Nina tatizo la kutapika nyongo mara kwa mara

Flashfifty

JF-Expert Member
Feb 10, 2021
226
563
Habari wadau, naombeni msaada wenu na ushauri,

Nina tatizo la kutapika nyongo mara kwa mara na limeanza muda mrefu kidogo huu ni mwaka wa nne unaenda tafadhali naombeni msaada wenu maana hata hospital napatiwa antiacids lakini hazinisaidia.

Asanteni.
 
Pole sana, kiuhalisia ni vigumu sana kutapika nyongo, kimaumbile nyongo (bile) inaingia kwenye mfumo wa mmeng'enyo wa chakula kwenye utumbo mwembamba hivyo sio rahisi kutapika nyongo labda kama una tatizo la utumbo kuziba, nakushauri umuone daktari bingwa wa magonjwa ya ndani (Physician) nina imani tatizo lako litatatuliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana, kiuhalisia ni vigumu sana kutapika nyongo, kimaumbile nyongo (bile) inaingia kwenye mfumo wa mmeng'enyo wa chakula kwenye utumbo mwembamba hivyo sio rahisi kutapika nyongo labda kama una tatizo la utumbo kuziba, nakushauri umuone daktari bingwa wa magonjwa ya ndani (Physician) nina imani tatizo lako litatatuliwa.

Sent using Jamii Forums mobile app

Asante nashukuru
 
Unaweza kuelezea kwa week moja iliyopita umetapika mara ngapi? au week ya mwisho kutapika ni lini na ulitapika mara ngapi ndani ya siku na kwa week nzima?

Unajua je unatapika nyongo? ishara inayokwambia hiini nyongo ni ipi?

una uhakika unatapika au unachanganya kutapika na kucheua(regurgitation)?

Nina hakika ishara unayoitumia kusema unatapika nyongo inaweza isiwe ya kweli kama mdau alivyosema hapo juu, sio rahisi kutapika nyongo bila utumbo kuwa umeziba.

Emu tuelezee zaidi historia yako, wewe ni Me au Ke, umri wako, ugonjwa wowote sugu, historia ya kutapika kwa kuelezea rangi ya matapishi, matapishi hayo huruka?, huwa unatapika wakati gani, ukiwa umemaliza kula au ukiwa haujala, kitu gani uchochea wewe kutapika?

Je, kabla haujatapika au siku ukitapika kunakuepo na dalili nyingine kama kizunguzungu, kichwa kuuma?
 
Unaweza kuelezea kwa week moja iliyopita umetapika mara ngapi? au week ya mwisho kutapika ni lini na ulitapika mara ngapi ndani ya siku na kwa week nzima?....
Kwanza ilianza dalili za kiungulia hapo ni miaka mitatu nyuma na vipimo vikaonesha nina ulcerz baada ya kutumia tiba ya ulcerz nikabak nikisumbuliwa na kiungulia kikali sana pamoja na kutapika mate machachu meupe kama mlenda na hii hali ikawa ikitokea mara tatu mpaka mbili ndan ya kila mwez na ndipo mate yake yakaanza kuambatana na kutapika maji machungu yenye rangi ya njano kabisa so hali hii imekua ikijirudia kila mwez ndan ya siku mbili au tatu na hupotea then mwez mwingine itakua hivyo hovyo.

Jinsia yangu ni ke nina miaka 29 na mara nyingi huwa naitapika asubuh mara chache sana kuitapika usiku ambapo inakua ni katikati ya usingiz najiskia kichefchef na nitaamka na kuitapika hiyo manjano chungu sana
 
Unaweza kuelezea kwa week moja iliyopita umetapika mara ngapi? au week ya mwisho kutapika ni lini na ulitapika mara ngapi ndani ya siku na kwa week nzima?....
Dalili ambayo huanza kabla ya kutokea hali hii ni kusikia kama tumbo limejaa apetite ya chakula kupotea yan tumbo kuvurugika halielewek na kuwashwa mwili pindi ninapotoka kuoga mwili unawasha kama nimepakwa upupu kwa muda mfupi na kuacha ila baada ya kutapika hali zote hutoweka yaan baada ya kuitapika hiyo manjano yote
 
Kwanza ilianza dalili za kiungulia hapo ni miaka mitatu nyuma na vipimo vikaonesha nina ulcerz baada ya kutumia tiba ya ulcerz nikabak nikisumbuliwa na kiungulia kikali sana pamoja na kutapika mate machachu meupe kama mlenda na hii hali ikawa ikitokea mara tatu mpaka mbili ndan ya kila mwez na ndipo mate yake yakaanza kuambatana na kutapika maji machungu yenye rangi ya njano kabisa so hali hii imekua ikijirudia kila mwez ndan ya siku mbili au tatu na hupotea then mwez mwingine itakua hvo hvo
Jinsia yangu ni ke nina miaka 29 na mara nyingi huwa naitapika asubuh mara chache sana kuitapika usiku ambapo inakua ni katikati ya usingiz najiskia kichefchef na nitaamka na kuitapika hiyo manjano chungu sana
Inawezekana una tatizo la GERD ( Gastro Esophageal Reflux Disease) hili linafanana sana na vidonda vya tumbo japo matibabu yake ni tofauti kidogo, bado nashauri upate muda wa kumuona daktari bingwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inawezekana una tatizo la GERD ( Gastro Esophageal Reflux Disease) hili linafanana sana na vidonda vya tumbo japo matibabu yake ni tofauti kidogo, bado nashauri upate muda wa kumuona daktari bingwa

Sent using Jamii Forums mobile app

Asante sana hili pia nimewah kuambiwa na daktar mmoja wa kcmc hiyo GERD nashukuru umenifumbua nilifatilie kwa ukaribu zaid kwa kumuona specialist
 
Habari wadau, naombeni msaada wenu na ushauri,

Nina tatizo la kutapika nyongo mara kwa mara na limeanza muda mrefu kidogo huu ni mwaka wa nne unaenda tafadhali naombeni msaada wenu maana hata hospital napatiwa antiacids lakini hazinisaidia.

Asanteni.

Pole kwa kuumwa.
Hili ni suala la kutanabaisha kati ya kutapika na kuwa na hali ya vitu vilivyoko tumboni kurudi kinywani bila utashi/reflux.

Kama ni reflux, tatizo linawezakuwa liko kwenye kifundo kilichopo pale ambapo tumbo la chakula linapoanzia.

Kifundo hiki kina kazi ya kuzuia vitu vilivyoko tumboni visirudi kinywani. Kutokufanya kazi vyema kwa kifundo hicho huweza kusababisha vyakula kurudi kirahisi.

Moja ya sababu zinazohusishwa ni:
1: Unene kupita kiasi
2: Kukonda sana
3: Hernia kwenye eneo husika
4: Presha ya uvimbe eneo husika
5: Matumizi ya baadhi ya madawa
Nk.

Ni vyema kufika hospitali ili kutanabaisha ni nini hasa chanzo na tiba yako iweje.
 
Pole kwa kuumwa.
Hili ni suala la kutanabaisha kati ya kutapika na kuwa na hali ya vitu vilivyoko tumboni kurudi kinywani bila utashi/reflux.

Kama ni reflux, tatizo linawezakuwa liko kwenye kifundo kilichopo pale ambapo tumbo la chakula linapoanzia.

Kifundo hiki kina kazi ya kuzuia vitu vilivyoko tumboni visirudi kinywani. Kutokufanya kazi vyema kwa kifundo hicho huweza kusababisha vyakula kurudi kirahisi.

Moja ya sababu zinazohusishwa ni:
1: Unene kupita kiasi
2: Kukonda sana
3: Hernia kwenye eneo husika
4: Presha ya uvimbe eneo husika
5: Matumizi ya baadhi ya madawa
Nk.

Ni vyema kufika hospitali ili kutanabaisha ni nini hasa chanzo na tiba yako iweje.

Asante sana nashukuru kwa ufafanuzi pia nalifatilia kwa kina zaid kwa kumuona specialist
 
Gastroenterologist/daktari bingwa wa njia ya chakula ni chaguo zuri kuanza naye kama utampata.

Nashukuru sana nitafatilia kwa kina na pia nitajaribu kuulizia huyo specialist nadhan ndio nitakapoweza kupata suluhisho la tatizo langu..
 
Inawezekana una tatizo la GERD ( Gastro Esophageal Reflux Disease) hili linafanana sana na vidonda vya tumbo japo matibabu yake ni tofauti kidogo, bado nashauri upate muda wa kumuona daktari bingwa

Sent using Jamii Forums mobile app

Habari za wakat huu....nashukuru kwa ushaur wako wa juu ya nani natakiwa kumuona due to tatizo langu kama nilivolielezea hapo juu na nmefanya kama ushaur wako ulivosema na nimeambiwa ni hiyo GERD according to vipimo..niko ktk hatua za kupata matibabu na kufuata masharti nashukuru sana
 
Pole kwa kuumwa.
Hili ni suala la kutanabaisha kati ya kutapika na kuwa na hali ya vitu vilivyoko tumboni kurudi kinywani bila utashi/reflux.

Kama ni reflux, tatizo linawezakuwa liko kwenye kifundo kilichopo pale ambapo tumbo la chakula linapoanzia.

Kifundo hiki kina kazi ya kuzuia vitu vilivyoko tumboni visirudi kinywani. Kutokufanya kazi vyema kwa kifundo hicho huweza kusababisha vyakula kurudi kirahisi.

Moja ya sababu zinazohusishwa ni:
1: Unene kupita kiasi
2: Kukonda sana
3: Hernia kwenye eneo husika
4: Presha ya uvimbe eneo husika
5: Matumizi ya baadhi ya madawa
Nk.

Ni vyema kufika hospitali ili kutanabaisha ni nini hasa chanzo na tiba yako iweje.

Habari za wakati huu...napenda kutoa shukran kwa ushaur wako and according to vipimo nmeambiwa tatizo ni hiyo GERD bado nalitaftia ufumbuz wa namna ya kuweza kuondokana nalo..asante sana
 
Habari za wakat huu....nashukuru kwa ushaur wako wa juu ya nani natakiwa kumuona due to tatizo langu kama nilivolielezea hapo juu na nmefanya kama ushaur wako ulivosema na nimeambiwa ni hiyo GERD according to vipimo..niko ktk hatua za kupata matibabu na kufuata masharti nashukuru sana
Ni jambo jema kuwa hatimae umegundua tatizo linalokusumbua, umefanya vizuri kuleta mrejesho, naimani daktari amekueleza matibabu ya tatizo lako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni jambo jema kuwa hatimae umegundua tatizo linalokusumbua, umefanya vizuri kuleta mrejesho, naimani daktari amekueleza matibabu ya tatizo lako

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna dawa nmepatiwa plus masharti magumu sana ambayo nimeambiwa hayo masharti ni tiba kuliko hata hizo dawa sasa kwa hali zetu za maisha ni ngumu kuweza kukaza kwenye masharti thou nitajitahid kadri ya uwezo wangu pia ningeomba kama unajua dawa ambayo inaweza kuwa ni tiba kabisa
 
Kuna dawa nmepatiwa plus masharti magumu sana ambayo nimeambiwa hayo masharti ni tiba kuliko hata hizo dawa sasa kwa hali zetu za maisha ni ngumu kuweza kukaza kwenye masharti thou nitajitahid kadri ya uwezo wangu pia ningeomba kama unajua dawa ambayo inaweza kuwa ni tiba kabisa
Kwa sababu sijui dawa aliyokupa daktari, nakushauri uendelee kuzitumia ulizopewa kwa kama ulivyo elekezwa na ufuate masharti na kuzingatia kurudi tena kumuona daktari wako kwa ajili ya follow up

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom