Ninaekereka au Kuchoshwa na hili linaloendelea sasa katika Redio nyingi za Tanzania nipo peke yangu au?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,869
Unakuta Kipindi fulani ni cha ama dakika 30 au Saa Moja tu lakini Watangazaji wake wote Watano wanataka Kuonesha Umahiri wao katika Kupiga Stori na hapo hapo tena Matangazo ya Biashara yanafululiza na Content husika iliyokufanya usikilize hicho Kipindi unakuja kuipata ndani ya dakika 5 tu.

Halafu namtafuta sana huyu Mtu aliyebuni kuwa kwa Siku hizi ili Redio yako ipendwe na Vipindi pia vivutie Wasikilizaji basi ni lazima kiwe na Watangazaji kuanzia Watano mpaka hata Saba tena wote wakiwa Hewani Wanabwabwaja tu Pumba zao.

Enyi Wamiliki na Watangazaji wa Redio na Vipindi mbalimbali vya nchini Tanzania Sisi Wasikilizaji wenu tunataka kusikia ' Content ' husika tu na siyo huu ' Upuuzi ' wenu wa kutupigia ' Mikelele ' ya Stori zenu zisizo na Miguu wala Kichwa kwani si tu mnaharibu bali mnatukera mno.

Kuhusu Upigaji wa Matangazo (ambayo najua ndiyo yanawalipeni sana) tafuteni utaratibu wa kuyapiga lakini siyo Kuyafululiza mpaka yanakula muda mrefu wa Kipindi na hatimaye 'Content' husika inakuja kusikika kwa dakika 5 pekee.

Halafu acheni Umbwiga (Ushamba) wenu yaani unakuta Tangazo la Biashara linapochezwa Hewani linajieleza vyema tu mwanzo mwisho kwa Sisi Wasikilizaji na likiisha tu utasikia Watangazaji wote waliojazana Studioni nao wanaanza tena Kulizungumzia. Hivi mliambiwa akina GENTAMYCINE ni Viziwi na hawakulisikia au Kulielewa?

Nina uhakika kuwa kwa Kero hii Kubwa kukifanyika Audience Research ya kuhusu Media za Tanzania na Contents zake ' Findings ' zitaonyesha kuwa Wasikilizaji wengi wamepungua na sasa tumekimbilia huku katika Mitandao ya Kijamii (JamiiForums) ambako binafsi kama GENTAMYCINE naona ' Kumenoga ' kuliko huko kwenye ' Upuuzi ' wenu.

Unaacha Kutangaza ' Content ' ya Kipindi unaanza Kutuambia Mambo yako ya Nyumbani na Mkeo pamoja na Wanao huku ' Ukijisifu ' tu Kipopoma (Kipumbavu) utadhani tumekuuliza.

Na wengine mlivyo Waongo mkiwa ' Vipindini ' huwa ' mnajimwambafai ' kweli kweli kuwa mna Maisha Bora wakati baadhi yenu ( kama si wengi wenu) tunawajua jinsi mlivyo Mafukara kama nilivyo Rais wa Mafukara JamiiForums GENTAMYCINE Mimi.

Ujumbe huu uzifikie 'Redio' zote nchini.
 
Mimi mara chache nawasikiliza, bora siku hizi kuna options kibao mitandaoni. Watu wanapiga stori kama wapo kijiweni then matangazo alafu wakianza kuongea tena wanaanza na matangazo

Pengine waandaaji wa vipindi ndio tatizo au waandaaji wanakosa vipaji vinavyojitosheleza. Hadi vipindi vya burudani unakuta team ya watu watano na madj si chini ya 2! Zamani mtu mmoja au wawili tu walikuwa wanaweza kukimbiza. Hii inampa mtu jukumu kubwa la ubunifu tofauti na sasa na huo mlundikano.
 
Sasa kama kipindi cha michezo kinaanza saa 2 hadi saa 5 au 6 Unadhani wataongea nini zaidi ya porojo tu, lazima waishiwe ya maana na wajikite kwenye porojo.

Labda East Africa Radio. Kuhusu michezo walau kidogo wanajitambua
 
Yani mfano clouds kwenye PB wakiwa wengi kuna noga bana. Yani awe barbra masud na siza yani wote akili nyingi wanaongea kwa nidhamu akija tena samsasali ndio utamu unazindi, unajua ishu sio kuwa na watangazaji wengi kipindi kina masaa 4 wakiwa watu wawili akinogi kitaboa tu yani nachotaka kusema ni watangazaji wawe wawena akili nyingi uwezo mkubwa wakufikiri wasome sanaa local radio adi kero kunaboa atariii.
 
Break fast (Clouds fm). PB nilishaacha kusikiliza. Huwezi elewa kipindi kinahusu nini, mwanzo mwisho wanasifia matangazo tu
Jahazi hapo ni soga mwanzo nwisho huwezi elewa kipindi kinahusu nini
Hawa unawaonea Mkuu ' Uozo ' mkubwa uko Clouds FM, EFM, Magic FM na Wasafi FM.

Kidogo Radio One na RFA kuna Nidhamu na Kujielewa fulani ila siyo kwa hawa niliowataja.
 
Nimehamia TikTok na Mpira. Habari zote nilisha acha siku mingi.Huku kunatosha kabisa.

Mtangazaji anakuja mgeni aliyemzidi kipaji au kipato,badala ya kuhoji kinachomhusu unaona kabisa Mtangazaji anajitutumua kama chura mkavu.

Sasa hapo utangalia lipi.
 
Back
Top Bottom