Kwa wasomaji wa maandiko wanakumbuka tukio moja la Yesu kristo pale waandishi na mafarisayo walipomtuhumu kwamba imekuwaje Yeye kula na kujichanganya na wenye dhambi, wakiwemo watoza ushuru waliotuhumiwa kwa kula rushwa ( sawa na TRA hapa TZ. ila TRA sio wala rushwa). Yesu kristo aliwajibu kwamba waliowazima hawahitaji daktari.
Dr. Slaa amedai kwamba Chadema aliyoijenga ni ya waadilifu. Kwa maana hiyo, kwa falsafa ya Yesu kristo, Dr. Slaa alipasa kumpokea Edward Lowassa na kisha amwadilishe. Tofauti na mafundisho ya kanisa katoliki, Dr. Slaa anawakimbia wenye dhambi kisha anasimama majukwaani akiwatuhumu wenye dhambi hao.
Aidha, Dr. Slaa ameonesha kuwa mwongo kabisa. Amehusisha suala la ubomomoaji wa mabucha ya nguruwe na uvamizi wa polisi ndani ya msikiti wa Mwembechai (1999) na Mh. Sumaye. Kwa kumbukumbu zangu,(niko tayari kusahihishwa) miaka ile Rais wa Tanzania alikuwa Mzee Mwinyi na kipindi hicho Mh. Sumaye hakuwa Waziri Mkuu.
Lakini pia, kitendo cha Dr. Slaa kuingiza udini katika hoja zake pale Serena Hotel juzi, hakutumia hekima. Ameongea kwamba eti wachungaji na maaskofu 30 wamehongwa na Mh. Lowassa; akaenda mbali zaidi akisema eti hata kanisa la KKKT liko nyuma ya Lowassa. Kauli hizi ni hatari mno, hazipaswi kuachwa pasipo kukemewa.
Yamkini, labda, ni mkakati wa makusudi kutumia dini ili kumbomoa Mh. Lowassa kwa maana siku tatu kabla ya Dr. Slaa kujitokeza pale Serena Hotel, ndugu Mpanju naye alisikika huko mkoani Njombe akimnadi mgombea urais wa CCM; akisema Masheikh wa Zanzibar ambao wako mahabusu Segerea walihusika na mauaji ya Padri kule Zanzibar lakini pia akasema eti masheikh hao walihusika na uchomaji wa makanisa kule Mbagala.
Kauli za jinsi hii, kama hiyo ya ndugu Mpanju, haikustahili kusemwa kwa kuwa kesi ya masheikh hao ingali mahakamani na ni mahakama ambayo inaweza kuthibitisha uhusika wa masheikh hao na tuhuma hizo juu yao.
Tuongee yote majukwaani lakini tuchunge ndimi zetu. Hata kama tumedhamiria kwa dhati kuwafurahisha mabwana zetu, kwa kusema kile tudhaniacho kina (kita) wapendeza na kuwafurahisha; tusiingize kauli zinazoweza chochea uvunjifu wa amani kiimani.
Dr. Slaa amedai kwamba Chadema aliyoijenga ni ya waadilifu. Kwa maana hiyo, kwa falsafa ya Yesu kristo, Dr. Slaa alipasa kumpokea Edward Lowassa na kisha amwadilishe. Tofauti na mafundisho ya kanisa katoliki, Dr. Slaa anawakimbia wenye dhambi kisha anasimama majukwaani akiwatuhumu wenye dhambi hao.
Aidha, Dr. Slaa ameonesha kuwa mwongo kabisa. Amehusisha suala la ubomomoaji wa mabucha ya nguruwe na uvamizi wa polisi ndani ya msikiti wa Mwembechai (1999) na Mh. Sumaye. Kwa kumbukumbu zangu,(niko tayari kusahihishwa) miaka ile Rais wa Tanzania alikuwa Mzee Mwinyi na kipindi hicho Mh. Sumaye hakuwa Waziri Mkuu.
Lakini pia, kitendo cha Dr. Slaa kuingiza udini katika hoja zake pale Serena Hotel juzi, hakutumia hekima. Ameongea kwamba eti wachungaji na maaskofu 30 wamehongwa na Mh. Lowassa; akaenda mbali zaidi akisema eti hata kanisa la KKKT liko nyuma ya Lowassa. Kauli hizi ni hatari mno, hazipaswi kuachwa pasipo kukemewa.
Yamkini, labda, ni mkakati wa makusudi kutumia dini ili kumbomoa Mh. Lowassa kwa maana siku tatu kabla ya Dr. Slaa kujitokeza pale Serena Hotel, ndugu Mpanju naye alisikika huko mkoani Njombe akimnadi mgombea urais wa CCM; akisema Masheikh wa Zanzibar ambao wako mahabusu Segerea walihusika na mauaji ya Padri kule Zanzibar lakini pia akasema eti masheikh hao walihusika na uchomaji wa makanisa kule Mbagala.
Kauli za jinsi hii, kama hiyo ya ndugu Mpanju, haikustahili kusemwa kwa kuwa kesi ya masheikh hao ingali mahakamani na ni mahakama ambayo inaweza kuthibitisha uhusika wa masheikh hao na tuhuma hizo juu yao.
Tuongee yote majukwaani lakini tuchunge ndimi zetu. Hata kama tumedhamiria kwa dhati kuwafurahisha mabwana zetu, kwa kusema kile tudhaniacho kina (kita) wapendeza na kuwafurahisha; tusiingize kauli zinazoweza chochea uvunjifu wa amani kiimani.