Tunakoelekea siyo kuzuri. Ninasikitishwa sana kupanda kwa kasi ya ajabu bei ya vifaa vya ujenzi. Pamoja na kupanda kwa mafuta haiwezekani bei ya vifaa kupanda kwa kasi vile. Nitoe tu mifano michache.
(1) Sheet moja ya alluminium ilikuwa inauzwa hapa Mwanza kwa Tshs.160,000 jana nimeambiwa sasa ni Tshs. 280,000. (2) Sementi mfuko moja ilikuwa inauzwa Tshs.19,500 sasa sementi mfuko huo moja unauzwa Tshs.22,000.
Mifano ni mingi ukichukulia nondo, mabati, gypsum powder, gypsum boards, rangi aina ya plascon, vitasa, misumari aina zote, mbao n.k vyote hivi bei imepanda kwa kasi sana.
Ni vema Serikali ikaingilia na kuona kuna tatizo gani na kutoa mrejesho kwa wananchi haraka iwezekanavyo.
(1) Sheet moja ya alluminium ilikuwa inauzwa hapa Mwanza kwa Tshs.160,000 jana nimeambiwa sasa ni Tshs. 280,000. (2) Sementi mfuko moja ilikuwa inauzwa Tshs.19,500 sasa sementi mfuko huo moja unauzwa Tshs.22,000.
Mifano ni mingi ukichukulia nondo, mabati, gypsum powder, gypsum boards, rangi aina ya plascon, vitasa, misumari aina zote, mbao n.k vyote hivi bei imepanda kwa kasi sana.
Ni vema Serikali ikaingilia na kuona kuna tatizo gani na kutoa mrejesho kwa wananchi haraka iwezekanavyo.