Nina milioni 45, nifanye biashara ipi kati ya hizi?

Mkuu umetoa hoja nzuri mimi nakushauri kwa alternative zifuatazo za uwekezaji tumia moja au zaidi ya moja

1. Unaweza tenga million kumi kwa ajili ya biashara lakini milioni thelasini na tano kaweke kwenye treasury bond yaani dhamana za serikari, fuatilia rate BOT utaamua uweke za muda gani miaka mitano,au kumi,au kumi na tano au ishirini, ingawa mimi napendekeza za miaka ishirini. Itakufanya uwe na kipato cha uhakika wakati unatumia milioni kumi kufanya biashara nyingine ambayo ni scalable.

2.Tafuta mfanyabiashara anayenua au kuprocess mazao ya biashara, muombe awe menthor wako au mshirikiane, hapa usihofu wapo wengi Songea au Ifakakara wana mashine na godown , tumia millioni 30 nunua mazoa mwezi wa saba au wa nane hifadhi kwenye magodown yao kwa kawaida atakayenunua atasaga au kukoboa kwao uza kuanzia November.

Usitumie 15 M iloyobaki, mwakani (2021) baada ya kujifunza tafuta washirika wawili ata mimi naweza kukutafutia wachangie kiasi kama hicho unaweza nunua na kuistall mashine za kukoboa mpunga Ifakara au kusaga unga Songea inategemea utakapopenda ku specializa, I prefer Songea. Then utakuwa unaprocess na kusafirisha kwenye masoko. Pia ukivutiwa na wazo hili awali unaweza kuamua kutembelea maeneo yenye bishara za vyakula kama Moro,Ifakara,Songea na baadhi ya wilaya za Mbeya ukaone watu wanavyofanya wakati sisi tunashinda jamiiforums. Usione tabu kutumia pesa kwa kusafiri ili upate business information na kupata technical know

3. Fanya survey ya mikoa na maeneo ambayo eneo la kiwanja cha millioni kumi au kumi na mbili unaweza jenga apartment ya vyumba viwili na sitting na choo na jiko unaweza pangisha kwa laki mbili au zaidi.

Ukipata eneo jenga apartment tatu au mbili with site plan inayoruhusu expansion kwenye kiwanja kimoja. Hapa for cost efficient apartment mbili itokane na design ya nyumba moja yaani huyu mbele mwengine nyuma, zinashare baadhi ya vitu kama ukuta ma mabomba ya majo.

Idea hii ni ngumu kwa dar kwa kuwa viwanja vya million kumi ni pembeni saana ila miki kama Moshi, Tanga,Mtwara,Lindi,Mbeya,Shinyanga,Tabora,n.k unaweza fanikiwa.

All the best

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapa ushauri namba 3 ndio wenye uhakika.
Hizo zingine ni pata potea,ingawa hiyo namba 1 pia ni nzuri ila inawafaa watu wenye sources nyingi za income ili awe na uwezo wa kuvumilia hiyo miaka mingi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hongera kwa mawazo mazuri...lakini kwa maisha ya sasa kuna biashara itakubidi uzizike!...things changed alot!..hizi mishe za real estate sidhan kama kwa hapa kwetu zinalipa tena! Au mie sielewi!
Kwwmba ajenge nyumba kwa mfano atumie 50m..then apangishe kila mwezk kwa 300k!...wakati kuna biashara nyingine zinazolipa zaidi!!... Au mie nafikiri kinyume nyume!...
Uko sahihi mkuu ila inategemea unawaza kwenye level gani.
Kwa mtu mwenye experience kubwa ya biashara na ana cash flow nzuri hatoona umuhimu wa kutumia milioni 50 ili kujenga nyumba ya kupokea 300k kila mwezi.
Lakini kwa mtu asiye na uzoefu wa biashara na anataka kupata uhakika wa pesa ya kujikimu kila mwezi kujenga nyumba ya kupangisha is the best option.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu ukiwa na kiwanja na good site plan 50 unajenga apartment tatu za vyumba viwili na sitting room utakazopangisha laki mbili au zaidi kila moja.

Nikwambie kitu mkuu mimi najua real estate haina return ya haraka sana lakini my ideas is

i. Jifunze maarifa ya biashara na jinsi ya kufanya kazi

ii. Ukipata nafasi wekeza kwenye biashara na nunua kiwanja kwenye potential area.

iii.Ukipata nafasi tanua biashara na jenga nyumba ndogo kwani nyumba kubwa zinatumia pesa nyingi ambazo hazirudi kwa kodi, lakini ndogo ni nora pia nyumba unapokwama kwenye maisha ndio kitu pekee kwenye maisha kitakacjokustiri fall back, BTW nyumba is long term investmest ambayo inaongezeka value in term of year.

Iv. Ukiwa una nyumba ata moja hasa sehemu unayotarajia kuishi maisha yako wewe focus kwenye biashara tuu ukipenda nunua kiwanja kiache tuu

Usipokuwa makini pesa zote zinaweza kuisha kabisa ukiwa huna pa kulala

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu nakusapoti kwa asilimia .
Kwa kipindi Cha Sasa I don't agree on any other kind of business rather than this real estate.
Nikibadilisha Sana labda ya kuuza duka la vifaa vya ujenzi ndio at least naikubali kwa vile bidhaa zake haziozi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
True real estates ni kama life backup maana hatuna garantii ya kesho yetu hasa ukwamapo kimaisha uongo familia haifi njaa hata mtu akili utulia wakati ukisaka miundombinu mingine unamwachia wife aangalie familia kupitia houses
Wewe una akili nyingi Sana.
Walio wengi wanarubuniwa na biashara ya kwenye makaratasi na kuaminishana utajiri fake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu...chukua pesa kidogo ufanye duka la bidhaa za chakula jumla na rejareja...utumie kipindi hicho kufatilia biashara nyingine utakayoweka mtaji mkubwa....45m kwenye baadhi biashara unazoshauriwa hapa bado ni mtaji mdogo sana...ukizingatia hapo hujatoa gharama za frem na pesa ya tahadhali....kumbuka inachukua muda kuona faida halisi ya biashara mpaka miaka miwili au zaidi...pia ushindani ni mkubwa sana...wewe unanunua kariakoo ...mshindani anaagiza nje....kupata mtaji ni kazi ngumu...lakini kuukuza mtaji ndio shughuri pevu zaidi.
 
Vipi hii idea Katika 45 toa 20 nunua site 25 jenga frem 10 zipangishe 7 kisha 3 zifungue business moja ya hardware,pili spea za pikipiki tatu duka la nafaka baada ya miezi 3 kalikopee bank hilo eneo 40m mpe muhindi akupe tata mpya ya mkataba tafuta ruti dume za nje ya mji zinazolaza 250000 kwa siku upate kulipa bank na kwa muhindi yaaani uchukue risk kubwa (unabet maisha) hasara roho potelea mbali.Hapo vipi
 
Wazo nalo 35 muhindi,10 navuta poweriller hp 10 plus waterpump,mipira,na sprinkler zake 5 hivi zile raingun zitupazo maji upana mita 50 kwa degree 360 nikalima nyanya,vitunguu,kabechi,bamia,viazi napeleka sokoni huku tata nimelikatia bima kubwa linapiga ruti ya nje ya mji yaani asubui nachukua hesabu kabla alijaondoka likiondoka linarudi kesho Mchana navuta tena hesabu naziweka fixed kwa mwaka mzima nachanga za tata na za shamba sitotoboa kweli?
Una mawazo mazuri sana mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi hii idea Katika 45 toa 20 nunua site 25 jenga frem 10 zipangishe 7 kisha 3 zifungue business moja ya hardware,pili spea za pikipiki tatu duka la nafaka baada ya miezi 3 kalikopee bank hilo eneo 40m mpe muhindi akupe tata mpya ya mkataba tafuta ruti dume za nje ya mji zinazolaza 250000 kwa siku upate kulipa bank na kwa muhindi yaaani uchukue risk kubwa (unabet maisha) hasara roho potelea mbali.Hapo vipi
Sound good too

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimecheka sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndio ukweli huo!! Mimi kuna jamaa yangu nilimpa onyo hilo, hakusikia, akajifanya ni afisa mwandamizi wa TBS!! nilitaka kumuunganisha na mtaalam wa kupekecha mpunga kwa mikono, yeye akiuuona tu anaupekecha, anakwambia huu sawa, na kwelii mule mule!! Akakataa, akajikuta ananunua biliani tupu!! Halafu ujazo mdogo alikula hasara kubwa!! Kule hata ndoo za kupimia ni tofauti, ulishawahi kusikia ndoo tupu ya lita 20,inauzwa laki 2?!!!
 
Hii biashara ya mazao hususani mpunga inahitaji umakini sana kwani unanunua kitu ambacho kiko kwenye maganda!!na bei zake huwa hazitabiriki sana!!bora hata ya mchele
Kununua mpunga kama sio mzoefu acha kabisa narudia tena kama wewe sio mzoefu na hauna MTU mzoefu kwenye hii biashara ya mpunga acha kabisa utakuja kuuziwa pumba badala ya mpunga nimeongea kwa uzoefu wangu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu hongera kwanza. Biashara zote hizo pasua kichwa. Nunua mpunga weka s tore. Mfano mpunga wakati wa kiangazi huwa ni kati ya elf 30 hadi 36 kwa ginia hapo ni july uweke store hado october hadi april then uuzekati ya miezi hiyo bei ya gunia la mpunga hupanda hadi elf 90. Nafikiri faida shilingi itazaa shilingi

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmh,shambani tu wakati wa mavuno sio bei hiyo mkuu!uliza vzr !

BTW,ukinunua huo mwezi wa ,5,6,7....uweke mpk Nov,dec, Jan,Feb,march,April.....ndo bei huwa inakua juu,baada ya hapo inashuka tena mavuno yanakua yameanza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom