Ninapata maumivu makali ya tumbo eneo la kitovu, Hospitalini tatizo halionekani kabisa

Mr Zed

New Member
Dec 20, 2020
3
1
Habarini wakuu! kabla sijaenda kwenye hoja yangu kama kichwa kinavyojieleza nitoe shukrani zangu za pekee kwa Mwenyezi Mungu anipae uhai, Wakuu ni wiki ya pili sasa tangu nilipoanza kupata tatizo la maumivu ya tumbo eneo lote la kitovu pamoja na pembeni kidogo upande wa kulia wa tumbo usawa na kitovu.

Siku mbili baada ya kuanza tatizo girl friend wangu alinishauri nitumie dawa ya kienyeji ya U.T.I akidhani ndo litakuwa tatizo baada ya yeye kwenda hospital akaambiwa ana hilo tatizo nilitumia hiyo dawa ya kienyeji siku 4 mfululizo 1x3 kila siku lakini hali iliendelea kuwa vilevile, siku ya 6 niliamua kwenda dispensary moja ya chuo kikuu kimoja huku kanda ya ziwa nikapimwa choo pamoja na mkojo lakini niliambiwa sina tatizo lolote ingawa haja kubwa ilikuwa lain sana mithili ya mtu anaeharisha lakini doctor aliniambia ni hali ya kawaida tu na kwamba hakuna tatizo lolote kwa mjibu wa vipimo.

Nilipewa flagly kusaidia, nilitumia kwa muda wa siku tatu bila mafanikio kabisa niliendelea kupata haja kubwa laini sana na maumivu ya tumbo yasiyo na miungurumo siku iliyofuata nilirudi hospital kupima tena, doctor alinipima tena vipimo vilevile lakini hakukuta tatizo alinipa dawa fulani hivi zimeandikwa kwa kifupi diclof kwa ajiri ya kupunguza maumivu lakini sijaona mafanikio toka juzi hadi leo ni siku ya tatu.

Basi leo nimejaribu kumpigia simu doctor fulani ni rafiki yangu akanishauri niende hospitali kubwa kwa ajiri ya vipimo zaidi. Wakuu hali yangu siyo mbaya sana ispokuwa nakosa raha kabisa kwani tumbo linauma mfululizo hadi sek 10 hadi 15 ndipo linaachia nakutulia kabisa kama vile hakuna shida yoyote baada ya muda kidogo tena linabana.

Nimejaribu kufanya jitihada binafsi kama vile kutumia maji ya uvuguvugu, matunda na mboga za majani kwa wingi pamoja na kuhakikisha nakula chakula laini lakini juhudi zangu hazijazaa matunda kabisa.

Naombeni ushauri wakuu pengine shida inaweza ikawa ni nini maana tumbo bado linauma ingawaje si mfululizo sana lakini pia naanza kusikia maumivu kwa mbali kifuani upande wa kulia ahsanteni.
 
Inawezekeana kuwa ni maumivu yanasababishwa na kidole tumbo. Kama rafiki yako alivyokushauri nenda hospitali kubwa kwa vipimo zaidi.
 
Habarini wakuu! kabla sijaenda kwenye hoja yangu kama kichwa kinavyojieleza nitoe shukrani zangu za pekee kwa Mwenyezi Mungu anipae uhai, Wakuu ni wiki ya pili sasa tangu nilipoanza kupata tatizo la maumivu ya tumbo eneo lote la kitovu pamoja na pembeni kidogo upande wa kulia wa tumbo usawa na kitovu...
Kama maradhi hayaonekani na vipimo vya hospitali utakuw aunayo maradhi ya nguvu za giza aka uchawi ulilishwa na upo tumboni mwako nione kwa wakati wako ili nipate kukutibia upate kupona amradhi yako uguw apole.
 
Kama maradhi hayaonekani na vipimo vya hospitali utakuw aunayo maradhi ya nguvu za giza aka uchawi ulilishwa na upo tumboni mwako nione kwa wakati wako ili nipate kukutibia upate kupona amradhi yako uguw apole.
Huyu kapimwa choo tu tena zahanati. Aende hospitali yenye vipimo zaidi.
 
pole ndugu Mr zed
Kwa matatizo ya tumbo ikiwemo kuhara,n.k

Japo sijajua una umri gani,ulianza kusumbuliwa link,aina gani ya vyakula unavyopendelea kula,ni maIngira gani unayoishi
OK nisikuchoshe nenda Duka la dawa unalolijua katafute dawa inayoitwa NOR-T(norfloxacin Tinidazole) 1*2kila baada ya masaa 12. hakikisha unakula ndipo uinywe.

natumaini itakusaidia
 
We jamaa tafuta ciplofloxacin utakuja kunishukuru hiyo hali ilishanitokea baada ya sex, vijana kwa sasa tumezidisha mautundu ya kulamba lamba miili ya dada zetu wakati imejaa mabacteria ,h ilinipata hali hiyo hiyo full choo cha uharo homa, nikapiga ciplo ilipotea mazima, mean nilimeza baadhi ya bacteria wakaenda kuleta shida tumboni, sasa ciplo ndio kiboko yao tena ile ya ciprus
 
Its sound kama Vidonda vya Tumbo na Gesi ndio inasumbua, Lakini kama ni mwanafunzi wa Chuo nafikiria Pia Muscle Spasms. Ushauri wangu Jaribu kupima vidonda vya tumbo na utumie dawa za kupunguza Gesi Tumboni, Tumia muscle relaxant pia.

Usisahau kwenda Hospital kwa vipimo zaidi
 
Habarini wakuu! kabla sijaenda kwenye hoja yangu kama kichwa kinavyojieleza nitoe shukrani zangu za pekee kwa Mwenyezi Mungu anipae uhai, Wakuu ni wiki ya pili sasa tangu nilipoanza kupata tatizo la maumivu ya tumbo eneo lote la kitovu pamoja na pembeni kidogo upande wa kulia wa tumbo usawa na kitovu.

Siku mbili baada ya kuanza tatizo girl friend wangu alinishauri nitumie dawa ya kienyeji ya U.T.I akidhani ndo litakuwa tatizo baada ya yeye kwenda hospital akaambiwa ana hilo tatizo nilitumia hiyo dawa ya kienyeji siku 4 mfululizo 1x3 kila siku lakini hali iliendelea kuwa vilevile, siku ya 6 niliamua kwenda dispensary moja ya chuo kikuu kimoja huku kanda ya ziwa nikapimwa choo pamoja na mkojo lakini niliambiwa sina tatizo lolote ingawa haja kubwa ilikuwa lain sana mithili ya mtu anaeharisha lakini doctor aliniambia ni hali ya kawaida tu na kwamba hakuna tatizo lolote kwa mjibu wa vipimo.

Nilipewa flagly kusaidia, nilitumia kwa muda wa siku tatu bila mafanikio kabisa niliendelea kupata haja kubwa laini sana na maumivu ya tumbo yasiyo na miungurumo siku iliyofuata nilirudi hospital kupima tena, doctor alinipima tena vipimo vilevile lakini hakukuta tatizo alinipa dawa fulani hivi zimeandikwa kwa kifupi diclof kwa ajiri ya kupunguza maumivu lakini sijaona mafanikio toka juzi hadi leo ni siku ya tatu.

Basi leo nimejaribu kumpigia simu doctor fulani ni rafiki yangu akanishauri niende hospitali kubwa kwa ajiri ya vipimo zaidi. Wakuu hali yangu siyo mbaya sana ispokuwa nakosa raha kabisa kwani tumbo linauma mfululizo hadi sek 10 hadi 15 ndipo linaachia nakutulia kabisa kama vile hakuna shida yoyote baada ya muda kidogo tena linabana.

Nimejaribu kufanya jitihada binafsi kama vile kutumia maji ya uvuguvugu, matunda na mboga za majani kwa wingi pamoja na kuhakikisha nakula chakula laini lakini juhudi zangu hazijazaa matunda kabisa.

Naombeni ushauri wakuu pengine shida inaweza ikawa ni nini maana tumbo bado linauma ingawaje si mfululizo sana lakini pia naanza kusikia maumivu kwa mbali kifuani upande wa kulia ahsanteni.
Nenda hospitals kubwa usiende tu dispensary YAWEZA kuwa Appendix na hi huwa HAIONEKANI kwenye vipimo.kipimo Cha kienyeji Kama unayo hiyo Ni kula nyama ya mbuzi au kunywa maziwa ukiharisha au kupata choo laini Sana na TUMBO kukata Kama una TUMBO la kuhara Ni appendix (KIDOLE TUMBO)
 
Back
Top Bottom