William Mshumbusi
JF-Expert Member
- Mar 27, 2012
- 1,657
- 2,252
1. Wakati akitoa ushahidi wake wote Mara kadhaa wakili aliyemuongoza alisita kuendelea kumuuliza na kuanza kuteta chini kwa chini ikionesha Kuna majibu Alitoa nje ya matarajio yao.
2. Kucheleweshwa ushaidi wake kwa siku moja ama kulikuwa na mashaka juu ya ushaidi wake kutoka kwa mawakili wa Serikali au yeye mwenyewe.
3. Amejaribu kutoa kauli za kumtetea Mbowe kuwa pesa alizotumiwa na Mbowe zilikuwa za nauli kwaajili ya kuifikisha walinzi kwa Mbowe na sio za kununua vifaa au vya Ugaidi au malipo ya kufanya Ugaidi.
4. Hoja ya Mbowe kuajiri makomando wanne tu kwaajili ya kukata miti ni kiloja kabisa. Kwamba ilihitaji kuwa na makomando ndio wakate miti.
5. Je, makomando wanne wanawezaje kukata miti na kuchoma vituo vya mafuta Tanzania nzima ni swali gumu kabisa kulielezea.
6. Je, mawakili wanaamini uchomaji vituo vya mafuta na kukata miti ungeweza kuvutia maandamano au kuwatia watu woga na kujifungia ndani? Kama vibomu vya machozi tu na milio ya riasasi watu hujifungia ndani milipuko ya vituo vingevutiaje watanzania kuandamana.
7. Tanzania ina makomando wangapi? Makomando hao wanne wangesaidia vipi Mbowe na elimu yake hao makomando wanne tu kusimamisha nchi isitawalike na kudhibiti makomando zaidi mia watiifu serikalini.
8. Urio lazima aoneshe baada ya kile alichopanga baada ya kuchomà vituo ni vipi Mbowe angepewa nchi na
sio Wanajeshi kuchukua nchi.
9. Je, Urio hajaonesha chochote ambacho kinaonesha kuwa makomando wa Mbowe na yeye walivyojiratibu ualifu na ushahidi waliokuwa nao kama vile kuambiwa silaha walizokuwa nazo.
10. Je, kwanini Urio hakuchagua kusimama na makomando kwa kuweka nguvu kwao ya pesa na hata ajira serikalini upya ili waende kukusanya ushahidi wa ualifu na sio kuwaunganisha kwenye ualifu moja kwa moja.
11. Urio alionesha walijuana na Mbowe tokea 2009. Iweje Sasa Mbowe akate mawasiliano nae tu mara baada ya kumuunganisha na makomando. Yani akaacha kumwamini na kuanza kuwaamini makomando aliokutana nao chini ya mwezi na kuwashirikisha kwenye mipango hatari.
12. Kwanini wapelelezi walimuachia Urio jukumu la kutafuta watu wake mwenyewe na sio kumuandalia kati ya hao watu makachero au kachero moja wapo ili akafanye Kazi na Mbowe ili wapate usibitisho kamili na usio na Shaka.
13. Kwa ushaidi wa Urio mtuhumiwa kamili alikuwa moja tu Mbowe. Hawa wengine ni watuhumiwa aliowafundisha uhalifu na kuwaingiza ni yeye.
14. Urio anakiri pia kujua uadilifu wa watu aliomtafutia Mbowe afanye nao Kazi. Ndio maana akasema alijua wapo kwenye viapo na angewaambia kuhusu kufanya uhalifu wangekataa.
15. Urio pia anakiri pia hao watu aliheshimiana nao na kujuana nao kitambo. Na aliwaalifu wakiona kuna dalili ya uhalifu wamtaarifu. Akawakumbusha kuwa bado wapo kwenye kiapo. Hivyo yeye Kama kiongozi wao hakuwapanga kufanya ualifu. Je kwa mazingira hayo walithubutu vipi kuwa huru kumweleza moja kwa moja kuwa wanaenda kufanya uhalifu bila woga wowote Wala kuwashawishiwa kwake?.
16. Urio anasema hajui maana ya home boy.
17. Urio anaonesha pia kuaminiwa mwanzo na wapelelezi na kuachiwa kuratibu kila kitu. Lakini mwishoni anaonesha kutoaminika tena na kuombwa simu zake zichunguzwe. Maana Kama wangemuamini wasingemnyanganya simu bali wangemuomba namba zake za simu tu ili watafute ushaidi wanaoutaka. Kuchukua simu ni kutafuta ambayo hakuyasema.
18. Kwa kunyanganywa mawasiliano binafsi wakati yeye si mhalifu ilikuwa ni Kama kumtesa Urio kisaikolkjia.
19. Urio anasema amejuana na Mbowe toka mwaka 2009. Toka wakati huo wote hajasema Mbowe kumshirikisha kwenye uhalifu wowote na kunachaguzi nyingi zimepita. Kwanini mwaka 2020 Tena Mbowe anashirikisha watu aliofahamina nao kwa siku chache mno. Chini ya siku 10.
20. Urio amejenga hoja tokea awali kuwa Mbowe alihitaji ukaribu na Urio ili kupata mifumo ya ulinzi na kuwajua wanaoutaka kuhujumu chama kwa kutoa Siri.
Urio akija kesho mahakamani nishitueni. Naona ushaidi wake unaegemea kumuondolea Mbowe shutuma.
2. Kucheleweshwa ushaidi wake kwa siku moja ama kulikuwa na mashaka juu ya ushaidi wake kutoka kwa mawakili wa Serikali au yeye mwenyewe.
3. Amejaribu kutoa kauli za kumtetea Mbowe kuwa pesa alizotumiwa na Mbowe zilikuwa za nauli kwaajili ya kuifikisha walinzi kwa Mbowe na sio za kununua vifaa au vya Ugaidi au malipo ya kufanya Ugaidi.
4. Hoja ya Mbowe kuajiri makomando wanne tu kwaajili ya kukata miti ni kiloja kabisa. Kwamba ilihitaji kuwa na makomando ndio wakate miti.
5. Je, makomando wanne wanawezaje kukata miti na kuchoma vituo vya mafuta Tanzania nzima ni swali gumu kabisa kulielezea.
6. Je, mawakili wanaamini uchomaji vituo vya mafuta na kukata miti ungeweza kuvutia maandamano au kuwatia watu woga na kujifungia ndani? Kama vibomu vya machozi tu na milio ya riasasi watu hujifungia ndani milipuko ya vituo vingevutiaje watanzania kuandamana.
7. Tanzania ina makomando wangapi? Makomando hao wanne wangesaidia vipi Mbowe na elimu yake hao makomando wanne tu kusimamisha nchi isitawalike na kudhibiti makomando zaidi mia watiifu serikalini.
8. Urio lazima aoneshe baada ya kile alichopanga baada ya kuchomà vituo ni vipi Mbowe angepewa nchi na
sio Wanajeshi kuchukua nchi.
9. Je, Urio hajaonesha chochote ambacho kinaonesha kuwa makomando wa Mbowe na yeye walivyojiratibu ualifu na ushahidi waliokuwa nao kama vile kuambiwa silaha walizokuwa nazo.
10. Je, kwanini Urio hakuchagua kusimama na makomando kwa kuweka nguvu kwao ya pesa na hata ajira serikalini upya ili waende kukusanya ushahidi wa ualifu na sio kuwaunganisha kwenye ualifu moja kwa moja.
11. Urio alionesha walijuana na Mbowe tokea 2009. Iweje Sasa Mbowe akate mawasiliano nae tu mara baada ya kumuunganisha na makomando. Yani akaacha kumwamini na kuanza kuwaamini makomando aliokutana nao chini ya mwezi na kuwashirikisha kwenye mipango hatari.
12. Kwanini wapelelezi walimuachia Urio jukumu la kutafuta watu wake mwenyewe na sio kumuandalia kati ya hao watu makachero au kachero moja wapo ili akafanye Kazi na Mbowe ili wapate usibitisho kamili na usio na Shaka.
13. Kwa ushaidi wa Urio mtuhumiwa kamili alikuwa moja tu Mbowe. Hawa wengine ni watuhumiwa aliowafundisha uhalifu na kuwaingiza ni yeye.
14. Urio anakiri pia kujua uadilifu wa watu aliomtafutia Mbowe afanye nao Kazi. Ndio maana akasema alijua wapo kwenye viapo na angewaambia kuhusu kufanya uhalifu wangekataa.
15. Urio pia anakiri pia hao watu aliheshimiana nao na kujuana nao kitambo. Na aliwaalifu wakiona kuna dalili ya uhalifu wamtaarifu. Akawakumbusha kuwa bado wapo kwenye kiapo. Hivyo yeye Kama kiongozi wao hakuwapanga kufanya ualifu. Je kwa mazingira hayo walithubutu vipi kuwa huru kumweleza moja kwa moja kuwa wanaenda kufanya uhalifu bila woga wowote Wala kuwashawishiwa kwake?.
16. Urio anasema hajui maana ya home boy.
17. Urio anaonesha pia kuaminiwa mwanzo na wapelelezi na kuachiwa kuratibu kila kitu. Lakini mwishoni anaonesha kutoaminika tena na kuombwa simu zake zichunguzwe. Maana Kama wangemuamini wasingemnyanganya simu bali wangemuomba namba zake za simu tu ili watafute ushaidi wanaoutaka. Kuchukua simu ni kutafuta ambayo hakuyasema.
18. Kwa kunyanganywa mawasiliano binafsi wakati yeye si mhalifu ilikuwa ni Kama kumtesa Urio kisaikolkjia.
19. Urio anasema amejuana na Mbowe toka mwaka 2009. Toka wakati huo wote hajasema Mbowe kumshirikisha kwenye uhalifu wowote na kunachaguzi nyingi zimepita. Kwanini mwaka 2020 Tena Mbowe anashirikisha watu aliofahamina nao kwa siku chache mno. Chini ya siku 10.
20. Urio amejenga hoja tokea awali kuwa Mbowe alihitaji ukaribu na Urio ili kupata mifumo ya ulinzi na kuwajua wanaoutaka kuhujumu chama kwa kutoa Siri.
Urio akija kesho mahakamani nishitueni. Naona ushaidi wake unaegemea kumuondolea Mbowe shutuma.