Nina uhahika 98% hawajui hili

Kiswahili kigumu sana... Japo tafsiri yake hapo ni KUKUHAMU
Kupeza ndio neno linalotumika, na hata ukiangalia hizi tamthilia zinazofanyiwa tafsiri ya lugha ya kiswahili za Azam TV na Star Times Swahili hutumia neno hilo
 
acha uongo mkuu,, NIMEKUMISS=NIMEKUKOSA
Nimekukosa?? Direct translation ni common mistake. I don't blame you!!

Kwa namna moja upo sawa - if you were a sniper, shooting to kill someone, and you missed the shot hapo ungesema "I missed you!" kwa tafsiri ya kuwa umemkosa ila kwenye kuonesha hisia za kumkumbuka mtu sababu ya absence yake ni "UMEMUPEZA."
 
Nimekukosa?? Direct translation ni common mistake. I don't blame you!!
Kwa namna moja upo sawa - if you were a sniper, shooting to kill someone, and you missed the shot hapo ungesema "I missed you!" kwa tafsiri ya kuwa umemkosa ila kwenye kuonesha hisia za kumkumbuka mtu sababu ya absence yake ni "UMEMUPEZA."
Shukrani mkuu. Yani hapo ulichofanya ni kumpatia maji mtu aliyekuwa na kiu kali sana. Mifano yako inajitosheleza vya kutosha maana watu walikuwa hawanielewi kabisa
 
Nakumbuka pia nilishawahi kutoa uzi unaoeleza kuwa chips kwa kiswahili zinaitwa "VIBANZI" ila niliambiwa mi mwongo ninabunibuni maneno
Maneno mengi ya kiswahili yamepotea kwa sababu tulio wengi wa Tanzania hatuna utaratibu wa kusoma vitabu vya zamani kidogo au hata kamusi. Ndio, kiswahili ni lugha yetu ya taifa, lakini hatuijui.

Kiswahili kipo complicated kuliko hata tunavyoweza kuelezea.
 
Maneno mengi ya kiswahili yamepotea kwa sababu tulio wengi wa Tanzania hatuna utaratibu wa kusoma vitabu vya zamani kidogo au hata kamusi. Ndio, kiswahili ni lugha yetu ya taifa, lakini hatuijui.

Kiswahili kipo complicated kuliko hata tunavyoweza kuelezea.
Ila kama ulivyosema, tutafika tu.
 
Habari wa JamiiForum.

Najua imezoeleka katika jamii zetu kwa rika zote (watoto,vijana,wazazi, na hata wazee) aidha wasomi au wasio wasomi kutumia neno Nimekumiss pale unapomaanisha kumkumbuka mtu hasa uwepo wake. Hata hivyo neno mbadala la kiswahili ni Kupeza hivyo basi unaweza ukwamwambia mpendwa wako kuwa Nimekupeza
I miss you, maana yake una hamu ya (uwepo) wa mtu, sidhani kama ni kumkumbuka.
 
Habari wa JamiiForum.

Najua imezoeleka katika jamii zetu kwa rika zote (watoto, vijana, wazazi na hata wazee) aidha wasomi au wasio wasomi kutumia neno Nimekumiss pale unapomaanisha kumkumbuka mtu hasa uwepo wake. Hata hivyo neno mbadala la kiswahili ni Kupeza hivyo basi unaweza ukwamwambia mpendwa wako kuwa Nimekupeza
angalau leo nimepata jina la kutumia ....asante
 
13 Reactions
Reply
Back
Top Bottom