Nina sifa zote lakini sipati mpenzi, je nina gundu?

Heshima mbele waungwana.

Kuna ishu inanitatiza sana wakuu, kipindi cha nyuma, hususan wakati nikiwa nasoma high school na baada ya kumaliza form six (mwaka 2006) nilikuwa na zali sana la kupendwa na wasichana kiasi kwamba nishawahi tongozwa na wasichana kadhaa, na hali iliyonifanya nisipate tabu kabisa kutafuta madem by that time, kwa kweli nilikuwa na wasichana wengi ambao walifika 7 na wote walikuwa active (ndani ya miaka 2 tu), kwa kipindi nikiwa a-level, mpaka namaliza mwaka 2006 hadi najianda kuanza chuo mwaka 2007.

Mwaka 2007 kwenye mwezi wa 6 niliamua kubadili tabia na nikashawishika kwenda kupima ukimwi kwa mara ya kwanza, na nikasema kama nikiwa negative, basi naachana kabisa na mambo ya kuwa na wasichana wengi, namshukuru mungu nilienda pale angaza mnazi mmoja na nikapima na majibu yakatoka niko poa kabisa, kuanzia pale nikawapiga chini wale madem mmoja baada ya mwingine, kwa kweli watatu kati ya hao 7 walishikwa na uchungu na walinililia sana na ilifikia kipindi nikawaambia nimeamua kuokoka, so ni mpaka nifunuliwe.

Sasa baada ya pale niliishi kwa amani sana na nilipata nafasi ya kujiunga na chuo kikuu mwaka 2007 huo huo. Baada ya pale sikuwa kabisa na ishu za wasichana, na mpaka namaliza chuo nilikuwa peke yangu, na sikuwahi ku experience ile hali ya "kutokewa" na wasichana kwa kipindi chote chuoni hali iliyonifanya nifanye vizuri kwenye course zote mpaka namaliza mwaka wa 3 sijawai pata supplementary .

Nilimaliza chuo mwaka jana 2010, na namshukuru mungu suala la ajira halikunisumbua kwani nilipata kazi nzuri tu.

Tatizo linalonisumbua ni kwamba kwa sasa ndio nahitaji sasa nimpate msichana mwenye heshima na mtulivu ili kama tukienda vyema, nimuandae kwa ajili ya kufanya naye future.

Wakuu hili limekuwa ni bonge la changamoto, maana sioni hata msichana yoyote mwenye time na mimi, japokuwa now days nina tofauti kubwa na kipindi hicho cha nyuma, kipindi cha nyuma nilikuwa mwembamba na kamwili kadogo tofauti na sasa hivi nimepata mwili na ninafanya mazoezi kiasi kwamba nina mwonekano mzuri ukilinganisha na kipindi kile, lakini zaidi ya hapo ni kwamba, now days nina hela kiasi kwamba kuwa na milioni 2, 3 kwenye account yangu ni kitu cha kawaida tofauti na kipindi cha nyuma ambapo sijawahi kuwa hata na laki moja na sijawahi hata siku moja kumhonga dem hela wala kumnunulia nguo lakini nilikuwa napendwa.

Imefikia wakati naanza kuwaza isije kuwa miongoni mwa wale wasichana niliokuwa nao alinisababishia gundu ndo maana sipati msichana wa kufanya uhusiano.

Naombeni mnisaidie waungwana.

Nifanye nini?

Je jambo hili ni la kawaida au kuna kitu hapa?

kweli watanzania bado tunaitaji kufanya kazi sana ili tuweze kukabiliana na haya mabadiliko ya kidunia na utandawazi. graduate anapofikiria ushirikina katika mapenzi na kuamua kupost thread jf ili akina ritz, faizafox,omr,mwita,zomba na............... wajue kwamba yeye ni handsome anahela kama million 2 or 3 kwenye his bank account.na maelezo kibao ya kuonyesha jinsi gani alivyokuwa akibadilisha wanawake.
jiulize nani anayekusifu kwa kuwabadili wanawake. bulll...shit.........mwenzio sijui yupo wapi naye alitokea udom akaja na habari za uhandsome apa jf. alichokipata anajua mwenyewe. jiandae kufata nyayo zake.
 
Dah, pole sana..
Lakini jina Zipompapompa mbona limekaa kike zaidi?
 
kweli watanzania bado tunaitaji kufanya kazi sana ili tuweze kukabiliana na haya mabadiliko ya kidunia na utandawazi. graduate anapofikiria ushirikina katika mapenzi na kuamua kupost thread jf ili akina ritz, faizafox,omr,mwita,zomba na............... wajue kwamba yeye ni handsome anahela kama million 2 or 3 kwenye his bank account.na maelezo kibao ya kuonyesha jinsi gani alivyokuwa akibadilisha wanawake.
jiulize nani anayekusifu kwa kuwabadili wanawake. bulll...shit.........mwenzio sijui yupo wapi naye alitokea udom akaja na habari za uhandsome apa jf. alichokipata anajua mwenyewe. jiandae kufata nyayo zake.

kwake hizo ni sifa "zote", kazi ipo!
 
kweli watanzania bado tunaitaji kufanya kazi sana ili tuweze kukabiliana na haya mabadiliko ya kidunia na utandawazi. Graduate anapofikiria ushirikina katika mapenzi na kuamua kupost thread jf ili akina ritz, faizafox,omr,mwita,zomba na............... Wajue kwamba yeye ni handsome anahela kama million 2 or 3 kwenye his bank account.na maelezo kibao ya kuonyesha jinsi gani alivyokuwa akibadilisha wanawake.
Jiulize nani anayekusifu kwa kuwabadili wanawake. Bulll...shit.........mwenzio sijui yupo wapi naye alitokea udom akaja na habari za uhandsome apa jf. Alichokipata anajua mwenyewe. Jiandae kufata nyayo zake.

mkuu nachelea kusema kwamba umenielewa vibaya, na wala sipo hapa kwa ajili ya kujisifu maana ni upuuzi kujisifu with anonymous id, nani anayenijua hapa jf?? Mkuu wewe hujui lakini mwenzako kila siku najiuliza sababu ni nini, may be hayajakukuta ndo maana unaona nimekuja kujisifu.
 
kwa kifupi watafuta msichana humu jf!
Au nimekosea mkuu

in short sina kawaida ya kutafuta wasichana sehem za namna hii, nimekuja ku-shere hapa mmu nikijua huenda kuna mtu ashawai kutana na ishu kama yangu, what if kama kuna kitu nakosea??
 
Unajua nini mwombe mungu mwanangu ndo mpango mzima alafu fanya urafiki na wasichana wengi esp wale unao wataka ili uweze kusort, hela ndo kila kitu mzee make more frind 2mia hela jaman.
 
unamvuto wa nje Huna swaga kwa madem ndo maana wanakupotezea be flexible jichanganye na watu mademu wako wengi sana afu usisahau ku hangout clasic areas.kila la kheri
 
in short sina kawaida ya kutafuta wasichana sehem za namna hii, nimekuja ku-shere hapa mmu nikijua huenda kuna mtu ashawai kutana na ishu kama yangu, what if kama kuna kitu nakosea??

hakuna hata binti unayeona ana kidalili cha kumind swaga zako? Au unawafungia vioo?
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom