Nina hasira sana!

Hmaster

JF-Expert Member
Dec 27, 2010
346
86
Katika gazeti la mwananchi la leo ukurasa wa pili nimekutana na picha ikimwonyesha Rehema Mohamed (diwani viti maalum CHADEMA-Arusha Mjini aliyetimuliwa uanachama) akichangia hoja katika kikao cha baraza hilo katika halmashauli hiyo kilichofanyika jana. Hivi wanaCHADEMA hili jambo tunalichukuliaje hasa? Yaani nimekosa raha kabisa hapa na najilaumu kwanini nilisoma hili gazeti leo kwa vile tata habari yake ya mbele sijaipenda kabisa. Yaani tunakubali kirahisi hivi katiba ya nchi inakanyagwa na mtu kama Mkuchika tu? Toeni maoni yenu jamani. Na je zile siku 30 alizotoa Mh. Mbowe kuhusu kumfungia nje ya ofisi mkurugenzi wa halmashauli zinaisha lini?
 
Back
Top Bottom