Nina milioni 20. Nahitaji kufanya biashara ya spare za pikipiki kwa jumla na rejareja

Premij canoon

JF-Expert Member
May 27, 2018
1,115
2,490
Salaam wanajukwaa,

Pole na mitikasi na mihangaiko ya kila siku, natumai sote ni wazima wa afya njema. Kama kichwa cha habari kinavyojieleza, katika uhangaikaji nimefanikiwa kufikisha kiasi cha milioni ishirini (20,000,000), nahitaji kufanya biashara ya spare za pikipiki kwa jumla na reja reja nipo nje kidogo ya Dar mkoa wa Pwani (Bagamoyo)

Naomba ushauri kwa wazoefu wa hii biashara... Je, milioni 20 itaweza kujitosheleza? Ikiwa ni pamoja na kwenda China, kununua mzigo, kuusafirisha hadi kufika TZ.

Kwa taarifa za awali nilizopata ni kwamba:

• Nauli GO & RETURN makadirio ya juu $1800 (Inaweza kupungua).
• Chakula & Malazi $35 per day. Nitatumia siku 3 tu kununua mzigo nakuukabidhi kwa kampuni ya usafirishaji kisha kurudi TZ ili kuepuka kupunguza mtaji kwa gharama kubwa za chakula & malazi! Hivyo $35 kwa siku 3 itakua $105 (Tsh 250,000)

Naomba kwa wazoefu kunisaidia mawazo na ushauri kwa huu mtaji wangu je, utajitosheleza kwenye biashara tajwa? kwa kuuza jumla na rejareja?

NB: Nafahamu kuna corona kwa sasa, hivyo nipo hapa kupata ushauri na kupata taarifa muhimu kwa sasa, hali itakapotulia ndipo natarajia kwenda.

NATANGULIZA SHUKRAN

1619425975494.png

 
Premij canoon,

Mkuu sina uzoefu na biashara hiyo ila kwa mtazamo wangu hiyo pesa ni nyingi lakini sio ya kuanzia China,ingetosha sana kama tayari ungekuwa umeshaanza biashara,kama unaanza ningekushauri uanzie Kuchukulia Dar tena kwa mtaji wa milioni 5 hapo ndio utapata uzoefu nini kinatoka zaidi na nini hakitoki zaidi.

Hapo ndio utapata taswira kamali nini ununue ukienda ,biashara sio mtaji pekee,biashara inahitaji maarifa zaidi!,kwani mimi nauza simu used ni mjinga?natumia fursa ya wapenda kitonga.


Sent using IPhone X
 
Sio rahisi kihivyo mkuu. Anza kununua mizigo kariakoo kisha uuze hapo kwako ili uone biashara ikoje. Tengeneza urafiki na angalau wafanyabiashara wa spare watano wa jumla wa kariakoo wakuelezee jinsi biashara wanavyofanya. Wakuelezee gharama zote, spare zipi zinahitajika sana na mbinu za kutoa mzigo bandarini.


Pia kwenye ofisi yako weka mafundi
 
Milioni ishirini Kwa vifaa vya pikipiki Anza kuuza rejareja Kwa kununua mzigo kariakoo, Kwa kufungua gereji ya pikipiki pamoja na Duka la spare mwenyewe ni sehemu nategemea kuwekeza, Ila Kwa 20m kama huna eneo na ni biashara mpya wekeza kwenye rejareja Kwanza Huku ukiwa na mafundi wako hapo ofisini

Yaani unamaanisha niende kariakoo ninunue mzigo wa milioni 20 mkuu? Mbona kama namtajirisha muuza duka kwa mkupuo?

Mimi ninachotaka kujua ni je, hii mil 20 itaniwezesha kwenda china kuchukua mzigo, kuusafirisha hadi TZ? Na si kupata uzoefu wa kipi kinaenda kipi hakiendi, mimi nijue tuu bajeti yangu hii inanitosha au laa

Maana naona kuchukua mzigo wa mil 20 kariakoo kama uwoga wa kuthubutu hivi

Ila shukraan kwq ushauri wako mkuu, tusubiri wengine waje.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mkuu sina uzoefu na biashara hiyo ila kwa mtazamo wangu hiyo pesa ni nyingi lakini sio ya kuanzia China,ingetosha sana kama tayari ungekuwa umeshaanza biashara,kama unaanza ningekushauri uanzie Kuchukulia Dar tena kwa mtaji wa milioni 5 hapo ndio utapata uzoefu nini kinatoka zaidi na nini hakitoki zaidi hapo ndio utapata taswira kamali nini ununue ukienda ,biashara sio mtaji pekee,biashara inahitaji maarifa zaidi!,kwani mimi nauza simu used ni mjinga?natumia fursa ya wapenda kitonga


Sent using IPhone X

Ahsante kwa mawazo yako mkuu, Inaonesha ni mtazamo chanya wenye maono ya mbali..

Kuhusu uzoefu wa kipi kinaenda sana ili ninunue vingi na kipi hakiendi sana ili ninunue vichache hili nitalifanyia kazi huku huku mtaani.

Ingependeza sana akatokea member anaefanya biashara kwa kwenda china akasema... " Bwana mdogo.. kwa mtaji wako nunua bidhaa za kiasi fulani, kisha usafiri utacheza kwa wastani wa kiasi fulani hadi fulani, inayobaki iweke akiba kwa ajili ya ishu fulani.

Maelezo hayo yatanipa mwanga saana... Kuhusu kuuza jumla au rejareja ni mimi sasa niangalie uwingi wa mzigo wangu niuzaje..

Mkuu ahsante kwa kutoa mawazo yako.

KUDOS





Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Sio rahisi kihivyo mkuu. Anza kununua mizigo kariakoo kisha uuze hapo kwako ili uone biashara ikoje. Tengeneza urafiki na angalau wafanyabiashara wa spare watano wa jumla wa kariakoo wakuelezee jinsi biashara wanavyofanya. Wakuelezee gharama zote, spare zipi zinahitajika sana na mbinu za kutoa mzigo bandarini.


Pia kwenye ofisi yako weka mafundi

Ahsante mkuu... Hili la mafundi nalifahamu, na nitalifanyia kazi. Ila kuhusu kutoa mzigo bandarini naskia sasaivi kuna makampuni ya usafirishaji na yanatoa hadi mzigo bandarini, wewe unaenda tu kwenye ifisi zao kuchukua mzigo wako.
 
Premij canoon

Mkuu 20m ni sawasawa na takribani $9000. Ukienda china huwezi kujaza container ya 40ft au 20ft hata nusu yake manaake unataka ulete loosed cargo.

ambayo hujui utapata lini mtu wa kukuwekea kwenye behewa lake, hapo hujajua TRA wanakulipisha kiasi gani shiping cost hujui paka Dar, na lini utapokea huo mzigo .

Kwa ukweli hiyo pesa ninyingi kwa wakati hu ila kwa biashara ya china hususani spare za piki piki ni peanuts utakimbia mwenyewe huna connection yoyote ya ma clearing agents au TRA, husioni tu watu wanafanya biashara sio rahisi kama unavyo fikiria wako well connected wanatembeza pesa huo mtaji wako unakufa siku ya kwanza. unaenda kupambana na wafanya biashara wakubwa sana ingia kwanza ndo utaelewa biashara ya Bongo iko je.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu 20m ni sawasawa na takribani $9000. Ukienda china huwezi kujaza container ya 40ft au 20ft hata nusu yake manaake unataka ulete loosed cargo.

ambayo hujui utapata lini mtu wa kukuwekea kwenye behewa lake, hapo hujajua TRA wanakulipisha kiasi gani shiping cost hujui paka Dar, na lini utapokea huo mzigo .

Kwa ukweli hiyo pesa ninyingi kwa wakati hu ila kwa biashara ya china hususani spare za piki piki ni peanuts utakimbia mwenyewe huna connection
yoyote ya ma clearing agents au TRA, husioni tu watu wanafanya biashara sio rahisi kama unavyo fikiria wako well connected wanatembeza pesa huo mtaji wako unakufa siku ya kwanza. unaenda kupambana na wafanya biashara wakubwa sana ingia kwanza ndo utaelewa biashara ya Bongo iko je.

Sent using Jamii Forums mobile app
Duu 20M sawa na Peanuts.

Portfolio | 2020
 
Premij canoon

Tajiri mtarajiwa,
Hicho ni kiwango kilicho na makadirio yenye mafanikio.
Uwe mjuaji hasa na elimu utakayoweza kujiongoza bila mpambe sababu ugenini maamuzi yanahitaji kisomo vinginevyo uwe na mpambe na at least ficha m 10 nyingine kibindoni. Siku hizo biashara ni changa moto.
Ukiwasemaji mzuri sample nyingi utapewa Bure zitakufidia gharama.
 
Ok ,umepata eneo ambalo utaweza kufanya na service za pik pik?

Unaweza kwenda china cha kufanya usingojee hesabu za jf ww nenda kwa wauza spare ongea nao hata wa5 tofaut tofaut kwa muda wako utapata details nzuri zaid ila usiingiza 20 mil yote ingiza tu 10-12 mil basi
Eneo lipo, nimeshapata tayari.


Sent from my iPhone using JamiiForums

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duu 20M sawa na Peanuts.

Portfolio | 2020
Mkuu ni kweli watu wana mitaji ya zaidi $100,000 ila wanashinda pale TRA zaidi ya wiki kubembeleza maofisa wa TRA ku clear container zao bila figisufigisu na kubabikizwa ma kodi, ya ajabu hasikudanganyi ntu eti rushwa elisha isha TRA, hiyo 20m haitoshi hata kuhonga ma ofisa wa TRA kutowa container 40ft ilio sheheni vipuri vya pikipiki, aanza biashara hiyo ndo utajua hi Tz inawenyewe wengine ni wasidikizaji wa wenye nchi..........

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom