Nina kadi za vyama viwili

Avanti

JF-Expert Member
Aug 24, 2010
1,209
239
Nilipoanza kidato cha kwanza 1990 nilikuta chama kimoja na hivyo nikawa mwanachama wa UVCCM kama ilivyokuwa desturi. Nikasonga na UVCCM mpaka nikapata na uongozi. Then niliacha kufanya siasa na nikajikita na fani yangu ingawa sikutupa kadi zangu za CCM. Mwaka jana niliposikia Dr Slaa ana kadi ya CCM nikajua kumbe inawezekana kuwa mwanachama wa vyama viwili nami nikajiunga na CDM na ninaretain kadi zote. Nikitathmini umaarufu wa kadi zangu ya CDM ilikuwa inakimbiza sana na nilikuwa naitoa toa mfukoni mbele ya kadamnasi ili kupata ujiko ila kwa sasa nayo imeporomoka umaarufu wake ghafla na imekuwa km zile za CCM tu. Hakika Zitto ana kanguvu fulani hivi tusimchukulie kwa papara!
 
Back
Top Bottom