Nina ndoto ya kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania siku moja huko mbeleni

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,217
26,008
Amani iwe nanyi wadau!

Kama kichwa cha uzi kinavojielezea hapo juu hii ndo ndoto yangu kuu siku moja. Na kwa kadri siku zinavyozidi kwenda naona hii ndoto inazidi kuwa na muamko mkubwa.

kwanza kabisa Mimi ni mfuasi wa sera za kipebari kiuchumi kumaanisha kila mtu anakuwa huru kushiriki kwenye uchumi na kujenga maisha bora kwake na kwa jamii yake. Sio muumini wa serikali kukamata njia za uchumi kwa sababu naamini hii inawanyima fursa watu kuwa creative na innovative, inawanyima watu fursa ya kukua na kuchangamsha akili zao.

Kwa jinsi nilivyoiona nchi yangu kwa umri wangu, nimegundua kuwa ingawa tutajisifu kuwa na maendeleo ila Sera zetu za kijamaa zimetufanya kuwa jamii ambayo haifikirii sawasawa hasa kwenye suala la maendeleo na pili zimetufanya kuwa na tofauti kubwa sana ya kimaisha kati ya wenye nacho na wasio nacho kiasi kwamba imekuwa ni lazima ili mtu aendelee na kufanikiwa ni lazima daraja la wenye nacho liweze kukubali aendelee. Hili nitalielezea vizuri badae.

Hivyo nitalazimika kuomba nafasi ya uraisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania huko mbele kwa sababu zifuatazo

1. Kufutilia mbali Sera zote za kijamaa ambazo kiukweli sio tu zimetufanya tushindwe kuwa na maendeleo tunayostahili ila zimefanya jamii yetu kugubikwa na ujinga uliokithiri. Kwenye hili nitafanya mabadiriko makubwa kwenye sera zote za elimu, uchumi na biashara kuwezesha na kufanya watu wafikiri tofauti kuhusu maendeleo yao na maisha yao, pili watu washiriki kwa Uhuru bila vikwazo kwenye shughuli za ubunifu na biashara wakijua kuwa watapata faida kubwa na kubadirisha jamii zao na maisha yao.

Mtu atakuwa huru kusajili kwa jina lake ubunifu wake wowote aliouanzisha na kuiuzia serikali, kampuni au shirika lolote ubunifu wake huo na kufaidika nao.

2. Nitabadirisha sera zote za kibiashara. Nitaweka mfumo kuwa mtu anaposajili biashara au kampuni , anafanya application yake kwenye taasisi moja tu na anapata vibali vyote anavyoitaji kwenye taasisi hiyo tu. Kuanzia vibali vya reseni zote mpaka TIN no. Zoezi la kupata vibali hivyo halitachukua zaidi ya siku 14. (Maximum)

3. Nitafumua na kuboresha kwa asilimia 100 Sera zote za makazi na mipango miji. Itakuwa ni lazima kwa kila mwananchi kuishi kwenye makazi yaliyopangwa na yenye huduma zote za msingi (Shule na Hospitali). Nitaweka mwongozo maalumu wa ujenzi kuanzia makazi, sehemu za biashara hadi maeneo ya starehe. Hakutakuwa na Bar ya wazi wala sehemu ya muziki ya wazi. Muongozo utatolewa sehemu zote zijengwe kuwezesha privacy na kuzuia bughuza kwa watu wengine.

Itakuwa marufuku kwa watu kufanya biashara kwenye mazingira Holela. Sehemu zote za biashara ziwe za barabarani au masoko zitajengwa na kupangwa vizuri , kuwezesha wafanyabiashara sio tu kuwa wanafanya biashara zao kwenye mazingira mazuri, safi na yaliyopangwa vizuri bali wanaona thamani ya kazi zao na utu wao.

4. Nitahimiza kilimo safi, chenye ubora na uwekezaji mkubwa wa ndani na nje kwenye kilimo, kuwezesha sio tu sekta ya kilimo inaajili na kufaidisha watu wengi ila inazalisha vya kutosha na kuifaidisha nchi kiusalama na kiuchumi.

5. Sayansi na Teknolojia- Nitahimiza na kuwekeza sana kwenye tafiti za kisayansi na kiteknolojia kuwezesha zinaifaidisha nchi kiusalama na kiuchumi. Mtu akiwa na teknolojia yake serikali inaweza kushirikiana nae katika kuiendeleza na kutumia kwenye jamii. Hili litafanya huyo mtu alipwe na serikali na hata kampuni binafsi pale watakapoitaji

5. Kuhusu wafugaji- Nitana kusimamia ufugaji wa kibiashara. Wafugaji wote watapigwa marufuku kufanya ufugaji wa kuhama. Watalazimishwa kufuga kiteknolojia kwa kufuga mbegu bora zinazohimili mazingira yao. Nitahimiza na kukaribisha uwekezaji wa kimkakati wa viwanda vya bidhaa za mifugo Mf nyama na maziwa ili kuwezesha wafugaji wauze nyama zao na maziwa yao kwenye viwanda husika.

Miondombinu
Nitahimiza na kuwekeza kwenye ujenzi wa barabara kubwa zenye viwango vya kisasa( njia 3-4 kwa barabara moja) kwenye miji yote mikubwa na ya kibiashara. Nitaruhusu na uwekezaji binafsi kwenye sekta ya miundombinu kuruhusu kampuni kubwa kujenga reli na barabara za kodi ( Toll roads) Hii itawezesha si tu miji yetu kupendeza ila serikali kupata mapato mengi na mazuri kwa kuihudumia jamii.

Mazingira
Nitahimiza na kusimamia utunzaji wa mazingira kwa nguvu kubwa. Nitahimiza ushiriki wa sekta binafsi katika kuanzisha misitu, mapori na hifadhi ambazo si tu zitatumika kibiashara Bali katika kuhakikisha mazingira yanakuwa mazuri na afya za wananchi zinakuwa salama. Katik mikoa yenye ukame tafiti zitafanywa za miti ya kupandwa kwenye mikoa hiyo na nitahakikisha inapandwa tena kwa kiwango kikubwa sana. Nitahimiza ushiriki mkubwa wa sekta binafsi katika kutangaza na kukupa utalii. Nchi itakuwa branded vizuri kwenye media za kimataifa hasa kwenye suala la utalii na kuhakikisha tunakuwa na watalii wasiopungua milioni 10 kwa mwaka.

Ulinzi na Usalama

Kimfumo sitabadilisha sana ila nitafanya vyombo viwe vya kisasa vinavyotumia teknolojia bora na vyenye zana nyingi na za kisasa. Nitafanya uwekezaji mkubwa kwenye jeshi la anga na maji kuwezesha kuwa na military bases kwenye visiwa vyetu bahari kuu na pia kuimarisha ulinzi wa bahari kuu na rasilimali zetu za kwenye maji.

Hospitali na afya
Nitahimiza uwekezaji wa serikali na sekta binafsi kwenye hospitali bora , za kisasa na zenye vifaa vya kisasa.

Asilimia fulani ya mapato ya serikali yatagharamia bima ya afya kwa wazee, walemavu na watu wasio na ajira. Itakuwa ni lazima kwa kila mwananchi kuwa na bima ya afya ambayo itagharimiwa na serikali kwa asilimia kadhaa ( Kutemegea kama ana ajira au la au yuko kwenye hayo makundi maalum)

Elimu

Nitabadirisha kabisa mitaala yote ya elimu ili iendane sio tu na mabadiriko ya dunia ila iwafanye watoto wetu wafikiri kama sayansi ya teknolojia inavyoenda na kama Sera mpya za kipebari zinavyoeleza. Nitaboresha mazingira ya shule zetu zote na kuzifanya ziwe safi na bora kwa elimu ya watoto wetu.

Mwisho nitabadiri aina ya utawala wa Taifa letu na kuondoa wakuu wa Mikoa na Wilaya. Nchi yetu itakuwa na majimbo yasiyozidi 8 na yatatawaliwa na magavana. Watapigiwa kura na kujipangia maendeleo yao kwa uhuru.

Ipo siku. Sio leo bali inakuja na itafika tu!

Mungu awe nasi!
 
Vilevile bado nafikiria Chama. Mimi sio mpenzi wa ujamaa, ni mfuasi wa ubepari wa Xi jinping na Deng Xiaoping
 
Amani iwe nanyi wadau!

Kama kichwa cha uzi kinavojielezea hapo juu hii ndo ndoto yangu kuu siku moja. Na kwa kadri siku zinavyozidi kwenda naona hii ndoto inazidi kuwa na muamko mkubwa.

kwanza kabisa Mimi ni mfuasi wa sera za kipebari kiuchumi kumaanisha kila mtu anakuwa huru kushiriki kwenye uchumi na kujenga maisha bora kwake na kwa jamii yake. Sio muumini wa serikali kukamata njia za uchumi kwa sababu naamini hii inawanyima fursa watu kuwa creative na innovative, inawanyima watu fursa ya kukua na kuchangamsha akili zao.

Kwa jinsi nilivyoiona nchi yangu kwa umri wangu, nimegundua kuwa ingawa tutajisifu kuwa na maendeleo ila Sera zetu za kijamaa zimetufanya kuwa jamii ambayo haifikirii sawasawa hasa kwenye suala la maendeleo na pili zimetufanya kuwa na tofauti kubwa sana ya kimaisha kati ya wenye nacho na wasio nacho kiasi kwamba imekuwa ni lazima ili mtu aendelee na kufanikiwa ni lazima daraja la wenye nacho liweze kukubali aendelee. Hili nitalielezea vizuri badae.

Hivyo nitalazimika kuomba nafasi ya uraisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania huko mbele kwa sababu zifuatazo

1. Kufutilia mbali Sera zote za kijamaa ambazo kiukweli sio tu zimetufanya tushindwe kuwa na maendeleo tunayostahili ila zimefanya jamii yetu kugubikwa na ujinga uliokithiri. Kwenye hili nitafanya mabadiriko makubwa kwenye sera zote za elimu, uchumi na biashara kuwezesha na kufanya watu wafikiri tofauti kuhusu maendeleo yao na maisha yao, pili watu washiriki kwa Uhuru bila vikwazo kwenye shughuli za ubunifu na biashara wakijua kuwa watapata faida kubwa na kubadirisha jamii zao na maisha yao.

Mtu atakuwa huru kusajili kwa jina lake ubunifu wake wowote aliouanzisha na kuiuzia serikali, kampuni au shirika lolote ubunifu wake huo na kufaidika nao.

2. Nitabadirisha sera zote za kibiashara. Nitaweka mfumo kuwa mtu anaposajili biashara au kampuni , anafanya application yake kwenye taasisi moja tu na anapata vibali vyote anavyoitaji kwenye taasisi hiyo tu. Kuanzia vibali vya reseni zote mpaka TIN no. Zoezi la kupata vibali hivyo halitachukua zaidi ya siku 14. (Maximum)

3. Nitafumua na kuboresha kwa asilimia 100 Sera zote za makazi na mipango miji. Itakuwa ni lazima kwa kila mwananchi kuishi kwenye makazi yaliyopangwa na yenye huduma zote za msingi (Shule na Hospitali). Nitaweka mwongozo maalumu wa ujenzi kuanzia makazi, sehemu za biashara hadi maeneo ya starehe. Hakutakuwa na Bar ya wazi wala sehemu ya muziki ya wazi. Muongozo utatolewa sehemu zote zijengwe kuwezesha privacy na kuzuia bughuza kwa watu wengine.

Itakuwa marufuku kwa watu kufanya biashara kwenye mazingira Holela. Sehemu zote za biashara ziwe za barabarani au masoko zitajengwa na kupangwa vizuri , kuwezesha wafanyabiashara sio tu kuwa wanafanya biashara zao kwenye mazingira mazuri, safi na yaliyopangwa vizuri bali wanaona thamani ya kazi zao na utu wao.

4. Nitahimiza kilimo safi, chenye ubora na uwekezaji mkubwa wa ndani na nje kwenye kilimo, kuwezesha sio tu sekta ya kilimo inaajili na kufaidisha watu wengi ila inazalisha vya kutosha na kuifaidisha nchi kiusalama na kiuchumi.

5. Sayansi na Teknolojia- Nitahimiza na kuwekeza sana kwenye tafiti za kisayansi na kiteknolojia kuwezesha zinaifaidisha nchi kiusalama na kiuchumi. Mtu akiwa na teknolojia yake serikali inaweza kushirikiana nae katika kuiendeleza na kutumia kwenye jamii. Hili litafanya huyo mtu alipwe na serikali na hata kampuni binafsi pale watakapoitaji

5. Kuhusu wafugaji- Nitana kusimamia ufugaji wa kibiashara. Wafugaji wote watapigwa marufuku kufanya ufugaji wa kuhama. Watalazimishwa kufuga kiteknolojia kwa kufuga mbegu bora zinazohimili mazingira yao. Nitahimiza na kukaribisha uwekezaji wa kimkakati wa viwanda vya bidhaa za mifugo Mf nyama na maziwa ili kuwezesha wafugaji wauze nyama zao na maziwa yao kwenye viwanda husika.

Miondombinu
Nitahimiza na kuwekeza kwenye ujenzi wa barabara kubwa zenye viwango vya kisasa( njia 3-4 kwa barabara moja) kwenye miji yote mikubwa na ya kibiashara. Nitaruhusu na uwekezaji binafsi kwenye sekta ya miundombinu kuruhusu kampuni kubwa kujenga reli na barabara za kodi ( Toll roads) Hii itawezesha si tu miji yetu kupendeza ila serikali kupata mapato mengi na mazuri kwa kuihudumia jamii.

Mazingira
Nitahimiza na kusimamia utunzaji wa mazingira kwa nguvu kubwa. Nitahimiza ushiriki wa sekta binafsi katika kuanzisha misitu, mapori na hifadhi ambazo si tu zitatumika kibiashara Bali katika kuhakikisha mazingira yanakuwa mazuri na afya za wananchi zinakuwa salama. Katik mikoa yenye ukame tafiti zitafanywa za miti ya kupandwa kwenye mikoa hiyo na nitahakikisha inapandwa tena kwa kiwango kikubwa sana. Nitahimiza ushiriki mkubwa wa sekta binafsi katika kutangaza na kukupa utalii. Nchi itakuwa branded vizuri kwenye media za kimataifa hasa kwenye suala la utalii na kuhakikisha tunakuwa na watalii wasiopungua milioni 10 kwa mwaka.

Ulinzi na Usalama

Kimfumo sitabadilisha sana ila nitafanya vyombo viwe vya kisasa vinavyotumia teknolojia bora na vyenye zana nyingi na za kisasa. Nitafanya uwekezaji mkubwa kwenye jeshi la anga na maji kuwezesha kuwa na military bases kwenye visiwa vyetu bahari kuu na pia kuimarisha ulinzi wa bahari kuu na rasilimali zetu za kwenye maji.

Hospitali na afya
Nitahimiza uwekezaji wa serikali na sekta binafsi kwenye hospitali bora , za kisasa na zenye vifaa vya kisasa.

Asilimia fulani ya mapato ya serikali yatagharamia bima ya afya kwa wazee, walemavu na watu wasio na ajira. Itakuwa ni lazima kwa kila mwananchi kuwa na bima ya afya ambayo itagharimiwa na serikali kwa asilimia kadhaa ( Kutemegea kama ana ajira au la au yuko kwenye hayo makundi maalum)

Elimu

Nitabadirisha kabisa mitaala yote ya elimu ili iendane sio tu na mabadiriko ya dunia ila iwafanye watoto wetu wafikiri kama sayansi ya teknolojia inavyoenda na kama Sera mpya za kipebari zinavyoeleza. Nitaboresha mazingira ya shule zetu zote na kuzifanya ziwe safi na bora kwa elimu ya watoto wetu.

Mwisho nitabadiri aina ya utawala wa Taifa letu na kuondoa wakuu wa Mikoa na Wilaya. Nchi yetu itakuwa na majimbo yasiyozidi 8 na yatatawaliwa na magavana. Watapigiwa kura na kujipangia maendeleo yao kwa uhuru.

Ipo siku. Sio leo bali inakuja na itafika tu!

Mungu awe nasi!
Bwana mdogo hapo umewapa CCM desa muhimu sana ktk ilani yao ya mwaka huu ya uchaguzi, sehemu kubwa ya ulichokiweka ktk hoja zako itawalazimu kufanya "C&P" na pengine itakuwa "word by word'. Subiri muda kidogo ili uweze kushuhudia.
 
Huko mbeleni kwa kasi hii ya mjomba Magu hizo zote hazitakuwa hoja.

Subiri huo wakati ufike.
 
Amani iwe nanyi wadau!

Kama kichwa cha uzi kinavojielezea hapo juu hii ndo ndoto yangu kuu siku moja. Na kwa kadri siku zinavyozidi kwenda naona hii ndoto inazidi kuwa na muamko mkubwa.

kwanza kabisa Mimi ni mfuasi wa sera za kipebari kiuchumi kumaanisha kila mtu anakuwa huru kushiriki kwenye uchumi na kujenga maisha bora kwake na kwa jamii yake. Sio muumini wa serikali kukamata njia za uchumi kwa sababu naamini hii inawanyima fursa watu kuwa creative na innovative, inawanyima watu fursa ya kukua na kuchangamsha akili zao.

Kwa jinsi nilivyoiona nchi yangu kwa umri wangu, nimegundua kuwa ingawa tutajisifu kuwa na maendeleo ila Sera zetu za kijamaa zimetufanya kuwa jamii ambayo haifikirii sawasawa hasa kwenye suala la maendeleo na pili zimetufanya kuwa na tofauti kubwa sana ya kimaisha kati ya wenye nacho na wasio nacho kiasi kwamba imekuwa ni lazima ili mtu aendelee na kufanikiwa ni lazima daraja la wenye nacho liweze kukubali aendelee. Hili nitalielezea vizuri badae.

Hivyo nitalazimika kuomba nafasi ya uraisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania huko mbele kwa sababu zifuatazo

1. Kufutilia mbali Sera zote za kijamaa ambazo kiukweli sio tu zimetufanya tushindwe kuwa na maendeleo tunayostahili ila zimefanya jamii yetu kugubikwa na ujinga uliokithiri. Kwenye hili nitafanya mabadiriko makubwa kwenye sera zote za elimu, uchumi na biashara kuwezesha na kufanya watu wafikiri tofauti kuhusu maendeleo yao na maisha yao, pili watu washiriki kwa Uhuru bila vikwazo kwenye shughuli za ubunifu na biashara wakijua kuwa watapata faida kubwa na kubadirisha jamii zao na maisha yao.

Mtu atakuwa huru kusajili kwa jina lake ubunifu wake wowote aliouanzisha na kuiuzia serikali, kampuni au shirika lolote ubunifu wake huo na kufaidika nao.

2. Nitabadirisha sera zote za kibiashara. Nitaweka mfumo kuwa mtu anaposajili biashara au kampuni , anafanya application yake kwenye taasisi moja tu na anapata vibali vyote anavyoitaji kwenye taasisi hiyo tu. Kuanzia vibali vya reseni zote mpaka TIN no. Zoezi la kupata vibali hivyo halitachukua zaidi ya siku 14. (Maximum)

3. Nitafumua na kuboresha kwa asilimia 100 Sera zote za makazi na mipango miji. Itakuwa ni lazima kwa kila mwananchi kuishi kwenye makazi yaliyopangwa na yenye huduma zote za msingi (Shule na Hospitali). Nitaweka mwongozo maalumu wa ujenzi kuanzia makazi, sehemu za biashara hadi maeneo ya starehe. Hakutakuwa na Bar ya wazi wala sehemu ya muziki ya wazi. Muongozo utatolewa sehemu zote zijengwe kuwezesha privacy na kuzuia bughuza kwa watu wengine.

Itakuwa marufuku kwa watu kufanya biashara kwenye mazingira Holela. Sehemu zote za biashara ziwe za barabarani au masoko zitajengwa na kupangwa vizuri , kuwezesha wafanyabiashara sio tu kuwa wanafanya biashara zao kwenye mazingira mazuri, safi na yaliyopangwa vizuri bali wanaona thamani ya kazi zao na utu wao.

4. Nitahimiza kilimo safi, chenye ubora na uwekezaji mkubwa wa ndani na nje kwenye kilimo, kuwezesha sio tu sekta ya kilimo inaajili na kufaidisha watu wengi ila inazalisha vya kutosha na kuifaidisha nchi kiusalama na kiuchumi.

5. Sayansi na Teknolojia- Nitahimiza na kuwekeza sana kwenye tafiti za kisayansi na kiteknolojia kuwezesha zinaifaidisha nchi kiusalama na kiuchumi. Mtu akiwa na teknolojia yake serikali inaweza kushirikiana nae katika kuiendeleza na kutumia kwenye jamii. Hili litafanya huyo mtu alipwe na serikali na hata kampuni binafsi pale watakapoitaji

5. Kuhusu wafugaji- Nitana kusimamia ufugaji wa kibiashara. Wafugaji wote watapigwa marufuku kufanya ufugaji wa kuhama. Watalazimishwa kufuga kiteknolojia kwa kufuga mbegu bora zinazohimili mazingira yao. Nitahimiza na kukaribisha uwekezaji wa kimkakati wa viwanda vya bidhaa za mifugo Mf nyama na maziwa ili kuwezesha wafugaji wauze nyama zao na maziwa yao kwenye viwanda husika.

Miondombinu
Nitahimiza na kuwekeza kwenye ujenzi wa barabara kubwa zenye viwango vya kisasa( njia 3-4 kwa barabara moja) kwenye miji yote mikubwa na ya kibiashara. Nitaruhusu na uwekezaji binafsi kwenye sekta ya miundombinu kuruhusu kampuni kubwa kujenga reli na barabara za kodi ( Toll roads) Hii itawezesha si tu miji yetu kupendeza ila serikali kupata mapato mengi na mazuri kwa kuihudumia jamii.

Mazingira
Nitahimiza na kusimamia utunzaji wa mazingira kwa nguvu kubwa. Nitahimiza ushiriki wa sekta binafsi katika kuanzisha misitu, mapori na hifadhi ambazo si tu zitatumika kibiashara Bali katika kuhakikisha mazingira yanakuwa mazuri na afya za wananchi zinakuwa salama. Katik mikoa yenye ukame tafiti zitafanywa za miti ya kupandwa kwenye mikoa hiyo na nitahakikisha inapandwa tena kwa kiwango kikubwa sana. Nitahimiza ushiriki mkubwa wa sekta binafsi katika kutangaza na kukupa utalii. Nchi itakuwa branded vizuri kwenye media za kimataifa hasa kwenye suala la utalii na kuhakikisha tunakuwa na watalii wasiopungua milioni 10 kwa mwaka.

Ulinzi na Usalama

Kimfumo sitabadilisha sana ila nitafanya vyombo viwe vya kisasa vinavyotumia teknolojia bora na vyenye zana nyingi na za kisasa. Nitafanya uwekezaji mkubwa kwenye jeshi la anga na maji kuwezesha kuwa na military bases kwenye visiwa vyetu bahari kuu na pia kuimarisha ulinzi wa bahari kuu na rasilimali zetu za kwenye maji.

Hospitali na afya
Nitahimiza uwekezaji wa serikali na sekta binafsi kwenye hospitali bora , za kisasa na zenye vifaa vya kisasa.

Asilimia fulani ya mapato ya serikali yatagharamia bima ya afya kwa wazee, walemavu na watu wasio na ajira. Itakuwa ni lazima kwa kila mwananchi kuwa na bima ya afya ambayo itagharimiwa na serikali kwa asilimia kadhaa ( Kutemegea kama ana ajira au la au yuko kwenye hayo makundi maalum)

Elimu

Nitabadirisha kabisa mitaala yote ya elimu ili iendane sio tu na mabadiriko ya dunia ila iwafanye watoto wetu wafikiri kama sayansi ya teknolojia inavyoenda na kama Sera mpya za kipebari zinavyoeleza. Nitaboresha mazingira ya shule zetu zote na kuzifanya ziwe safi na bora kwa elimu ya watoto wetu.

Mwisho nitabadiri aina ya utawala wa Taifa letu na kuondoa wakuu wa Mikoa na Wilaya. Nchi yetu itakuwa na majimbo yasiyozidi 8 na yatatawaliwa na magavana. Watapigiwa kura na kujipangia maendeleo yao kwa uhuru.

Ipo siku. Sio leo bali inakuja na itafika tu!

Mungu awe nasi!
Mkuu nimekuelewa, mimi naomba uje unitue niwe Moja ya watendaji wakuu katika serikali yako.

Bado naendelea kujifunza, natumai muda ukifika nitakuwa nimeiva.
 
Bwana mdogo hapo umewapa CCM desa muhimu sana ktk ilani yao ya mwaka huu ya uchaguzi, sehemu kubwa ya ulichokiweka ktk hoja zako itawalazimu kufanya "C&P" na pengine itakuwa "word by word'. Subiri muda kidogo ili uweze kushuhudia.
CCM hawawezi kuondokana na sera za ujamaa. Wakifanya ivyo wataweza tawala hii nchi milele
 
Kila la kheri mkuu, nitakuwa ktk serikali yako Kama sio wewe kuwa ktk serikali yangu ili kukujenga kwanza kisiasa.
 
Kila la kheri mkuu, nitakuwa ktk serikali yako Kama sio wewe kuwa ktk serikali yangu ili kukujenga kwanza kisiasa.
Karibu ndugu. Natumai tutajenga pamoja serikali bora na taifa bora kuwai kutokea katika afrika yetu hii
 
Ngoja nifue kwanza sisi ambao bado single jumapili ndio siku ya usafi kwetu
 
Bwana mdogo hapo umewapa CCM desa muhimu sana ktk ilani yao ya mwaka huu ya uchaguzi, sehemu kubwa ya ulichokiweka ktk hoja zako itawalazimu kufanya "C&P" na pengine itakuwa "word by word'. Subiri muda kidogo ili uweze kushuhudia.
Kwani hata waki c&p mwisho wa siku anayefaidika si mwananchi..kwanini unakuwa m binafsi we Jomba. This is for public consumption
 
Back
Top Bottom