Mwanamayu
JF-Expert Member
- May 7, 2010
- 11,349
- 6,476
Jamani wadau naomba msaada, mana nimeangaika hadi nimechoka kutafuta kazi. Nina Ordinary Diploma in Accountancy GPA 4, Advance Diploma in Accountancy GPA 4.2. zote nimepiga IFM.
Nilipomaliza Advance mwaka 2009 niliunganisha kufanya masters ya Accounting and Finance toka Mzumbe University, and on the same time nikawa nafanya CPA.
CPA nilipass zote at 1st sitting na June mwaka jana nikawa nimeipata. Masters nina GPA 4.1, bado kudefend thesis tu. lakini wadau nimetafuta kazi tangu nilivyopata hiyo CPA hadi leo hola! Nisaidieni basi ndugu zangu!
Unakuwaje na Master's degree kabla ya kupata matokeo ya dissertation? Je unafahamu baada ya kupata marks za hiyo dissertation hiyo GPA inaweza kupanda au kushuka? Pia ufahamu kuwa interview uanza kwenye shortlisting sasa kama kuandika kwako maombi kunaonesha walakini basi kupata kazi ni issue. Pia inawezekana wengine wengi wa calibre yako wamefaulu sana kuliko wewe yaani wana GPA 4.5 na kuendelea!!