Nina hakika muda wa kusajili laini za simu utaongezwa. Watanzania msiwe na wasiwasi

magode

JF-Expert Member
Oct 2, 2014
2,201
3,322
Wanajamvi Salaam!

Zoezi la kusajili laini za mitandao ya simu litakamilika rasmi December 31. Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimekuwa zikitolewa na TCRA, Waziri anayehusika na mawasiliano pamoja na kampuni za Simu, zoezi hilo litakapokamilika muda hautoongezwa.

Kwa maoni yangu, naomba niwaondoe wasiwasi Watanzania wenzangu, kutokana na sababu chache nitakazozitaja hapa chini, zoezi hilo iwe isiwe lazima litaongezwa muda, tena siyo muda tu, muda wa kutosha!

Sababu hizo ni hizi zifuatazo:

1. Utaratibu wa kupata kitambulisho cha uraia sio rafiki kwa wananchi, na makosa kwa 85 yapo kwa NIDA wenyewe, hivyo kwa vyovyote vile serikali haiwezi kuwaadhibu wananchi wasio na kosa kwa kuwafungia mawasiliano.

2. Kampuni za simu kwa sasa zina mchango mkubwa sana katika kuchangia uchumi wa nchi. Serikali haiwezi kujiingiza kwenye mkenge wa kupoteza mapato.

3. Serikali ya awamu hii ni ya wapenda kiki. Kwa vyovyote vile number 1 atatafutia kiki hii issue. Kama TCRA na Waziri wataendelea kukomaa kuwa wanafungia laini za simu, number 1 atatoka kama kawaida yake na ataongeza muda wa kutosha! Kumbukeni mwaka ujao ni uchaguzi mkuu. Number 1 hawezi kukubali kuharibu kura hadi za CCM.

Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Watakao fungiwa ni wale tuu ambao wanavitambulisho au wana namba za vitambulisho.


Kama wewe hujapata hivyo viwili tarehe 31 Dec haikuhusu kabisa.
Wanajamvi Salaam!

Zoezi la kusajili laini za mitandao ya simu litakamilika rasmi December 31. Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimekuwa zikitolewa na TCRA, Waziri anayehusika na mawasiliano pamoja na kampuni za Simu, zoezi hilo litakapokamilika muda hautoongezwa.

Kwa maoni yangu, naomba niwaondoe wasiwasi Watanzania wenzangu, kutokana na sababu chache nitakazozitaja hapa chini, zoezi hilo iwe isiwe lazima litaongezwa muda, tena siyo muda tu, muda wa kutosha!

Sababu hizo ni hizi zifuatazo:

1. Utaratibu wa kupata kitambulisho cha uraia sio rafiki kwa wananchi, na makosa kwa 85 yapo kwa NIDA wenyewe, hivyo kwa vyovyote vile serikali haiwezi kuwaadhibu wananchi wasio na kosa kwa kuwafungia mawasiliano.

2. Kampuni za simu kwa sasa zina mchango mkubwa sana katika kuchangia uchumi wa nchi. Serikali haiwezi kujiingiza kwenye mkenge wa kupoteza mapato.

3. Serikali ya awamu hii ni ya wapenda kiki. Kwa vyovyote vile number 1 atatafutia kiki hii issue. Kama TCRA na Waziri wataendelea kukomaa kuwa wanafungia laini za simu, number 1 atatoka kama kawaida yake na ataongeza muda wa kutosha! Kumbukeni mwaka ujao ni uchaguzi mkuu. Number 1 hawezi kukubali kuharibu kura hadi za CCM.

Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vitambulisho vya NiDa vinapatikana Kwa urahisi tu sema ni watu ndio hawana muamko wa kufuatilia na kujisajili. Sasa acha tuzimiwe simu kama wk moja then waturudishe hewani kisha waongeze miezi mitatu uone watu watavyokimbia kujisajili!
 
Vitambulisho vya NiDa vinapatikana Kwa urahisi tu sema ni watu ndio hawana muamko wa kufuatilia na kujisajili. Sasa acha tuzimiwe simu kama wk moja then waturudishe hewani kisha waongeze miezi mitatu uone watu watavyokimbia kujisajili!
Unajua ukizima laini milioni 2 kwa masaa 24 tu,zinapotea Tsh ngapi!?? Hayupo mtu mjinga wa kutekeleza ujinga wa aina hiyo. We subiri baada ya Tar.31 utarudi hapa..!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vitambulisho vya NiDa vinapatikana Kwa urahisi tu sema ni watu ndio hawana muamko wa kufuatilia na kujisajili. Sasa acha tuzimiwe simu kama wk moja then waturudishe hewani kisha waongeze miezi mitatu uone watu watavyokimbia kujisajili!
Mkuu utakua umezoea shida ndio maana huon dhahama watu wanayopata katika kufuatilia hivyo vitambulisho vya nida, au utakua mtumishi wa umma kwahivyo ulipata kitambulisho ki ubwete.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acha uongo, nenda ofisi za halmashsuri uone nida wanavyo zingua.

Kila siku kuna police kuwalinda wahudumu maana nasikia kila siku kuna varangati na kuna siku kidogo wapigwe na raia wenye hasira.
Vitambulisho vya NiDa vinapatikana Kwa urahisi tu sema ni watu ndio hawana muamko wa kufuatilia na kujisajili. Sasa acha tuzimiwe simu kama wk moja then waturudishe hewani kisha waongeze miezi mitatu uone watu watavyokimbia kujisajili!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vitambulisho vya NiDa vinapatikana Kwa urahisi tu sema ni watu ndio hawana muamko wa kufuatilia na kujisajili. Sasa acha tuzimiwe simu kama wk moja then waturudishe hewani kisha waongeze miezi mitatu uone watu watavyokimbia kujisajili!
Kuwa serious,vinapatikana kwa urahisi wapi,watu wanaamka saa 10 usiku wanakuwa wamepanga foleni,labda kama wewe uliandikishiwa ofisini kwako na kuletewa hapo hapo ndiyo maana unaona rahisi
 
Vitambulisho vya NiDa vinapatikana Kwa urahisi tu sema ni watu ndio hawana muamko wa kufuatilia na kujisajili. Sasa acha tuzimiwe simu kama wk moja then waturudishe hewani kisha waongeze miezi mitatu uone watu watavyokimbia kujisajili!
Duu kweli wewe kichefuchefu na comment imekuwa kichefuchefu zaidi,,,,hujaijua shida iliyopo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimefuata the same procedure kupata no ya NiDa. Its not that easy but also not that hard!
Nilipata ID enzi za Jk wakati watu hawana time navyo,ila baada ya waliokuwa wamepewa training nzuri kuondolewa na kuokotwa okotwa tu wasio na ujuzi,zoezi limekuwa gumu maana walioletwa wengi hawana ujuzi sana........kwasasa siyo huduma ila ni kero
 
Subiri izimiwe ndiyo utajua kumbe maharage ni mboga!
Watu wanacheza karata ya 2020,hazitazimwa muda utaongezwa mpaka nwakani........Ila kama hujasajili usilale endelea kufuatutilia usifuate comment yangu mi ninacho tayari
 
Mimi nitafarijika tu kuona yale matapeli yakidhibitiwa! Haiwezekani tapeli linakupigia simu na likishaona tu umelishtukia, linakuporomoshea matusi ya nguoni! Na mwisho wa siku huna cha kulifanya.
 
Kuwa serious,vinapatikana kwa urahisi wapi,watu wanaamka saa 10 usiku wanakuwa wamepanga foleni,labda kama wewe uliandikishiwa ofisini kwako na kuletewa hapo hapo ndiyo maana unaona rahisi
Mkuu, wakati nafuatilia kitambulishosikuwa hata na ajira kwa hiyo nauli ya kwenda NiDa ilikuwa ni shida. Nilikuwa natembea kwa mguu kwenda ofisi za NiDa umbali wa kama km 6. Nadhani unajua ofisi za NiDa zilivyo mbali kule Morogoro. So kama mie niliweza, wewe huna sababu ya kushindwa.
 
Duu kweli wewe kichefuchefu na comment imekuwa kichefuchefu zaidi,,,,hujaijua shida iliyopo

Sent using Jamii Forums mobile app
If you want to kill Green Algae, all you need is to shock the Pond. Line inabidi zizimwe kwa mda wa wk moja, then mkombozi wetu Magufuli ajitokeze kwenye vyombo vya habari kuongeza miezi mingine sita ya usajili kitu kitakacho mpa porpularity boosting kuelekea 2020. Mie japo nina No ya NiDa, nasubiri kuzimiwa simu ndio nikasajiliwe.
 
Kwa nini kitambulisho cha kupigia kura nilikipata ndani ya masaa mawili halafu cha nida miaka na miaka?

acheni wazime unless wangeanzisha online application ili kuhudumia watu hata wasio na muda mrefu wa kupoteza kwenye kufatilia
 
Wakijichanganya wakazifunga nahisi kuna kitu kibaya lazima tu kitokee kwa jinsi watanzania walivyokuwa addicted na simu
 
Wanajamvi Salaam!

Zoezi la kusajili laini za mitandao ya simu litakamilika rasmi December 31. Kwa mujibu wa taarifa ambazo zimekuwa zikitolewa na TCRA, Waziri anayehusika na mawasiliano pamoja na kampuni za Simu, zoezi hilo litakapokamilika muda hautoongezwa.

Kwa maoni yangu, naomba niwaondoe wasiwasi Watanzania wenzangu, kutokana na sababu chache nitakazozitaja hapa chini, zoezi hilo iwe isiwe lazima litaongezwa muda, tena siyo muda tu, muda wa kutosha!

Sababu hizo ni hizi zifuatazo:

1. Utaratibu wa kupata kitambulisho cha uraia sio rafiki kwa wananchi, na makosa kwa 85 yapo kwa NIDA wenyewe, hivyo kwa vyovyote vile serikali haiwezi kuwaadhibu wananchi wasio na kosa kwa kuwafungia mawasiliano.

2. Kampuni za simu kwa sasa zina mchango mkubwa sana katika kuchangia uchumi wa nchi. Serikali haiwezi kujiingiza kwenye mkenge wa kupoteza mapato.

3. Serikali ya awamu hii ni ya wapenda kiki. Kwa vyovyote vile number 1 atatafutia kiki hii issue. Kama TCRA na Waziri wataendelea kukomaa kuwa wanafungia laini za simu, number 1 atatoka kama kawaida yake na ataongeza muda wa kutosha! Kumbukeni mwaka ujao ni uchaguzi mkuu. Number 1 hawezi kukubali kuharibu kura hadi za CCM.

Nawasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
Wazime tuone ataumia nani ? mimi pesa niliokuwa nanunulia vocha sasa naongeza bajeti ya bia
 
Back
Top Bottom