indundidotcom
JF-Expert Member
- Mar 4, 2017
- 229
- 226
Wandugu mimi ni mfanyakazi katika taasisi binafsi ya elimu, nna mke na watoto wawili, nimeishi na mke wangu Sasa mwaka wa 4 baada ya kumzalisha baadae nikamchukua awe mke wangu,
Mwaka Jana mwishoni nlilipa mahari kiasi Cha tsh 1.5m na tumeishi maisha ya amani mpaka leo ila Ana matatizo haya ndio yamenifanya niwaone wakuu:
Mosi, huwa anapata wakati mgumu kunijibu ninapomuuliza kitu
Pili, ni muongo, anaweza kukueleza kwamba alikueleza kitu Fulani wakati hakusema kabisaaa
Tatu, amekuwa mvivu kunifulia hasa baada ya Mimi kufanya kufua nguo kipindi akiwa mgonjwa, now anahisi ni wajibu wangu kufua
Nne, Jambo la Mimi kuoga Wala usimuulize, nna Zaidi ya mwezi sijatengewa maji ya kuoga najitengea mwenyewe
Tano, anapenda Sana kunichunguza Kama nachepuka, juzi tumegombana kwa kusachi simu yangu japo hapakuwa na pa kunikamatia ila kuona sms ya mdada kanisalimia ilikuwa Vita.
Na hii ndio shida kuu, ananivizia usiku anasearch simu yangu Sana na sometime anawapigia wadada nilowasave namba zao, KEROOO
NATAMANI SANA AMANI LAKINI NAHISI ANATAFUTA SHIDA
NISHAACHA UJINGA JAPO HATA YEYE NILIMPATIA UJINGANI LAKINI NAHISI ATANIRUDISHA UJINGANI
USHAURI WENU PLEASE....
Mwaka Jana mwishoni nlilipa mahari kiasi Cha tsh 1.5m na tumeishi maisha ya amani mpaka leo ila Ana matatizo haya ndio yamenifanya niwaone wakuu:
Mosi, huwa anapata wakati mgumu kunijibu ninapomuuliza kitu
Pili, ni muongo, anaweza kukueleza kwamba alikueleza kitu Fulani wakati hakusema kabisaaa
Tatu, amekuwa mvivu kunifulia hasa baada ya Mimi kufanya kufua nguo kipindi akiwa mgonjwa, now anahisi ni wajibu wangu kufua
Nne, Jambo la Mimi kuoga Wala usimuulize, nna Zaidi ya mwezi sijatengewa maji ya kuoga najitengea mwenyewe
Tano, anapenda Sana kunichunguza Kama nachepuka, juzi tumegombana kwa kusachi simu yangu japo hapakuwa na pa kunikamatia ila kuona sms ya mdada kanisalimia ilikuwa Vita.
Na hii ndio shida kuu, ananivizia usiku anasearch simu yangu Sana na sometime anawapigia wadada nilowasave namba zao, KEROOO
NATAMANI SANA AMANI LAKINI NAHISI ANATAFUTA SHIDA
NISHAACHA UJINGA JAPO HATA YEYE NILIMPATIA UJINGANI LAKINI NAHISI ATANIRUDISHA UJINGANI
USHAURI WENU PLEASE....