wazunguwawili
JF-Expert Member
- May 29, 2019
- 3,984
- 4,131
Madam tuandikie stori..japo hata page 10.Umenikumbusha miaka Zaid ya mitano nyuma nilipoenda marekani kwa mara ya kwanza, nilienda kwa mwaliko wa shirika na nilikua peke yangu kutoka tanzania..bas nikaingia kwenye ndege sijui chochote na kwenye gar hata sioni mbongo mwenzangu yaani niko peke yangu dah! Lakini sikua na wasiwasi sana zaid ya furaha tu! Kimbembe ni tulifika sehem tunataka kubadilisha ndege asee mpaka leo huwa nachekaaa akili ikanijia niulize wale polis mle ndani.
Sasa jaman ugeni huu..naenda kumuuliza na Kiingereza changu cha kuunga nimesahau sasa ntasema marekan? Aah polis hajui marekan kimoyo moyo nasema sasa hili jina la marekani lilitokea wap? Sasa niseme amerika? Amerika si bara hatonielewa aah nikaachana naye nikaanza kufata watu..baahat nzuri kulikua na muda mrefu kabla ya kubadili ndege ndiyo nikaenda kusoma kwenye zile board zao nikaona napotakiwa kwenda..kiufup ni kama vile kulikua tu na roho mtakatifu ananiongoza.
Mpaka baadae tunashuka airpot ya D.C ndiyo nikakutana na mbongo tukasalimiana sasa pale ndiyo tunatoka nje ya uwanja na vimbwa vyao vile vinatunusa dah! Nikachukua tax hadi hotelini lakini jina la marekan lilinisumbua sana kwakwel...tulikaa wiki mbili siku ya kurudi tena niko peke yangu uwanjani mle kuna sehem ya kupanda zile tren za ndani heehee nasikiliza tren imetaja kituo nikadandia chap..kutika ndan aah mbona tena kama siyo hii nikashuka fasta kufika chini tu nikauliza nikaambiea ndiyo hiyohiyo zena chap nikarukia kwa mlango mwingine jaman siku ile nilitetemeka uwiiii..ngoja niishie hapa lakin mkuu we nenda tu utafika tu wala hutopotea.
Unajua kusimulia kwa kweli.
Vp migegedo ya huko kama ilitokea?