Ninauza shamba lenye ukubwa wa ekari moja

M-pesa

JF-Expert Member
Sep 4, 2011
602
151
Ninauza shamba lenye ukubwa wa ekari moja, lipo umbali wa kilometa 25 kutoka ferry. Eneo linaitwa mbutu Mkwajuni.
Bei Tshs. 4000,000 ( Milioni nne). Mmiliki ni mimi mwenyewe, ni pm tufanye biashara.

Nimeattach Pdf document ya Kigamboni new city ili ujuwe ni eneo gani litakaloathiriwa na mradi. Pia mnunuzi yuko huru kwenda kufanya search ya eneo Manispaa ya Temeke na wizarani ili kujiridhisha kabla ya kununua.

View attachment Kigamboni New City B.pdf

Kwa Maelezo ya Ziada Kuhusu Kigamboni Tafadhali Tembelea website ifuatayo kujiridhisha kabla ya kufanya maamuzi:
http://www.ardhi.go.tz/kigamboni-new-city.html
 
Eka moja ni shamba au plot ya kujenga nyumba ndogo ya kuishi?
 
Mbutu ni miongoni mwa maeneo ambayo yatachukuliwa na serikali kwa ajili ya kigamboni city project. Kabla hujanunua jihakikishie kuwa eneo hilo hutanyang'anywa.
 
Hilo liko wazi ambae anahitaji eneo yuko huru kwenda manispaa ya Temeke au Wizarani kuangalia usalama kabla hajanunua. Kuna ambae ananunua eneo bila kwenda manispaa kucheck?
Lakini kwenye Red Umedanganya nitatoa website ya wizara muaangalie maeneo yanayoathiriwa na mradi wa kigamboni.
Mbutu ni miongoni mwa maeneo ambayo yatachukuliwa na serikali kwa ajili ya kigamboni city project. Kabla hujanunua jihakikishie kuwa eneo hilo hutanyang'anywa.
 
Huyu muuzaji anayejiita M-pesa hayuko ethical. Kama kuna mtu anataka eneo ni bora akatafute kwa mtu mwingine. Hapa ananiandikia PM kibao za vitisho ili nisiseme ninayoyajua kuhusu mbutu. Alianzisha thread leo kaifuta baada ya kuona watu watajua ukweli. Sishauri kufanya biashara ya kiwanja hicho na M-pesa.
 
Ndugu yangu nani anakutisha? Hivi ulimwengu huu nani ananunua kiwanja bila kufanya search? Mnunuzi yupo huru kwenda Manispaa ya Temeke hadi wizara ya ardhi ili kujiridhisha kabla ya kununua. Nina hakika asilimia mia moja unakurupuka kwa posts zako.
Wewe ni Great thinker kweli? Thread ipi nimeifuta ndugu? Unaweza kuthibitisha?
Mimi nafanya biashara kwa akili, na ndio maana utaona nimeweka thread tofautitofauti zenye content moja katika majukwaa yafuatayo: Biashara, Matangazo madogomadogo na Habari Mchanganyiko.
Huyu muuzaji anayejiita M-pesa hayuko ethical. Kama kuna mtu anataka eneo ni bora akatafute kwa mtu mwingine. Hapa ananiandikia PM kibao za vitisho ili nisiseme ninayoyajua kuhusu mbutu. Alianzisha thread leo kaifuta baada ya kuona watu watajua ukweli. Sishauri kufanya biashara ya kiwanja hicho na M-pesa.
 
Huyu muuzaji anayejiita M-pesa hayuko ethical. Kama kuna mtu anataka eneo ni bora akatafute kwa mtu mwingine. Hapa ananiandikia PM kibao za vitisho ili nisiseme ninayoyajua kuhusu mbutu. Alianzisha thread leo kaifuta baada ya kuona watu watajua ukweli. Sishauri kufanya biashara ya kiwanja hicho na M-pesa.

Mkuu asante sana kwa kututonya. Nashangaa hata mimi nilimuuliza kuhusu documents na kama kiwanja/ shamba limepimwa. Hakujibu na wala maulizo yangu siyaoni, kumbe alifuta!
 
Huna haja ya kuniandikia PM kuhusu thread ambayo iko public. Hiyo ni dalili ya kukosa uaminifu na nitashangaa kuona mtu anainvest sh. Milioni nne katika biashara na wewe. Ninachokifanya ni kuhakikisha kuwa JF haitumiwi kwa utapeli. Kama unauza kitu weka thread na acha members watoe maoni yao, hupaswi kukataza members kusema wanayoyafahamu kuhusu product unayouza. Unaweza kutoa sababu ziliyokufanya ufute ili thread uliyoleta awali kuhusu hilo "shamba"?
 
Hulazimishwi kununua, sipo desperate kwenye kuuza ardhi yangu. Najua nafanya biashara ambayo ni genuine! By the way ninatoa ekari moja kati ya tatu nilizonazo. Kwa hivyo ambaye atanunua, nitakuwa naye jirani! Hofu yako ndo umaskini wako!!!!
Mkuu asante sana kwa kututonya. Nashangaa hata mimi nilimuuliza kuhusu documents na kama kiwanja/ shamba limepimwa. Hakujibu na wala maulizo yangu siyaoni, kumbe alifuta!
 
Huyu muuzaji anayejiita M-pesa hayuko ethical. Kama kuna mtu anataka eneo ni bora akatafute kwa mtu mwingine. Hapa ananiandikia PM kibao za vitisho ili nisiseme ninayoyajua kuhusu mbutu. Alianzisha thread leo kaifuta baada ya kuona watu watajua ukweli. Sishauri kufanya biashara ya kiwanja hicho na M-pesa.

Ndugu yangu nani anakutisha? Hivi ulimwengu huu nani ananunua kiwanja bila kufanya search? Mnunuzi yupo huru kwenda Manispaa ya Temeke hadi wizara ya ardhi ili kujiridhisha kabla ya kununua. Nina hakika asilimia mia moja unakurupuka kwa posts zako.
Wewe ni Great thinker kweli? Thread ipi nimeifuta ndugu? Unaweza kuthibitisha?
Mimi nafanya biashara kwa akili, na ndio maana utaona nimeweka thread tofautitofauti zenye content moja katika majukwaa yafuatayo: Biashara, Matangazo madogomadogo na Habari Mchanganyiko.

Mtakuwa mnajuana...
 
Unajua sorry to say, but real I doubt kuhusu uwezo wako wa kufikiri! Hivi moderators wakiulizwa kuthibitisha kama kuna thread yeyote nimeifuta alafu wakisema si kweli utajisikiaje? Nahakika hakuna thread hata moja iliyofutwa, Invisible anaweza kuthibitisha hilo.
Huna haja ya kuniandikia PM kuhusu thread ambayo iko public. Hiyo ni dalili ya kukosa uaminifu na nitashangaa kuona mtu anainvest sh. Milioni nne katika biashara na wewe. Ninachokifanya ni kuhakikisha kuwa JF haitumiwi kwa utapeli. Kama unauza kitu weka thread na acha members watoe maoni yao, hupaswi kukataza members kusema wanayoyafahamu kuhusu product unayouza. Unaweza kutoa sababu ziliyokufanya ufute ili thread uliyoleta awali kuhusu hilo "shamba"?
 
Katavi umenichekesha kuliko siku zote... Hahahahahahahahahaha.... Mtu anaweza kudhani tunajuana, ila I have no idea who this dude is! Nimeshangaa jamaa yuko aggressive utadhani katongozewa mke. Mimi nina ardhi huko na nimeacha kuidevelop kwa sababu tushapewa taarifa na hata TBC walionyesha kikao chetu na mkuu wa wilaya ya Temeke kuhusu kunyan'ganywa maeneo yetu, tunajaribu kuresist lakini najua mpaka mwisho hatutafanikiwa kwa sababu tuko devided sana. Sasa jamaa anataka kujifanya gwiji la matapeli, ila kinachoniudhi zaidi ni kwamba anamiss use Jamiiforums.
 
Mkuu nikikuambia hata simfahamu...huwezi kuamini, yaani the guy is coming from nowhere na kuanza kunishushia tuhuma nzito nzito. Hivi Tanzania ya leo mtu anaweza kununua ardhi bila kufanya search kwanza?
Mtakuwa mnajuana...
 
Uko huru kuongea lolote bwana! Lakini Muongo hawezi kudanganya siku zote! Mara ulitaka kununua, Saivi umesahau unaanza kudai una ardhi huko. Kwali uwezo wako wa kufikiri ni mdogo. Nikishauza ardhi nitakuja nikupe report, Lengo lako wewe si ni ku- tarnish image yangu?
Katavi umenichekesha kuliko siku zote... Hahahahahahahahahaha.... Mtu anaweza kudhani tunajuana, ila I have no idea who this dude is! Nimeshangaa jamaa yuko aggressive utadhani katongozewa mke. Mimi nina ardhi huko na nimeacha kuidevelop kwa sababu tushapewa taarifa na hata TBC walionyesha kikao chetu na mkuu wa wilaya ya Temeke kuhusu kunyan'ganywa maeneo yetu, tunajaribu kuresist lakini najua mpaka mwisho hatutafanikiwa kwa sababu tuko devided sana. Sasa jamaa anataka kujifanya gwiji la matapeli, ila kinachoniudhi zaidi ni kwamba anamiss use Jamiiforums.
 
Ndugu M-Pesa kizui chajiuza na kibaya chajitembeza!

Kwa jinsi ulivyoshika bango, wanunuzi watarajiwa tumeshtuka.
 
M-pesa, najua utauza tu hiyo ardhi kwa sababu matapeli mna njia mbalimbali za kurubuni watu. Mfano mdogo ni jinsi tu ulivyoanzisha thread nyingine chapchap na kuleta mikwara koko kwa kupitia PM. Ninachotaka kuhakikisha ni kwamba hata kama unatapeli lakini sio kwa kutumia JF.
 
Asante kwa ushauri, kama nilivyosema sipo desparate kwenye kuuza. Na mara nyingi waongeaji sana huwa sio wanunuzi.
Ndugu M-Pesa kizui chajiuza na kibaya chajitembeza!

Kwa jinsi ulivyoshika bango, wanunuzi watarajiwa tumeshtuka.
 
Back
Top Bottom