Ninawashangaa sana wana CCM wanaoshangilia ujio wa wahamiaji ndani ya chama chao!

Mchezaji skihamia timu hahami na mashabiki wake!!

Umesahau usajili wa Lowasa cdm je hakuhama na mashabiki wake? Mpira wa miguu usiulinganishe na siasa. Siasa mtu akiwa mbovu watu wanamtafuta aliko kiongizi wanaeamini atawavusha na kuwafikisha wanakokutaka.

Sent using Jamii Forums mobile app

Lowassa alihama na Nani, kama ni watu akiwakuta cdm. Yeye aliahidi kwenda cdm na wabunge zaidi ya mia wa ccm, je alienda nao? Haya huyo Lowassa karudi sasa hivi ccm, pita kwenye vituo vya kujiandikisha kupiga kura hapa mjini, uone kama kuna idadi ya kuridhisha ya wanaojiandikisha.
 
Ccm lazima washangirie kurudi sarama kwa vijana wao ambao walitumwa kufanya kazi maarum ndani ya chama cha chadema kiasi cha kufikia kupewa mpaka uongozi na kurudi sarama.

Hivyo unaeshangaa kurudi kwa vijana wao wapendwa unaonekana umekariri siasa za majukwaani na kuandamana pamoja nakutengeneza migomo ya wanafunzi na wafanyakazi wa sekta muhim km Elim ,afya nk.

Siasa ni taaruma, tofauti na hapo uwe mwanasiasa wa kutengeneza pesa tu nasio kuchukua dora
Maana siasa nayo ukiipatia nibiashara nzuri sana.
Kwahiyo hao vijana wameshafanya kazi yao wamerudi kwa bosi wao ccm wapangiwe majukum mengine.
 
Hii picha ina maelelzo mengi!
IMG-20150727-WA0013-729322.jpg
Sana ,hapa ni kama wanampokea Rais ...Hili Jamaa lilikuwa na guvu za ajabu sana! 😆 😆 😆 Hebu ona bashasha ya Dk Slaa! Siku hiyo jioni ndipo Josephine alipomchenjia na kubadilisha gia angani!
 
Ccm lazima washangirie kurudi sarama kwa vijana wao ambao walitumwa kufanya kazi maarum ndani ya chama cha chadema kiasi cha kufikia kupewa mpaka uongozi na kurudi sarama.

Hivyo unaeshangaa kurudi kwa vijana wao wapendwa unaonekana umekariri siasa za majukwaani na kuandamana pamoja nakutengeneza migomo ya wanafunzi na wafanyakazi wa sekta muhim km Elim ,afya nk.

Siasa ni taaruma, tofauti na hapo uwe mwanasiasa wa kutengeneza pesa tu nasio kuchukua dora
Maana siasa nayo ukiipatia nibiashara nzuri sana.
Kwahiyo hao vijana wameshafanya kazi yao wamerudi kwa bosi wao ccm wapangiwe majukum mengine.
Att;Faiza ona CCM damu huyu .....shangirie,sarama,maarum,taaruma,dora, Hii si bahati mbaya aisee!
 
Huoni kama josephine alikuwa na hakiri kuliko mbowe na kamati yake.

Huoni kama josephine alimsaidia Dr w.slaa kumchenjia ndo maana sasa anakula kwa raha zake.

Hii inaonekana josephine na Dr slaa ndo walikuwa nahakiri nyingi ndani ya chadema kuliko mbowe na kamati yake?
Viva josephene
Viva Dr slaa kwa kukubari ushauri wa mkeo.
 
Kwa wangeni wa siasa Tanzania huenda wanashangaa sana hii hama hama na watu kupewa vyeo ndani ya CCM au Serikali inayotekeleza ILANI ya CCM
Kuna mwanasheria nguli Dr. Masumbuko Lamwai, alikuwa wakili kichwa kwelikweli na amsha amsha ya NCCR Mageuzi wakati huo. Alirejea CCM na Rais Mkapa akampa ubunge wa kuteuliwa .

Akawepo Mbunge wa kwanza Chadema Dr. Walid Aman Kabour. Huyu alitikisa mwaka 1994 akiwa mbunge wa Kwanza kutoka chama cha upinzani. Baadae akawa katibu Mkuu CDM, then Makam Mkiti CDM.
Wakati Makamba, Yusuf akiwa katibu Mkuu CCM, Dr. Kabour alikwenda CCM na akapewa nafasi ya kugombea ubunge Afrika Mashariki na akashinda.

Makongoro Nyerere alikuwa Mbunge wa NCCR Mageuzi jimbo la Arusha. badae alirejea CCM, akawa mkiti Mkoa wa Mara CCM, akawa mbunge Afrika Mashariki.

Kuna Dani Makanga alikuwa mbunge UDP. Mara akarejea CCM ana CCM kumpa nafasi ya kugombe ubunge jimbo hilohilo la Bariadi Magharibi. Baada ya kushindwa, JK akampa u-DC.

Mkishangaa, Patrobas, Mashinji, akina Watara, akina Mwambe, sie tuliokuwepo wakati Dr. Kaborou anaishinda CCM pale Kigoma mjini, na baadae kuunga mkoni juhudi, ni either tuna waandishi ambao hawajui kuchambua historia au sisi wasomaji tunasoma from surface na hatutaki ku-dig deep in kuwa na depth kwenye masuala yaliyopita ili tukiona ya sasa tusibung'ae
 
Kiujumla Chadema ndo ishapotea hivyo! Mimi si mwana ccm , tafuta popote ! Hata ccm tumewasema walipokosea, mfano juzi hapa tumemsema ndg Gambo bila kukupepesa macho.

Ninachowashauri chadema muwe mnasoma ukosoaji wetu, sikweli kwamba hatuipendi chadema. Hapana tunaipenda sana pamoja na vyama vingine.

Maana bila vyama vya siasa serikari haiwezi fanya kazi kwa weredi.
Ila chadema mlibugi mapema sana! Mlisajiri mamruki mkawapa na vyeo.
Hata nyie mlikuwa na mamruki ndani ya serikari ya ccm kabla ccm haijashtuka na kuanza kuwaondoa kwenye serikari, nahicho ndo kinachowatesa sasa chadema.
 
Niwaombe wanasiasa wote wa vyama vya siasa km mmeamua kufanya siasa za kweli kama za Marekani, wingereza, ujerumani nk.
Fuateni yafuatayo.

Kwanza mtangulize masrahi ya vyama mbele kabla ya masrahi yenu.

Pili..tengenezeni vijana wenu kwa kuwapereka kusoma siasa kwa nchi rafiki na vyama vinavyowaunga mkono

Tatu...mkubari kukosolewa na kuheshim mamraka.

Nne... acheni siasa za chuki kwa nchi maana siwananchi wte ni wanasiasa. Mfano siasa km za zitto, lisu, leema nawengine km hao hizo cyo siasa.
Siasa nikuibua mambo ambayo wananchi hatuyajui, kupigania nasrahi ya wananchi
Cyo kuzuia misaada harafu unajisifu wakati wewe na wanao mnakula kodi zetu , watoto wanasoma shule nzuri kuliko zetu, wake zenu hawaujui umande, mnabima mpaka za vyombo vya ndani, wengine hta NHIF hatuijui harafu pimbi mmoja anajisifu kuzuia nikopo akitaka watoto wetu wazarishwe huku wakisoma... kuda da deki.
Tofauti nahayo namengine mengi mazuri ambayo cjayataja hapa basi fanyeni siasa km za mbowe , siasa za kupiga pes. Hapo sawa
 
Mtoa mada una hoja ya msingi, wafia chama ni watu wa kuwahurumia wanafanya kazi kubwa mno lakini wahamiaji wakija mara Mkuu wa Mkoa, Wilaya, Uwaziri, Naibu waziri, Balozi nk

Wafia chama kweli mnavyofanyiwa si haki.
 
Mtoa mada una hoja ya msingi, wafia chama ni watu wa kuwahurumia wanafanya kazi kubwa mno lakini wahamiaji wakija mara Mkuu wa Mkoa, Wilaya, Uwaziri, Naibu waziri, Balozi nk

Wafia chama kweli mnavyofanyiwa si haki.
Hao niwahamiji kwako wewe kipofu wa siasa! Walikuwa wakwetu, wakaja kwenu kuwaperereza mkawapokea
Wakakiperereza chama wakaleta taarifa tena wakiwa sarama.
Sasa lazima wapumzishwe kwa kupewa uteuzi. Harafu watumwe wengine kuja kuiperereza chadema.
Jifunzeni.
 
Hao niwahamiji kwako wewe kipofu wa siasa! Walikuwa wakwetu, wakaja kwenu kuwaperereza mkawapokea
Wakakiperereza chama wakaleta taarifa tena wakiwa sarama.
Sasa lazima wapumzishwe kwa kupewa uteuzi. Harafu watumwe wengine kuja kuiperereza chadema.
Jifunzeni.
kuperereza = kupeleleza
 
Hiyo ndio sera yao kuu, "The Cardinal Policy", kuhakikisha kuwa upinzani wa vyama unatoweka.

Hilo la maendeleo ni "Public Relations Affair" tu. Utapiganiaje maendeleo wakati kila siku umasikini unaongezeka na miradi unayoanzisha haina impact yoyote kwa maendeleo ya watu. This is very silly and awkward.
 
Back
Top Bottom