Ninapenda kulia sana kama njia ya kutuliza machungu, je kuna ubaya?

toplemon

JF-Expert Member
Mar 26, 2017
4,581
4,631
Mimi ni mwanaume ambaye ninavumilia mambo sana na kuyatafutia utatuzi kwa namna yoyote ile.

Ila kuna wakati mambo yananifika na kuniumiza sana hadi najikuta nakata tamaa au jambo baya linanifika au taarifa mbaya hapo unachanganya na shida za dunia.

Huwa najikuta nalia sana na nikiwa mwenyewe nitalia weee hadi nitaona kabisa kwa sasa inatosha na hii imekua siri yangu.

Nikikumbwa na madhila ya dunia nitajikaza na kuonyesha ukakamavu mbele ya hadhira kwamba ninalimudu na nina roho ngumu na watu wanaamini hivyo lakini nikishaondoka hapo nikifika sehemu nipo mwenyewe tu hususan usiku nitalia mno kwa lile jambo.

Kiukweli napenda kulia sana, tena sana tu, lakini nikiwa mwenyewe tu ndani huko hii imekua kama njia yangu ya kupunguza machungu.

Hata nikikaa na rafiki yangu mfano katoka safari kaja tumekaa wote tumeshazoeana kama zamani na kampani nk...aisee siku akiondoka kuna uwezekano mkubwa sana kulia au hata mtu wangu wa karibu niliyemzoea ananipenda na kunithamini siku akiondoka na ukute ndo harudi tena mimi machozi lazima yanitiririke humo nikiwa nimejifungia

Sijui unalizungumziaje kwa upande wako ndugu mwana JF?
 
Lia tu ili uondoe huo uchungu, tena afadhali yako wewe unayedondosha chozi kuliko wale wanaokaa nayo moyoni maana nahisi hao ndiyo huwa wanateseka zaidi..!

Tena bora wewe ukikutana na madhila tu ndiyo walia, Mimi nalia nikikasirika, nalia nikihuzunika na cha kushangaza zaidi hulia pia nikifurahi, rafiki zangu huniitaga 'crying baby'..!
 
Lia tu ili uondoe huo uchungu, tena afadhali yako wewe unayedondosha chozi kuliko wale wanaokaa nayo moyoni maana nahisi hao ndiyo huwa wanateseka zaidi..!

Tena bora wewe ukikutana na madhila tu ndiyo walia, Mimi nalia nikikasirika, nalia nikihuzunika na cha kushangaza zaidi hulia pia nikifurahi, rafiki zangu huniitaga 'crying baby'..!
Kuna vikundi vya kulia misibani, kajiunge navyo mkuu, utapunguza uchungu pia utaongeza kipato.
 
Lia tu ili uondoe huo uchungu, tena afadhali yako wewe unayedondosha chozi kuliko wale wanaokaa nayo moyoni maana nahisi hao ndiyo huwa wanateseka zaidi..!

Tena bora wewe ukikutana na madhila tu ndiyo walia, Mimi nalia nikikasirika, nalia nikihuzunika na cha kushangaza zaidi hulia pia nikifurahi, rafiki zangu huniitaga 'crying baby'..!
Hebu subiri kidogo
 
hakuna tatizo lolote la kulia, kama ukiona ndio njia ya kupunguza mawazo na kusamehe, bora ya hayo kuliko kuamua kulipiza kisasi au kufanya baya zaidi.
 
Kama hulii mbele za watu ni kawaida tu, kheri uonekane imara kuliko dhaifu maana hii dunia watu wakikuona ni dhaifu utapata tabu sana.
 
Kwakweli hayo ni maumbile hata mm huwa nalia sana. Hata nikiangalia baadhi ya move zenye hisia kali huwa machozi yananitoka.

Hata nikiagana na rafiki au mtu niliyemshiba kama kuna kutoa neno Fulani la shukrani huwa siwezi .

Mwaka huu, mwanangu alifukuzwa shule kwa kweli kitendo kile baada ya kumuona mwanangu nilipatwa na uchungu sana kama ningekuwa OSAMA siku nilikuwa nalipua shule.

Nililia sana.
 
Pole Mkuu ila ilo ni tatizo, ushauri

Tafuta psychologist atakusaidia, maana unamsongo wa mawazo kupitiliza, usipofanya hivyo ipo siku utajikuta unajinyonga au kunywa sumu au Kuwa kichaa so Zingatia ushauri huu kwenye hospitali za rufaa wapo

Pole sana mkuu
 
Kwa mujibu wa kichwa cha uzi wako inashauriwa kulia ili kutuliza hasira au kupunguza machungu (sijasoma maelezo)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom