Ninakiwanja na leseni ya madini (dhahabu) nipo kilindi nahitaji muwekezaji wadau

MAKOLA

Member
Jun 5, 2010
46
16
wadau nina leseni ya kuchimba madini "mining license" katika kitalu changu cha madini, natafuta muwekezaji ambaye nitaingia nae ubia, na kama ana dau la kutosha mi namwachia kitalu cha madini. Nitsaidieni nipate mwekezaji. Nitashukuru kwa msaada
 
Sasa mkuu hii ndo breaking news?

Maelezo hayajitoshelezi hata kidogo, Mf madini ya aina gani?ukubwa wa kitalu?kiko wapi?. nahdani ungeweka hayo maelezo wenye nia wanaweza shawishika

All the best
 
Predigo son. Kiwanja kipo wilaya kilindi, kina hekta 10 au ekari 25, madini ni ya dhahabu. Then n - handsome. Nipe adress ya kanada ili nitume cv mtu wangu.
 
Predigo son. Kiwanja kipo wilaya kilindi, kina hekta 10 au ekari 25, madini ni ya dhahabu. Then n - handsome. Nipe adress ya kanada ili nitume cv mtu wangu.

Mkuu ulitaka usiliwe chimba mwenyewe ufaidike.Ukiingiza muwekezaji umekwenda na maji.
Swali la kwanza atakuuliza kuna madini kiasi gani chini-Tshs bilioni 1,6 au 30
Pili gharama ambazo wewe umetumia kiasi gani na je una fedha za kuwekeza?(your level of equity in investment)
Tatu Kama jibu la kwanza ni bil 30 na kuendelea na jibu la pili ni milioni mbili au tatu basi inakuwa rahisi kukufidia gharama zako mhata mara tatu ili wakubwa wale.
NB Idara ya madini wakifahamu unatafuta mwekezaji watauza hiyo sehemu wenyewe.
 
Maelezo hayajitoshelezi hata kidogo, Mf madini ya aina gani?ukubwa wa kitalu?kiko wapi?. nahdani ungeweka hayo maelezo wenye nia wanaweza shawishika/QUOTE]

Makola tatizo lako ni zaidi ya kiwanja ndugu yangu. Kwanza nina wasi wasi na unavyoweza ku market! Mwekezaji anahitaji detail nyingi sana kabla hajaamua kuonana na wewe. Sasa unaposema nina kiwanja, hatujui ukubwa wake, madini gani, leseni ya daraja gani, kadirio la madini,leseni inakwisha lini n.k sijui unategemea nini. Kwa ushauri wangu, hapa Tanzania wapo watu wa madini na project management, hawa ni wazuri sana kabla hujaingia mikataba mikubwa au huja market bidhaa au mali yako. Watakusaidia maana ninaona hata akipatikana uwezekanao wa kutapeliwa ni asilimia 1000%
Hii ni sawa na ile ya mheshimiwa kitomari wa JF anatangaza nyumba za kupanga haweki hata picha,! wapo watu wako nje ya nchi mathalani wanataka kukodi nyumba kwa sababu mbali mbali, sasa kama hakuna picha na details utawapata wapi wateja. Jana kuna mtu kanipigia simu toka ireland eti niende nikaangalie apartment zinafanana vipi hiko kimara! kazi hii Kitomari angeshaimaliza kama angeweka picha na kuwa makini.
Please Watanzania, amkeni na mjue mbinu za kuuza na kujiuuza, ikiwa ni pamoja na buisness plan and management. Tusifanye kazi kwa kubabaisha, that time is over, now is competition from north to south, east to west!

Mheshimiwa Makola, hata ungeenda UDSM wapo watu wangekusaidia bure kuliko kukurupuka,'' nina kiwanja na leseni .....'' fanya mambo kisayansi my brother, unaweza uza eneo la bilion 30 kwa milion 3! simply because you don't ask!
 
Back
Top Bottom