William Mshumbusi

JF-Expert Member
Mar 27, 2012
1,657
2,252
1. Wakati akitoa ushahidi wake wote Mara kadhaa wakili aliyemuongoza alisita kuendelea kumuuliza na kuanza kuteta chini kwa chini ikionesha Kuna majibu Alitoa nje ya matarajio yao.

2. Kucheleweshwa ushaidi wake kwa siku moja ama kulikuwa na mashaka juu ya ushaidi wake kutoka kwa mawakili wa Serikali au yeye mwenyewe.

3. Amejaribu kutoa kauli za kumtetea Mbowe kuwa pesa alizotumiwa na Mbowe zilikuwa za nauli kwaajili ya kuifikisha walinzi kwa Mbowe na sio za kununua vifaa au vya Ugaidi au malipo ya kufanya Ugaidi.

4. Hoja ya Mbowe kuajiri makomando wanne tu kwaajili ya kukata miti ni kiloja kabisa. Kwamba ilihitaji kuwa na makomando ndio wakate miti.

5. Je, makomando wanne wanawezaje kukata miti na kuchoma vituo vya mafuta Tanzania nzima ni swali gumu kabisa kulielezea.

6. Je, mawakili wanaamini uchomaji vituo vya mafuta na kukata miti ungeweza kuvutia maandamano au kuwatia watu woga na kujifungia ndani? Kama vibomu vya machozi tu na milio ya riasasi watu hujifungia ndani milipuko ya vituo vingevutiaje watanzania kuandamana.

7. Tanzania ina makomando wangapi? Makomando hao wanne wangesaidia vipi Mbowe na elimu yake hao makomando wanne tu kusimamisha nchi isitawalike na kudhibiti makomando zaidi mia watiifu serikalini.

8. Urio lazima aoneshe baada ya kile alichopanga baada ya kuchomà vituo ni vipi Mbowe angepewa nchi na
sio Wanajeshi kuchukua nchi.

9. Je, Urio hajaonesha chochote ambacho kinaonesha kuwa makomando wa Mbowe na yeye walivyojiratibu ualifu na ushahidi waliokuwa nao kama vile kuambiwa silaha walizokuwa nazo.

10. Je, kwanini Urio hakuchagua kusimama na makomando kwa kuweka nguvu kwao ya pesa na hata ajira serikalini upya ili waende kukusanya ushahidi wa ualifu na sio kuwaunganisha kwenye ualifu moja kwa moja.

11. Urio alionesha walijuana na Mbowe tokea 2009. Iweje Sasa Mbowe akate mawasiliano nae tu mara baada ya kumuunganisha na makomando. Yani akaacha kumwamini na kuanza kuwaamini makomando aliokutana nao chini ya mwezi na kuwashirikisha kwenye mipango hatari.

12. Kwanini wapelelezi walimuachia Urio jukumu la kutafuta watu wake mwenyewe na sio kumuandalia kati ya hao watu makachero au kachero moja wapo ili akafanye Kazi na Mbowe ili wapate usibitisho kamili na usio na Shaka.

13. Kwa ushaidi wa Urio mtuhumiwa kamili alikuwa moja tu Mbowe. Hawa wengine ni watuhumiwa aliowafundisha uhalifu na kuwaingiza ni yeye.

14. Urio anakiri pia kujua uadilifu wa watu aliomtafutia Mbowe afanye nao Kazi. Ndio maana akasema alijua wapo kwenye viapo na angewaambia kuhusu kufanya uhalifu wangekataa.

15. Urio pia anakiri pia hao watu aliheshimiana nao na kujuana nao kitambo. Na aliwaalifu wakiona kuna dalili ya uhalifu wamtaarifu. Akawakumbusha kuwa bado wapo kwenye kiapo. Hivyo yeye Kama kiongozi wao hakuwapanga kufanya ualifu. Je kwa mazingira hayo walithubutu vipi kuwa huru kumweleza moja kwa moja kuwa wanaenda kufanya uhalifu bila woga wowote Wala kuwashawishiwa kwake?.

16. Urio anasema hajui maana ya home boy.

17. Urio anaonesha pia kuaminiwa mwanzo na wapelelezi na kuachiwa kuratibu kila kitu. Lakini mwishoni anaonesha kutoaminika tena na kuombwa simu zake zichunguzwe. Maana Kama wangemuamini wasingemnyanganya simu bali wangemuomba namba zake za simu tu ili watafute ushaidi wanaoutaka. Kuchukua simu ni kutafuta ambayo hakuyasema.

18. Kwa kunyanganywa mawasiliano binafsi wakati yeye si mhalifu ilikuwa ni Kama kumtesa Urio kisaikolkjia.

19. Urio anasema amejuana na Mbowe toka mwaka 2009. Toka wakati huo wote hajasema Mbowe kumshirikisha kwenye uhalifu wowote na kunachaguzi nyingi zimepita. Kwanini mwaka 2020 Tena Mbowe anashirikisha watu aliofahamina nao kwa siku chache mno. Chini ya siku 10.

20. Urio amejenga hoja tokea awali kuwa Mbowe alihitaji ukaribu na Urio ili kupata mifumo ya ulinzi na kuwajua wanaoutaka kuhujumu chama kwa kutoa Siri.

Urio akija kesho mahakamani nishitueni. Naona ushaidi wake unaegemea kumuondolea Mbowe shutuma.
 
Na kwanini Mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi wake akiwa na Bilicanas?

Je, hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishirini?

Je, wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?
 
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas...
Mabaunsa unazani diamond huyo? Je, wanaweza kuzuia au kupambana kwa kutumia silaha za Moto Kama zile zilizomkuta lisu. Je, hujifunza kutumia silaha?

Baunsa ilikuwa sawa kabla ya lisu
 
Aisee, kiukweli ushahidi wa kubumba wa mtu aliyekalishwa chini ili akaseme uongo kum - incriminate ndugu yake asiye na hatia ni rahisi mno kuugundua kwa sababu huwa unakosa uhalisia na siku zote huyu shahidi wa uongo hujisahau na hukosa consistency katika melezo yake.

Kwa mfano, huyu Denis Urio, kuna maelezo ya matendo yake mwenyewe au ya wale anaotaka wahukumiwe akiwemo Freeman Mbowe hayana uhalisia bali ni hisia zake tu na kwa namna yoyote hayathibitiki na mtu mwenye akili timamu hawezi kuàmini wala kufikiri kutendwa na mtu smart kichwani mwenye nia kutenda uovu mkubwà kama wa ugaidi!

Najua (anaweza) kuendelea kumwaga pumba zake kesho.

Nakubaliana na wewe kuwa, kwa hakika kabisa, pengine huyu Denis Urio ndiye anayeweza kuwa shahidi wa hovyo zaidi wa upande wa mashtaka kuliko mashahidi wengine 11 wote waliotangulia anàyejaribu kuweka wazi (expose) udhaifu wa mashitaka haya!

Ni afadhali hata Kingai au Mahita!

To cut it short, hii timu ya kubumba kesi hii ili kum - incriminate Ndg Freeman Mbowe wamefeli kwa kiwango cha juu sana maana hata mjinga kabisa aweza kujua ukweli huu mpaka hapa ilipofika!
 
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas?
...
Pamoja na kujua hayo yote bado jeshi likawafukuza kazi na wengine wakawa madereva wa IT. Hivi jeshi halikujua kuwa hawa watu kukosa kazi ni hatari zaidi? Inakuwaje kama wangeamua kuwa majambazi?

Kuhusu Mbowe kuhitaji ulinzi wa makomandoo jibu ni kwasababu Mbowe amewahi kupigwa na kuvunjwa mguu. Lissu amewahi kupigwa risasi mchana kweupe hivyo alihitaji ulinzi wa professional na well trained personnel.
 
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas?
Je hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishilini?

Je wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?

Luteni Urio amekosea kuwalengesha vijana wa watu wakaacha ajira zao na kuwatumbukiza ktk " mipango " ya Mbowe.

Mbowe alitakiwa achomekewe undercover police ambao wangeenda naye taratibu mpaka wamkamate kukiwa na ushahidi usio na mashaka.
 
Homeboy Urio katika ushahidi kakiri pesa zilizotumwa kwake zilikuwa ni nauli ili kufanikisha watu wanne wakapate kazi ya upambe/ulinzi...

Nyuma kidogo, kutoka mashahidi wale waliokuwa na simu, waliweka bayana kuwa hakuna mahali katika maandishi yaliyokaguliwa kama kulionesha kiashiria cha ugaidi...
 
Aliogopa kukutwa na yaliyomkuta Lissu.
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas?
Je hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishilini?

Je wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?
 
..Luteni Urio amekosea kuwalengesha vijana wa watu wakaacha ajira zao na kuwatumbukiza ktk " mipango " ya Mbowe.

..Mbowe alitakiwa achomekewe undercover police ambao wangeenda naye taratibu mpaka wamkamate kukiwa na ushahidi usio na mashaka.

Hadi sasa nasubiri kusikia ni wakati gani Jeshi la Polisi liliishirikisha Idara ya Ujasusi ya Tanzania baada ya kusikia kuna uhalifu mkubwa unaoratibiwa na unahatarisha amani ya nchi na pengine uRais wa nchi...

Pia nasubiria ni wakati gani ambapo Jeshi la Polisi lilihusisha Jeshi la Wananchi (Idara ya Ujasusi wa jeshi) kuieleza kuwa kuna watu wanapanga nchi kutotawalika maana jukumu mojawapo la jeshi la wananchi ni kuhakikisha nchi ipo stable...
 
Na kwa nini mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi .wake akiwa na bilicanas?
Je hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishilini?

Je wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?
VIP protection haifanywi na mtu yeyote ila mtu mwenye mafunzo.
 
Ni kwamba kwenye ada za mpesa na tigo pesa hata kabla ya ujio wa tozo

Makato ya kutoa muamala wa 10,000 ilikuwa ni 1,450

Ila luteni alitumiwa 500,000 akatoa 499,000 yani alikatwa buku

Unaweza ukaona ni hoja nyepesi lakini kumbuka pesa hiyo kaielezea kwenye ushahidi ilivyotumika mpaka ikaisha, so hakutakuwa na excuse kwamba nilikosea

Kwasababu kufanya hivyo kutaharibu chain nzima ya ushahidi wake aliotoa na kuonesha kile kiwango alichowapa wale makomandoo kama nauli hakikuwa sahihi, kosa ambalo alitakiwa aliepuke mapema wakati akiongozwa na wakili wake
 
Back
Top Bottom