Hivi punde
JF-Expert Member
- Apr 1, 2017
- 2,554
- 8,552
Somo tajwa hapo juu lahusika. Twende kazi
1. Kwenda na kuni, maji, miti kwa ajili ya kufungia miti ya mizabibu
2. Kwenda shule na kinyesi cha ng'ombe kwa ajili ya kutandaza chini ili kupiga mtama
3. Kulima mashamba ya walimu na kupukuchua mahindi yao
4. Kwenda na majivu shuleni kwa ajili ya kupendezesha mawe na madhari ya shule
5. Michezo ya UMITASHUMTA
6. Kuweka kambi shule zaidi ya moja inapokaribia kufanya mtihani wa darasa la 7
7. Kukaguliwa meno, kucha, nyayo na kwenye pindo za kaptula na shati tukiwa paredi
8. Kukimbia mchaka mchaka chinja
9. Kupiga pushapu
10. Kulima mashamba ya shule
11. Kuiba zabibu za shule
12. Niliwahi mgomea Mwalimu wangu asinichape fimbo, akanitimua mbiyo
13. Kuchelewa shule na kujificha kichakani au HADO
14. Kunywa uji usio kuwa na sukari
15. Kuweka madaftari mfuko wa nyuma
16. Kujaladia madaftari
17. Daftari la mwandiko mistari midogo na mikubwa
18. Niliwahi kuwa kiranja mkuu nikawa sichapwi mboko
19. Somo la uraia, historia, jogi, sayansi kimu. Vita vya maji maji
20. Hesabu za mafumbo
21. Mr na Mrs Daud, Neema na Baraka
22. Kufagia chini barabarani kwa kutumia ufagio wa majani
23. Nilikuwa natumia cha-cha-cha na raba aina ya DHU yaani Dingi Hana Uwezo
24. Nilikuwa napendelea kuvaa "cost" yaani chupi yenye rangi nyingiiii na ki-uzi katikati. Ambayo iliwahi kuchanika na kupanda kifuani wakati nacheza mpira
25. Nilikuwa napenda kukaa nyuma, monita wa darasa akawa ananoandika sana mpiga kelele
26. "Naam Mwalimu...Jana na leo"
Mungu acha aitwe Mungu.
Wewe je mwenzangu unakumbuka nn shule ya msingi?
Karibuni
1. Kwenda na kuni, maji, miti kwa ajili ya kufungia miti ya mizabibu
2. Kwenda shule na kinyesi cha ng'ombe kwa ajili ya kutandaza chini ili kupiga mtama
3. Kulima mashamba ya walimu na kupukuchua mahindi yao
4. Kwenda na majivu shuleni kwa ajili ya kupendezesha mawe na madhari ya shule
5. Michezo ya UMITASHUMTA
6. Kuweka kambi shule zaidi ya moja inapokaribia kufanya mtihani wa darasa la 7
7. Kukaguliwa meno, kucha, nyayo na kwenye pindo za kaptula na shati tukiwa paredi
8. Kukimbia mchaka mchaka chinja
9. Kupiga pushapu
10. Kulima mashamba ya shule
11. Kuiba zabibu za shule
12. Niliwahi mgomea Mwalimu wangu asinichape fimbo, akanitimua mbiyo
13. Kuchelewa shule na kujificha kichakani au HADO
14. Kunywa uji usio kuwa na sukari
15. Kuweka madaftari mfuko wa nyuma
16. Kujaladia madaftari
17. Daftari la mwandiko mistari midogo na mikubwa
18. Niliwahi kuwa kiranja mkuu nikawa sichapwi mboko
19. Somo la uraia, historia, jogi, sayansi kimu. Vita vya maji maji
20. Hesabu za mafumbo
21. Mr na Mrs Daud, Neema na Baraka
22. Kufagia chini barabarani kwa kutumia ufagio wa majani
23. Nilikuwa natumia cha-cha-cha na raba aina ya DHU yaani Dingi Hana Uwezo
24. Nilikuwa napendelea kuvaa "cost" yaani chupi yenye rangi nyingiiii na ki-uzi katikati. Ambayo iliwahi kuchanika na kupanda kifuani wakati nacheza mpira
25. Nilikuwa napenda kukaa nyuma, monita wa darasa akawa ananoandika sana mpiga kelele
26. "Naam Mwalimu...Jana na leo"
Mungu acha aitwe Mungu.
Wewe je mwenzangu unakumbuka nn shule ya msingi?
Karibuni