Nina ADA, CPA(T) na Masters in Accounting and Finance lakini sina kazi zaidi ya mwaka sasa!

Kikomelo

Senior Member
Sep 12, 2011
106
57
"Jamani wadau naomba msaada, mana nimeangaika hadi nimechoka kutafuta kazi. Nina Ordinary Diploma in Accountancy GPA 4, Advance Diploma in Accountancy GPA 4.2. zote nimepiga IFM.

Nilipomaliza Advance mwaka 2009 niliunganisha kufanya masters ya Accounting and Finance toka Mzumbe University, and on the same time nikawa nafanya CPA.

CPA nilipass zote at 1st sitting na June mwaka jana nikawa nimeipata. Masters nina GPA 4.1, bado kudefend thesis tu. lakini wadau nimetafuta kazi tangu nilivyopata hiyo CPA hadi leo hola! Nisaidieni basi ndugu zangu!"


Jamani wadau, hiyo topic hapo juu niliyoibold niliiweka mwishoni mwa mwaka 2011 wakati huo nilikuwa sijakamata line. Nashukuru Mungu baada ya muda kidogo (baada ya kuandika hiyo mada) nilipata mchongo kama mhasibu kwenye shirika moja la kimataifa, na kwa muda mfupi tu nilipanda na kufikia cheo kizuri kilichinifanya nisahahu shida nilizozipata. Nilikaa na hilo shirika kwa muda wa kama miezi tisa hivi, nikawa nimepata kazi kupitia utumishi kama assistant lecturer kwenye chuo kimoja cha elimu ya juu cha umma.
Wakati napata nafasi hiyo ya assistant lecturer nilikuwa nimeshaandaa mipango ya scholarship ya PhD. Mipango ilikubari na sasa niko huku ughaibuni nagonga PhD(Finance).
Nawashukuru nyote mlionishauri kwa kipindi kile kigumu, pamoja na wale walionibeza. Mungu ni mwema, sikupita mlimani wala nini lakini leo nafanya PhD na nina kazi nzuri. Nashauri watu kuwa waache kubezana! Good Lucky
 
pole sana,kama huna connections i suggest u look for a job in organizations that value education background such as TRA,TBL,and other private companies ambazo hazina wabongo wengi!!!!kuwa mvumilivu,utapata kazi!!!
By the way mie naenda hapo mzumbe,mbona wametuongezea ada,wanatupa kweli hivo vitabu au ndo tunalipia tu
 
Jamani wadau naomba msaada, mana nimeangaika hadi nimechoka kutafuta kazi. Nina Ordinary Diploma in Accountancy GPA 4, Advance Diploma in Accountancy GPA 4.2. zote nimepiga IFM. Nilipomaliza Advance mwaka 2009 niliunganisha kufanya masters ya Accounting and Finance toka Mzumbe University, and on the same time nikawa nafanya CPA. CPA nilipass zote at 1st sitting na June mwaka jana nikawa nimeipata. Masters nina GPA 4.1, bado kudefend thesis tu. lakini wadau nimetafuta kazi tangu nilivyopata hiyo CPA hadi leo hola! nisaidieni basi ndugu zangu!

Kwa sifa zako za elimu hustahili kulala huna kazi. Nachoweza kukushauri ajira kwa sasa ni gharama kwa mtu kama wewe ambaye huna uzoefu wowote maana utakuwa unahitaji mshahara mkubwa sana wakati uzalishaji wako (productivity) unaweza kuwa chini ya mtu mzoefu mwenye ATEC.

Nachokushauri tafuta audit firm ambayo iko busy uombe hata kukaa pale kama "Voluteer" wakikulipa kwa "assignment basis" baada ya miezi sita CV yako itapanda na utakuwa unatafutwa badala ya wewe kutafuta kazi. Kuna mtu alikuwa na tatizo kama lako nilikaa naye kama mwaka sasa hivi yuko kwenye chati na mara ya mwisho ilibidi aombe ushauri maana alipata zaidi ya kazi tatu kwa mara moja.

Kama uko Arusha unaweza jaribu Welcome to Facebook - Log In, Sign Up or Learn More
 
Kikomelo siju ya lubale Bukoba?Any way atafutae achoki akichoka kaisha pata.Endelea tu kutafuta ipo siku utapata.
 
Jamani wadau naomba msaada, mana nimeangaika hadi nimechoka kutafuta kazi. Nina Ordinary Diploma in Accountancy GPA 4, Advance Diploma in Accountancy GPA 4.2. zote nimepiga IFM. Nilipomaliza Advance mwaka 2009 niliunganisha kufanya masters ya Accounting and Finance toka Mzumbe University, and on the same time nikawa nafanya CPA. CPA nilipass zote at 1st sitting na June mwaka jana nikawa nimeipata. Masters nina GPA 4.1, bado kudefend thesis tu. lakini wadau nimetafuta kazi tangu nilivyopata hiyo CPA hadi leo hola! nisaidieni basi ndugu zangu!

Pole rafiki yangu, kazi utapata tuu, hata mimi hayo yalinikuta nikiwa nina vyeti safi lakini sikuwa na kazi. Chakufanya kwa kuanzia usiwe fasta na mishahara mikubwa. tena waweza anza kuomba kwa kutumia hicho cheti cha ADA. with time ukiwa una grow unaproduce vyeti vikubwa.

Mimi nakumbuka nilianza kama Bank teller CRDB ila nikiwa na CPA kibindoni ila nilishauriwa nisi produce mwanzoni kwasababu sina experience baada ya hapo nikapata nafasi ya Juu kidogo NMB nasasa nipo nusu ya safari ninayo i-dream. (sipo tena NMB)
 
Aisee hii nchi hii!

Nakuombea kheri ndugu yangu, usijali iko siku utafanikiwa....Mwombe sana Mungu, ajira zitakufuata na nyingine utazikimbia......

Ama kwa hakika hilo tu la kumuomba Mungu ndilo lililobakia, ingawa pia yanahitajika maelezo ya kina. Anatafuta kazi ya namna gani.

Isijekutokea kazi anazoomba zinahitaji uzeefu sorry uzoefu wa miaka 10 na yeye kwakuwa ana masters plus CPA anaamua kujitosa hivyo hivyo, na kwa mazingira yetu haya ya kujuana sia ajabu yuko kitaa kwa muda wote huo.
 
Kinachomnyima kazi ni kukosa "practical experience" huko Radar ni wakala tuu kule wanakowapeleka wanataka watu wenye uzoefu wa kufanya kazi wenyewe bila kusimamiwa.

Hao radar wenyewe magumashi tu. Vi post vidogo vidogo ndo wanawezesha kwa uhakika lakini "zilizonona" zina utata kuzipata,..... Kuna jamaa pale anaitwa Steve, huwa simsomi vizuri,....!!
 
Kwa nini usiombe hapo IFM tu wakupe ulecturer? mbona GPA yako inaruhusu ama ndo hizi GPA za kuchakachua? Mi nakushauri uombe kwenye vyuo ndo utapata kama hukuchakachua GPA otherwise CPA si kitu siku hizi kaka yahani uklitamba mbele za watu eti una CPA wanakuona umechelewa tu maana hazina maana kila mtu anayo siku hizi.
 
Hata mimi ninayo lakini sijaona matumizi wala faida yake na mshahara wa kawaida tu serikalini
 
pole sana,kama huna connections i suggest u look for a job in organizations that value education background such as TRA,TBL,and other private companies ambazo hazina wabongo wengi!!!!kuwa mvumilivu,utapata kazi!!!<br />
<i>By the way mie naenda hapo mzumbe,mbona wametuongezea ada,wanatupa kweli hivo vitabu au ndo tunalipia tu</i>

Hasante Janice, nimeshajaribu kila nionapo tangazo kwenye gazeti naomba, lakini siitwi hata kwenye interview.
Kuhusu vitabu, hiyo ishu imekuwa intriduced mwaka jana kwenye facult ya commerce, ila nasikia walirudishiwa pesa zao mana vitabu havikuwa tayari!
 
[QUOTE=yutong;Hata mimi ninayo lakini sijaona matumizi wala faida yake na mshahara wa kawaida tu serikalini
Kwa hiyo ambao hatuna hata tusiangaike kuitafuta.
 
Waone http://www.radarrecruitment.com" Radar Recruitment the leading Recruitment Agency in Tanzania: Home</a> pale BARCLAYS HOUSE Ohio Street muone Catherine Baretto au Janet Igogo utapata kazi halafu unisahau!

Asante sana ndugu yangu, nitaenda kuwaona na nitakupa feedback.
 
11 Reactions
Reply
Back
Top Bottom