SN.BARRY
JF-Expert Member
- Oct 12, 2012
- 4,040
- 8,895
Ushauri mzuri sana huu.Habari, Nimesoma maelezo yako na kuyaelewa ifuatavyo:-
Mosi, Ulifiwa na mke/mpenzi wako akiwa na kichanga tumboni hivyo kwa sasa huna mtoto lakini unahitaji mtoto kwa hali yoyote ukizingatia umri unakwenda na wenzio wenye umri kama wako wana watoto.
Pili, Uwezo wako kiuchumi siyo mbaya (uchumi wa kati) hivyo pesa ya mambo madogo madogo haikupigi chenga ikiwepo na ya kutuma nyumbani ambapo unauguza mama yako.
Tatu, Umepata mpenzi wa kijaluo mwenye mtoto wa umri wa miaka tisa (9) na yeye ana hamu ya kuolewa na kwa kuwa umeonyesha uwezo wa kumlea mwanae anataka umuoe haraka bila kujali unayoyapitia kwa sasa.
Ushauri wangu, Kwanza nakushukuru kwa kukiri kuwa umebugi (umekosea) Sasa unatakiwa kurekebisha makosa kwa kufanya ifuatavyo. Kuoa siyo jambo la kukurupuka, subiri kwanza ajifungue wakati mkiendelea kumuuguza mama yenu mzazi, pili tumia muda mrefu kumchunguza unayetaka kumuoa maana kwa mujibu wa maelezo yako (kama haumsingizii) inaonyesha hajali shida zako.
Wanawake wa Vyuoni (hasa vyuo vikuu) wanapitia mengi na wanajua mengi, sasa huyo wako amegundua una udhaifu hivyo anatumia udhaifu huo kukuendesha anavyotaka yeye. Simama kama Mwanaume unatakiwa kuwa mpangaji na muamuzi wa mwisho yeye abakie kuwa mshauri na asikupangie (au unaogopa digree yake!!).
Kwa maoni ya mmoja wa wadau ni kuwa Mwanamke mwenye mtoto (Single mother) aliyepata mtu wa kumlelea mwanae na kumuahidi ndoa si rahisi kumuacha na ukijaribu unaweza kulishwa hata vyura na mijusi na sisi wote ukatuona mmbwa. Hivyo hata ukitaka kumuacha ujipange usikurupuke anaweza kuuuwa au kukufanya kichaa.
Na ninavyohisi ameshawaambia ndugu zake kuhusu udhaifu wako hivyo nao wanakupelekesha tu. Kuhusu fedha hiyo milioni 5 usimpe maana atatumia itaisha kisha atakuja tena kwa ukali (maana ameshakuona poyoyo). KWA UJUMLA UNATAKIWA KUSIMAMA KIUME TENA KWA KUMAANISHA SIYO KUIGIZA.