Mashindanolivinus
Member
- Dec 10, 2016
- 27
- 22
Ndugu zanguni,
Hili jambo la kupotea kwa Ndg. Ben Saanane, kwa sasa huenda ndiyo Drama Kali zaidi Kisiasa na Kiusalama. Kwa binadamu yeyote lazima linapotokea jambo lisilo la kawaida kama hili ni lazima ajiulize maswali mengi kuwa inawezekana ni hivi au ni vile.
Katika kadhia hii, kuendana na mijadala inayoendelea kwenye majukwaa mbalimbali watoa maoni wanaonekana kuamini kati ya mawili. Ben kutekwa na vyombo vya serikali kwa ajili ya 'kumshikisha adabu' au kutoa onyo kwa wakosoaji wengine au Ben kufichwa na Viongozi wa taasisi anayofanyia kazi ya CHADEMA kwa ajili ya kuionyesha dunia kuwa Serikali haitaki kukosolewa. Kwa maana ya kuipakazia serikali imemteka, lakini katika maudhui hiyo ya pili wapo wanaofikiri kuwa huenda alitofautiana na viongozi wake wakaamua kumfanyia 'Umafia'.
Dhania zote hizi zinaibuka kwa sababu tulio wengi hatujui kabisa ukweli wa jambo hili ukiacha waandaaji na watekelezaji wa jambo lenyewe, na Mungu aonaye sirini. Na huwezi kumzuia binadamu kuwaza sana sana aamue tu kutokuyatoa hadharani mawazo yake.
Katika kila kundi la dhania hapo juu ni lazima mtu yeyote wa kizazi cha kuhoji ajiulize maswali mengi kabla ya kuipa dhana yake asilimia kubwa zaidi ya nyingine.
Mimi nimepembua na kuchanganua na kujikuta nashawishika kuamini kuwa kupotea kwa Ndugu yetu Ben Saanane ndiyo haswa Operesheni UKUTA ambayo siku Mwenyekiti anatangaza kuiahirisha alisema itafanyika kivingine.
Nimejiuliza yafuatayo:
1. Kwa nini Ben!?
Je, Ben ndiye mtoa Kashfa na mkosoaji wa serikali kuliko wengine!? Mbona wengine walifunguliwa mashtaka ya makosa ya Mtandao!?
2. Kwa nini CHADEMA wanatumia nguvu kubwa ya kutaka kuuaminisha Umma kuwa Serikali imehusika na jambo hili badala ya kushirikiana na vyombo vya usalama kufanya uchunguzi?
3. Kwa nini Mwajiri wake amekuwa na kigugumizi kuzungumzia sakata hili!?
4. Kama Taasisi hii hii iliweza kutengeneza mikakati ya kuwateka watu na kuwapa mateso makali kwa vile tu walitishia maslahi yao, watashindwaje kwa Ben!?
5. Hotuba ya Ndugu Mwenyekiti Mbowe huko ughaibuni aliyeelezea kuwa alilengwa na maguruneti na serikali ili atolewe uhai lakini watu waliompenda wakaamua kuwa ngao ili wafe badala yake.. (hotuba ile ilinishawishi nitamani kujua hatima ya uchunguzi wa ni nani aliyelipua lile bomu kule Arusha) nimejiuliza hili la Ben haliwezi kuwa ni maandalizi ya hotuba nyingine ughaibuni!?
Haya pamoja na mengine mengi yanayonizunguka kichwani yananishawishi niamini kuwa hii ndiyo operesheni UKUTA vol. 2, naomba kwa Mungu vyoyote iwavyo kijana huyu aliyetumika kama Starring kwenye Tamthiliya hii amalize salama, na arejee kuungana tena na familia yake, ndugu na marafiki zake katika kuchangia ujenzi wa nchi yake!!
Wakatabahu
Hili jambo la kupotea kwa Ndg. Ben Saanane, kwa sasa huenda ndiyo Drama Kali zaidi Kisiasa na Kiusalama. Kwa binadamu yeyote lazima linapotokea jambo lisilo la kawaida kama hili ni lazima ajiulize maswali mengi kuwa inawezekana ni hivi au ni vile.
Katika kadhia hii, kuendana na mijadala inayoendelea kwenye majukwaa mbalimbali watoa maoni wanaonekana kuamini kati ya mawili. Ben kutekwa na vyombo vya serikali kwa ajili ya 'kumshikisha adabu' au kutoa onyo kwa wakosoaji wengine au Ben kufichwa na Viongozi wa taasisi anayofanyia kazi ya CHADEMA kwa ajili ya kuionyesha dunia kuwa Serikali haitaki kukosolewa. Kwa maana ya kuipakazia serikali imemteka, lakini katika maudhui hiyo ya pili wapo wanaofikiri kuwa huenda alitofautiana na viongozi wake wakaamua kumfanyia 'Umafia'.
Dhania zote hizi zinaibuka kwa sababu tulio wengi hatujui kabisa ukweli wa jambo hili ukiacha waandaaji na watekelezaji wa jambo lenyewe, na Mungu aonaye sirini. Na huwezi kumzuia binadamu kuwaza sana sana aamue tu kutokuyatoa hadharani mawazo yake.
Katika kila kundi la dhania hapo juu ni lazima mtu yeyote wa kizazi cha kuhoji ajiulize maswali mengi kabla ya kuipa dhana yake asilimia kubwa zaidi ya nyingine.
Mimi nimepembua na kuchanganua na kujikuta nashawishika kuamini kuwa kupotea kwa Ndugu yetu Ben Saanane ndiyo haswa Operesheni UKUTA ambayo siku Mwenyekiti anatangaza kuiahirisha alisema itafanyika kivingine.
Nimejiuliza yafuatayo:
1. Kwa nini Ben!?
Je, Ben ndiye mtoa Kashfa na mkosoaji wa serikali kuliko wengine!? Mbona wengine walifunguliwa mashtaka ya makosa ya Mtandao!?
2. Kwa nini CHADEMA wanatumia nguvu kubwa ya kutaka kuuaminisha Umma kuwa Serikali imehusika na jambo hili badala ya kushirikiana na vyombo vya usalama kufanya uchunguzi?
3. Kwa nini Mwajiri wake amekuwa na kigugumizi kuzungumzia sakata hili!?
4. Kama Taasisi hii hii iliweza kutengeneza mikakati ya kuwateka watu na kuwapa mateso makali kwa vile tu walitishia maslahi yao, watashindwaje kwa Ben!?
5. Hotuba ya Ndugu Mwenyekiti Mbowe huko ughaibuni aliyeelezea kuwa alilengwa na maguruneti na serikali ili atolewe uhai lakini watu waliompenda wakaamua kuwa ngao ili wafe badala yake.. (hotuba ile ilinishawishi nitamani kujua hatima ya uchunguzi wa ni nani aliyelipua lile bomu kule Arusha) nimejiuliza hili la Ben haliwezi kuwa ni maandalizi ya hotuba nyingine ughaibuni!?
Haya pamoja na mengine mengi yanayonizunguka kichwani yananishawishi niamini kuwa hii ndiyo operesheni UKUTA vol. 2, naomba kwa Mungu vyoyote iwavyo kijana huyu aliyetumika kama Starring kwenye Tamthiliya hii amalize salama, na arejee kuungana tena na familia yake, ndugu na marafiki zake katika kuchangia ujenzi wa nchi yake!!
Wakatabahu