Dumelambegu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 1,052
- 257
Jamani sijui nanyi ni wahanga wa wanawake wanaojishaua wanapotembelewa na wageni maofisini mwao. Frankly speaking, wanawake wamezidi wanajishaua mpaka inakuwa kero. Kwa kweli ni ofisi chache sana mijini ambazo wanawake hususani masecretaries na watumishi wengine wa kike wanaopokea wageni kwa nyuso za bashasha. Ajabu ni kwamba mgeni akiwa mwanamke kujishaua ndiyo kunakuwa mara dufu. Hali hii ni tofauti kabisa na wanaume. Hata kama wapo wanaume pia wenye tabia hiyo lakini wanawake ndiyo wengi zaidi. Jamani wanawake acheni tabia hiyo kwani mnaowafanyia hivyo vituko ndiyo wateja wenu wanaowaweka hapo ofisini. Samahani, wanawake ambao hawana tabia hiyo.