Nina view 300 tu na nina miezi miwili kwene blogging! NAKOSEA WAPI?

Mr Chromium

JF-Expert Member
Aug 20, 2020
2,088
2,705
IMG_4706.jpg

Mimi ni kijana niaeishi Dar es salaam,Yaah unaweza ukasema n mtu mzima maana niko kwene 80s!!…Nimeajiriwa sehemu kadhaa lakini kwa sasa nimeacha kazi!!

Kwa kifupi sipendi kufanya kazi kwa mtu au institution naona tabu sana habar za kupangiwa,kutumikia mtu, formality,kugombezwa au vile visa vya makazini!!Kifupi napenda kupata shuhuli yangu ambayo inauhuru wa mm ndiye niwe muamuzi!! Kumsujudia boss siwezi yaan hapo tutasumbuana!!

Changamoto ni kua sijui biashara ambayo ndio ingekua inanifit kwa ninachotaka!!
Baada ya kuwaza kwa miezi kadhaa nilikuja na option ya kufanya biashara mtandaoni ambapo ilikua either Youtube au Blog!!
Youtube niliiweka pembeni kwasababu naona kama kuna changamoto fulani hivi kutengeneza video,kuedit,had kua attract viewers!!
Cha pili sielewi youtuber anaeingiza hela nyingi tanzania analipwa sh ngap ili niweze kuona nn anafanya tofauti na pesa inatoka hasa kwene nn viewers wengi au viewers wa wastan targeted,au aina ya topic!!

so nikaingia kwene Blogging!! …Weee!! Lahaulaaaah
Nilichokipata huku n kasheshe maana saa izi niko kwene viewer 300 tu na ni mwezi wa pili!!
Najaribu kushare magrup mengi mengi lakini watanzania kuview vitu serious hawawezi au kunakua na low trafic!!
Plan zangu nilifikiri nipige had miezi mitatu nianze kumonetise lakini naona hali si hali!!

Nimejalibu kufuatilia bloggers wengi wanaotengeneza hela n wale watu /kampunibza habar kama jf,habarleo,nk ambao kifupi wamewekeza hela nyingi

Je kuacha kazi na kujiajiri kama blogger au katka blogging kunaweza kukusaidia kukidhi kipato au ni bora nitafute kazi!!?
Kama kuna mifano halisi mnishauri niifuate nisije potea hasa ukizingatia kunakutumia resources kama muda,fedha na bundle
 
Kama target yako ni watanzani pekee, inabidi contents zako ziwe za kijinga jinga kama umbea, comedy hapo utawakamata chap....! Ila kama ni content za madini target worldwide tumia lugha ya malaika hapo utakua fastaa.! La sivyo hiyo kazi itakushinda....! Ila mkuu hujasema content yako ni ipi inawezekana youtube ungefanya poa zaidi...! Weka wazi content yako tukushauri
 
Umekosea kuacha kazi kisaTU shutuma,majungu kiukweli Kuna mambo hayakwepeki mfano kusemwa au kupewa kashfa..kikubwa we maisha yanaendelea...kwa hiyo ilifaa ufanye zote mbili...binafsi me napofanyia kazi Sina majukumu mengi Sana na komputa ipo nzuri Sana ila mambo ya blogging nayatamani nifanye ila sielewi nahisi mpk nikae na mtu anayejua anifundishe
 
Mimi sina uzoefu sana na haya mambo lakini jana kuna sehem nilisoma (i think Quora), kuna mtu aliandika kuhusu yputube shorts. Akasema hizo ni rahisi zaidi kutengeneza maana zinahitaji applications kama mbili tu pamoja na internet connection kutengeneza na traffic yake ni kubwa due to the fact kwamba watu wengi wako radhi kuangalia shorts ya sekunde 30 hadi dk 1 kuliko kuangalia video ya dk 7 or 15 na kuendelea. Kwangu mimi i think its cheap na iko na rewards nyingi other than youtube videos.
All in all kila la kheri mkuu.
 
Kama target yako ni watanzani pekee, inabidi contents zako ziwe za kijinga jinga kama umbea, comedy hapo utawakamata chap....! Ila kama ni content za madini target worldwide tumia lugha ya malaika hapo utakua fastaa.! La sivyo hiyo kazi itakushinda....! Ila mkuu hujasema content yako ni ipi inawezekana youtube ungefanya poa zaidi...! Weka wazi content yako tukushauri

matangazo ya kazi
 
Umekosea kuacha kazi kisaTU shutuma,majungu kiukweli Kuna mambo hayakwepeki mfano kusemwa au kupewa kashfa..kikubwa we maisha yanaendelea...kwa hiyo ilifaa ufanye zote mbili...binafsi me napofanyia kazi Sina majukumu mengi Sana na komputa ipo nzuri Sana ila mambo ya blogging nayatamani nifanye ila sielewi nahisi mpk nikae na mtu anayejua anifundishe

so unanishauri nirudi job
 
Blog vijana wa siku hizi hawazijui, ukimwambia mtu afungue browser a search kitu duh mtihan kweli.. wengi wanajua App tu.. Hizo blog tulifaid enz hizo bhana
 
Umeacha kazi kabla ya kuwa na uhakika wa kuingiza pesa.

Mimi ndio naanza Blogging lakini Kuna vitu kadhaa ambazo nimevisoma na kuwa Kama Roadmap endapo unataka Blog ikulipe
1)Uchague Niche Nzuri
2)Uandike post nyingi zenye ujazo na picha ndani (minimum post 60)
3)Uandike Content za kiingereza
4)Keywords & SEO
5)Mpangilio Nzuri wa maudhui

Blogging ipo hapo tu.
 
Blog vijana wa siku hizi hawazijui, ukimwambia mtu afungue browser a search kitu duh mtihan kweli.. wengi wanajua App tu.. Hizo blog tulifaid enz hizo bhana
Google Search ndio mtandao unaoongozwa kutembelwa na watu wengi hapa Tanzania. (Alexa ranking)
 
Kama target yako ni watanzani pekee, inabidi contents zako ziwe za kijinga jinga kama umbea, comedy hapo utawakamata chap....! Ila kama ni content za madini target worldwide tumia lugha ya malaika hapo utakua fastaa.! La sivyo hiyo kazi itakushinda....! Ila mkuu hujasema content yako ni ipi inawezekana youtube ungefanya poa zaidi...! Weka wazi content yako tukushauri
Huu si ukweli, Nina website na haiandiki vitu udaku wala ujinga, ina miezi sita Kwa sasa inapata watembeleaji 22,000 Kwa mwezi na ninaweza kui-monetize bila kutumia matangazo ya AdSense wala kampuni yoyote ya matangazo Kwa Sababu wanaotembelea ni wateja WA uhakika wanaotafuta taarifa za bidhaa Fulani kupitia Google Search. Na 97% ya traffic ni kutoka Tanzania
 
Back
Top Bottom