Nina mimba ya Miezi 9 natakiwa kusafiri kwenda ukweni

mshewa2

Member
Oct 30, 2012
77
12
Habari Wana JF

Mimi Nina mimba ya Miezi 9 nimebakisha week mbili nijifungue ila mume wangu analazimishia niende nikajifungulie huko kwao kanda ya ziwa, I thought of flying ila flights haziruhusu mtu wa type yangu kupanda ndege,so anasema tutaenda na gari taratibu hadi tufike even if it take us 3 days, Hospital nimeambiwa nisisafiri coz niko karibia kujifungua,he doesnt want to understand he think I'm jus making it coz I'm a medical personel 2, Hataki hata twende kwa specialist wote,wala hajawahi kwenda na mimi clinic,its our first born ,
Nifanyeje?nisafiri tu. kuwaridhisha ila its risk...anataka tusafiri 20th my due date ni 28th
 
Kuwa makini sana na huyo mumeo maana unaweza hata kujifungua before due date. Kwani ni kipi cha muhimu huko kwa wakwe au kuna daktari wa familia? Wewe umebeba mzigo miezi 9 unajua how u sufferd, usimridhishe mume na uteseke coz ni ujinga,kwanza hizo siasa za kujifungulia kwa wakwe zimepitwa na wakati.
 
miezi tisa,any time mtoto anaweza kuja,bora aje kabla ya hiyo 20th.Mueleweshe mme wako siku zimekwisha kwa sasa huwezi safiri,halafu mimba ya kwanza je uchungu ukiwakutia maporini huko mtafanya nini,kuna riski za kuchukua lakini sio hii aisee
 
mshewa2, Hongera saana kuwa kukaribia kuwa mama na kwa kubeba ujauzito hadi hapo ulipofikia.

Haya mambo ni mtihani saana. Hii inakuonesha kuwa ndoa sio ya watu wawili ni zaidi ya hapo. Naamini kuwa hadi umelileta hapa umejaribu kwa kila namna kumsomesha na kumuelewesha mumeo na hajakuelewa… Pole saana. Kwa condition ya uja uzito uliyo nayo bahati mbaya ama nzuri una emotions zaidi ya siku zote… Ila nakuomba vuta subira, jitahidi rudisha moyo na akili yako chini na uliangalie upya.

Kwa mtazamo wangu ni kuwa mumeo hakuwa na shida wewe kujifungulia ulipo sasa (yaani nyumbani kwenu); itakuwa nyumbani kwa wakwe zako wamesikia kuwa karibu unajifungua wakati wowote na wamemsisitiza mumeo kuwa ukazalie nyumbani kwao. Yeye kuomba hilo sio mbaya; mbaya ni kuwa hakukuarifu mapema kwani ilitakiwa uende hata mwezi mmoja kabla.

Nashauri ukubaliane nae… Sababu kujifungua huyo mtoto na hali wazazi wana vinyongo haitapendeza. Kama nilivyosema ni mtihani mkubwa aidha mwambie mumeo akubali kukodi mtu wa afya ya uzazi muambatane naye safari hadi nyumbani - USITHUBUTU kukubali mkawa wawili tu. AMA omba mtu mzima yeyote ambaye ni upande wa mumeo na ni karibu na familia ya upande wa mumeo na ueleze hali halisi… Na umuombe akufikishie hizo salamu kwa wakwe ukiahidi kuwa baada tu ya kujifungua salama utaenda huko nyumbani baada ya siku saba.

Hai mati kitu gani utachagua najua kwua lolote lile litakuumiza sababu mumeo hajatanguliza welfare yako na mtoto. Ila ndio hivo, hapa ni mwanzo taratibu mtasomana na kujuana na kujifunza namna ya kuchukuliana. Kila la kheri… Na Mwenyezi Mungu muweza akuwekee wepesi katika ujauzito hadi kujifungua. Pamoja Saana.
 
is it so very important?
jamani mimba miezi 9,imagine na hiyo miguu inavokua kweli uwe safarini hata siku tatu kisa tu wazazi wamesema? AshaDii i beg to differ with yu samahani mamii!
kwa kweli hili la huyu dada ni zaidi ya kwenda kujifungua ukweni!
sijui labda mie mimba zangu zinakuwa tofauti lakini kama ndo anakuwa na tumbo la kukata kona kama langu linavokuwa i see siendi kokote!
 
Last edited by a moderator:
is it so very important?
jamani mimba miezi 9,imagine na hiyo miguu inavokua kweli uwe safarini hata siku tatu kisa tu wazazi wamesema? AshaDii i beg to differ with yu samahani mamii!
kwa kweli hili la huyu dada ni zaidi ya kwenda kujifungua ukweni!
sijui labda mie mimba zangu zinakuwa tofauti lakini kama ndo anakuwa na tumbo la kukata kona kama langu linavokuwa i see siendi kokote!

Snowhite... unaweza kuwa sawa... Majibu yangu yamezingatia haya:-



  1. Tumetofautiana makabila... Kuna makabila ni marufuku kutoa mimba ama kuzaa mtoto wa kwanza nje ya nyumbani kwao. Nina mfano hai, binamu yangu aliolewa (mume wake alifariki may he rest in peace); mume wake alimwambia akazalie kwao... Binamu yangu ni mbishi... aligoma. Mimba ilipitiliza miezi 10 anaumwa uchungu anapona but hazai... Mashangazi wakachekecha wakaingilia kati na kumbwambia binamu aende kijijini. Of course alipofika tu kituoni uchungu ulimuanza na alipoingia tu ndani mule alizaa pale pale! Ki science tunaweza sema safari ilikuwa ndefu saana akachoka na ndio maana akazaa... Ki imani tunaweza sema upande wa kiume walimfunga kutozaa... Lipi ni kweli? Mimi na wewe hatujui.
  2. Lingine la msingi ni kuwa mshewa2 kaliwasilisha hapa tatizo lake... BUT yeye ndie anamface mume wake. Hatujui the nature ya mume wake ipo vipi. Inaweza kuwa moja ya wale wanaume ambao sio waelewa, kama kaamua ndio hilo hilo. Nimeona nikishikilia kwua dada akatae maamuzi ya mumewe SIO mumewe anaeteseka... Mshewa ndio anateseka zaidi. Akikubaliana katika nafsi yake kuwa anaweza enda itamfanya arudi hali nzuri na mood nzuri... Najua for personally nikiwa mjamzito SIPENDI wala SITAKI maudhi... Badala ya kumpa hiyo vita ya kupigana (kimaneno na mumewe) basi aangalie unafuu wa kuweza kubaliana na hilo.
  3. Mleta mada kisha onesha upande wake na ni wazi kuwa HATAKI! Nam support... BUT kutazama reality ni muhimu pia. Kuwa anaweza asitake lakini apende asipende lazima aende. Kama umenisoma vema nimempa options mbili... Aidha aende ma muuguzi AMA aombe mtu mzima kuwakilisha kuwa asubiri kujifungua.
 
Last edited by a moderator:
Snowhite... unaweza kuwa sawa... Majibu yangu yamezingatia haya:-



  1. Tumetofautiana makabila... Kuna makabila ni marufuku kutoa mimba ama kuzaa mtoto wa kwanza nje ya nyumbani kwao. Nina mfano hai, binamu yangu aliolewa (mume wake alifariki may he rest in peace); mume wake alimwambia akazalie kwao... Binamu yangu ni mbishi... aligoma. Mimba ilipitiliza miezi 10 anaumwa uchungu anapona but hazai... Mashangazi wakachekecha wakaingilia kati na kumbwambia binamu aende kijijini. Of course alipofika tu kituoni uchungu ulimuanza na alipoingia tu ndani mule alizaa pale pale! Ki science tunaweza sema safari ilikuwa ndefu saana akachoka na ndio maana akazaa... Ki imani tunaweza sema upande wa kiume walimfunga kutozaa... Lipi ni kweli? Mimi na wewe hatujui.
  2. Lingine la msingi ni kuwa mshewa2 kaliwasilisha hapa tatizo lake... BUT yeye ndie anamface mume wake. Hatujui the nature ya mume wake ipo vipi. Inaweza kuwa moja ya wale wanaume ambao sio waelewa, kama kaamua ndio hilo hilo. Nimeona nikishikilia kwua dada akatae maamuzi ya mumewe SIO mumewe anaeteseka... Mshewa ndio anateseka zaidi. Akikubaliana katika nafsi yake kuwa anaweza enda itamfanya arudi hali nzuri na mood nzuri... Najua for personally nikiwa mjamzito SIPENDI wala SITAKI maudhi... Badala ya kumpa hiyo vita ya kupigana (kimaneno na mumewe) basi aangalie unafuu wa kuweza kubaliana na hilo.
  3. Mleta mada kisha onesha upande wake na ni wazi kuwa HATAKI! Nam support... BUT kutazama reality ni muhimu pia. Kuwa anaweza asitake lakini apende asipende lazima aende. Kama umenisoma vema nimempa options mbili... Aidha aende ma muuguzi AMA aombe mtu mzima kuwakilisha kuwa asubiri kujifungua.
yaah!nakuelewa mamii
ila jamani mila nyingine hizi loh!
ndo mana nikasema pengine sio swala la kujifunguaa tu!ni zaidi ya hapo!
 
mshewa2, Hongera saana kuwa kukaribia kuwa mama na kwa kubeba ujauzito hadi hapo ulipofikia.

Haya mambo ni mtihani saana. Hii inakuonesha kuwa ndoa sio ya watu wawili ni zaidi ya hapo. Naamini kuwa hadi umelileta hapa umejaribu kwa kila namna kumsomesha na kumuelewesha mumeo na hajakuelewa… Pole saana. Kwa condition ya uja uzito uliyo nayo bahati mbaya ama nzuri una emotions zaidi ya siku zote… Ila nakuomba vuta subira, jitahidi rudisha moyo na akili yako chini na uliangalie upya.

Kwa mtazamo wangu ni kuwa mumeo hakuwa na shida wewe kujifungulia ulipo sasa (yaani nyumbani kwenu); itakuwa nyumbani kwa wakwe zako wamesikia kuwa karibu unajifungua wakati wowote na wamemsisitiza mumeo kuwa ukazalie nyumbani kwao. Yeye kuomba hilo sio mbaya; mbaya ni kuwa hakukuarifu mapema kwani ilitakiwa uende hata mwezi mmoja kabla.

Nashauri ukubaliane nae… Sababu kujifungua huyo mtoto na hali wazazi wana vinyongo haitapendeza. Kama nilivyosema ni mtihani mkubwa aidha mwambie mumeo akubali kukodi mtu wa afya ya uzazi muambatane naye safari hadi nyumbani - USITHUBUTU kukubali mkawa wawili tu. AMA omba mtu mzima yeyote ambaye ni upande wa mumeo na ni karibu na familia ya upande wa mumeo na ueleze hali halisi… Na umuombe akufikishie hizo salamu kwa wakwe ukiahidi kuwa baada tu ya kujifungua salama utaenda huko nyumbani baada ya siku saba.

Hai mati kitu gani utachagua najua kwua lolote lile litakuumiza sababu mumeo hajatanguliza welfare yako na mtoto. Ila ndio hivo, hapa ni mwanzo taratibu mtasomana na kujuana na kujifunza namna ya kuchukuliana. Kila la kheri… Na Mwenyezi Mungu muweza akuwekee wepesi katika ujauzito hadi kujifungua. Pamoja Saana.
Asante sana kwa ushauri wako ntaufanyia kazi,
 
Hongera sana kwa ujauzito!


Nisingekushauri usafiri kwa wakati huu, umeshachelewa. Mtoto wangu wa kwanza alikuja siku kumi kabla ya due date.
Naomba kuuliza, mbona mmechelewa kuamua hivo? kwa sababu za kiafya na usalama wako , na kiumbe chako nafikiri ingekuwa viZuri ubaki nyumbani.safari siku 3 ni nyingi mno kwa mama mjamzito!! utachoka, utaumia, na unaweza ukajifungulia njiani ambayo ni hatari sana. Inabidi upumzike ili uwe na nguvu muda wa kujifungua. hii ni mila mnayofuata? Mama mkwe hawezi kuja nyumbani kwenu? inabidi uangalie risks vs benefits. Kwa sasa naona risks ni kubwa sana. Maisha yako na ya mtoto yatakuwa hatarini.




Habari Wana JF

Mimi Nina mimba ya Miezi 9 nimebakisha week mbili nijifungue ila mume wangu analazimishia niende nikajifungulie huko kwao kanda ya ziwa, I thought of flying ila flights haziruhusu mtu wa type yangu kupanda ndege,so anasema tutaenda na gari taratibu hadi tufike even if it take us 3 days, Hospital nimeambiwa nisisafiri coz niko karibia kujifungua,he doesnt want to understand he think I'm jus making it coz I'm a medical personel 2, Hataki hata twende kwa specialist wote,wala hajawahi kwenda na mimi clinic,its our first born ,
Nifanyeje?nisafiri tu. kuwaridhisha ila its risk...anataka tusafiri 20th my due date ni 28th
 
kama alikuambia mapema nawe ukadharau huna ujanja kodini tu huyo wa afya tena mkunga mtu muende hata wiki asemayo mmeo njiani maana mambo ya wakwe tena kwenye ndoa ni balaa,
usipuuze kutokwendaz unles wakwe wameridhjia baada ya kuongea nao hasara za wewe kusafiri na hali yako,
na wakigoma pia nenda na uwe umeclear all posible risk kama kusafiri na huyo mtu atakyetoa msaada kiafya anything can hapen njiani
 
pole kwa mtihan dadangu ila we jaribu kumckiliza mumeo anachosema acje akasema huwapend ndugu zk we mkabiz mungu naiman utaenda salama na utarudi salama.
 
kama alikuambia mapema nawe ukadharau huna ujanja kodini tu huyo wa afya tena mkunga mtu muende hata wiki asemayo mmeo njiani maana mambo ya wakwe tena kwenye ndoa ni balaa,
usipuuze kutokwendaz unles wakwe wameridhjia baada ya kuongea nao hasara za wewe kusafiri na hali yako,
na wakigoma pia nenda na uwe umeclear all posible risk kama kusafiri na huyo mtu atakyetoa msaada kiafya anything can hapen njiani

Sasa mamie kwa mfano ndo ningechukua leave mwezi kabla ipi nisafiri na maternity ni Miezi mitatu so after kujifungua ndo ningekuwa nimebakiwa na Miezi miwili tu ya kukaa na mtoto afu narudi kazini huoni hio nayo issue
 
haijalishi utazalia hapo au ukweni, jambo la msingi ni; mimba ya kwanza ni busara kuzalia hospitalini.
Unaweza kusafiri. Hata ambulance ikikubeba tayari umesafiri.
 
Mimba za kwanza zina macomplication sana unaeza jiona sawa ila kumbe sio sawa...mm binafsi sikushauri uende.waambie wazingatie na afya yako omba sana Mungu na atakusaidia ujifungue salama baada ya wiki panda ndege nenda,kama swala ni kujifungulia kwao huyo mama mkwe kinachomshinda nn kuja ukijifungua unarudi nae...mueleze mume wako na kama anakupenda atakusikiliza kuna kufa wakati wa kuzaa kuna kupoteza mtoto...why riskin urself kiasi hicho.._kienda ni sawa na kujitoa mhanga aisee....ila akili kukichwa..
 
Haya mambo ya mila hua ni magumu sana, hapo itakua wanataka kitovu cha mtoto na mambo mengine kama hayo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom