chote cha mwaka mzima
 
Mkuu umedumu sana kwenye ajira .. pole sana.

Ebu fikiria kuhusu hii .. ni ndogo lakini ina faida kubwa kupita kiasi ...
Jaribu kilimo cha Nyanya chungu .. kwanza changamoto zake ni ndogo sana ..
Ukianza kuvuna ,, kwenye matuta 3 unaweza kupata ndoo 3 za nyanya chungu kila siku. Ndoo moja inauzwa Tshs. 12,000/= x 3 x 30 = 1,080,000.00 Kwa mwezi.
Zao hili unavuna kwa mwaka mzima na ni bila kuweka kwenye green house.
Asante mkuu kwa wazo zuri kama hili sikua nalo kuhusu nyanya chungu...ngoja nifanye utafiti wa mbegu bora
 
Mkuu nimegundua wewe pia ni miongoni mwa watu ambao wanaweza kushindwa hata kabla ya kuanza...kwa sababu wengi wanoshindwa ni kwa sababu hawafanyi utafiti wala projections ya mafanikio ya mbeleni ambayo hata nusu yake tu ukiyafikia wewe umefanikiwa... nilichohubiri mimi sio mafanikio ya uwekezaji bali ya ku-connect dots forward not backward. Na hili huhitaji akili ya ziada kuifanya..sikurupuki...miezi 6 ijayo ntakukaribisha uje ujionee kwa macho mkuu.. lengo ni kufunguana
Inna-allahu-maswaabrina!

Je subira yangu haitatimu?
 
Haya mambo ya kuajiriwa na kujiajiri ni changamoto sana wakuu. Nionavyo mimi wengi tunakosea sana kudhani kwamba ukiingia kwenye kilimo au biashara ndo ghafla bin vuu utafanikiwa. Kiuhalisia ni mchakato unaohitaji subira ili kufikia malengo. Kwamfano mtu anaeanza biashara leo from the scratch itabidi ajipe mwaka mzima au na zaidi ili kwanza kuweza kuaminika na jamii hasa bankers na wadau wengine wa biashara yake. Na katika huo muda ndo muda wa kupigika na kuonyesha uaminifu wa hali ya juu. Sasa kosa ni pale kijana anatoka na ndoto zake za chuo au huko kwenye alipokuwa ameajiriwa anataka ghafla atoboe. Jamani uvumilivu na uaminifu ndo mtaji wa kwanza.
 
Mkuu...nimefanya utafiti ndio maana nimesema miaka mitatu au miwili...tena hata hivyo ni mingi... kiufupi tayari ninashamba la ekari 20 ambalo nimeshajemga mabanda 15 kwa ufugaji wa nguruwe, mabanda ya kuku, mbuzi. Kilimo cha mbogamboga na matunda ambapo nimetuma sample ya udongo kituo cha utafiti ili nijue virutubisho vinavyopungua ambapo mwishoni mwa mwaka huu nitaweka greenhouse. Nimemnunulia fundi vifaa vya mizinga ya nyuki ambapo mpaka sasa tumetengeneza mizinga 23 bado kuipaka rangi na kuipanga kwenye bee house lengo ni kuweka mizinga mia mbili ila awamu hii ya kwanza ni mizinga 100
Mkuu, unaposema kupanga mizinga kny bee house ina maana kunakuwa na nyumba ya kupanga hiyo mizinga? Nilidhani inatundikwa tu juu ya miti msituni..
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom