Nina 5,000,000/= nataka kununua share ,je naanzaje?kampuni ipi inalipa?

FADHILIEJ

Senior Member
Nov 5, 2010
132
18
Wataalamu wa DSE Tafadhali naombeni shule ili kama huko hakufai nione tapeleka wapi kahela kangu,

Nasubiri advice kwa hamu.
 
Subiri za KQ, wametangaza ku-increase debt in a near future
na mpango wao wa expansion unaonekana imara.
kuna thread inayo husiana nahuo mpango jukwaa la kimataifa.
 
Soko la hisa hali yake inabadilika kila wakati. This is to say, hapa JF huwezi kupata actual and reliable answer.

Unachotakiwa kufanya ni kuresearch market ikoje. Kwa research yangu mimi ninaona hisa za Dar es salaam Community Bank kwa sasa zinalipa kwa malengo ya muda mfupi. Hata hivyo availability yake ndio shida kidogo. Hisa zinapokuwa na capital gain nzuri wamiliki huwa hawataki kuziuza.

Kwa malengo ya muda mrefu hisa za CRDB ni nzuri zaidi kwa sababu wamekuwa kwenye soko muda mrefu na wana historia nzuri financially. Hata hivyo capital gain yao siyo kubwa sana.

Hisa zinazopatikana kirahisi ni kama za Tanzania Oxygen ambazo zimekuwa na zero capital gain kwa muda mrefu. Vilevile, kumbuka kuwa biashara ya hisa siyo rahisi sana kama watu wengi wanavodhani, kama unataka kuhakikisha unatrade kwa faida ni vyema ukatumia muda mwingi kwenye kusoma sheria na taratibu za kufanya biashara hii kabla hujaianza.

NB: Hata kama wewe ni mkazi wa Tanzania siyo lazima ununue hisa za DSE tu, unaweza kuvuka mipaka na kuangalia mambo yakoje kwenye masoko mengine. Sheria inaruhusu na internet inawezesha.

Kila la heri katika uwekezaji.
 
Kaka, njoo huku Selous tufanye biashara ya mbao. Tusafiroshe kwenda Japani na Dubai. Hayo DSE ni chaka, biashara ya ku-hedge finance haiko reliable hapa bongo. Ni wazungu huko kwao wanapiga hela. Kwan unaweza kununua hisa za Microsoft leo za milioni 5 ukauza kesho milioni 7 haaaaa..... Bongo doesnt work!!! Mimi nimesomea hayo mamboooo
 
kwa tz biashara ya hisa haina mpango kwani haina mzunguko wa kutosha (capital market is not active), ni bora ukafanya biashara nyingine nakushauri anza na business ya nafaka kwa tenda maalum,search market then supply) but not stock business.
 
Soko la hisa hali yake inabadilika kila wakati. This is to say, hapa JF huwezi kupata actual and reliable answer.

Unachotakiwa kufanya ni kuresearch market ikoje. Kwa research yangu mimi ninaona hisa za Dar es salaam Community Bank kwa sasa zinalipa kwa malengo ya muda mfupi. Hata hivyo availability yake ndio shida kidogo. Hisa zinapokuwa na capital gain nzuri wamiliki huwa hawataki kuziuza.

Kwa malengo ya muda mrefu hisa za CRDB ni nzuri zaidi kwa sababu wamekuwa kwenye soko muda mrefu na wana historia nzuri financially. Hata hivyo capital gain yao siyo kubwa sana.

Hisa zinazopatikana kirahisi ni kama za Tanzania Oxygen ambazo zimekuwa na zero capital gain kwa muda mrefu. Vilevile, kumbuka kuwa biashara ya hisa siyo rahisi sana kama watu wengi wanavodhani, kama unataka kuhakikisha unatrade kwa faida ni vyema ukatumia muda mwingi kwenye kusoma sheria na taratibu za kufanya biashara hii kabla hujaianza.

NB: Hata kama wewe ni mkazi wa Tanzania siyo lazima ununue hisa za DSE tu, unaweza kuvuka mipaka na kuangalia mambo yakoje kwenye masoko mengine. Sheria inaruhusu na internet inawezesha.

Kila la heri katika uwekezaji.

Mkuu, upo sahihi, but wawekezaji wengi kwenye stock market hapa Tanzania hawaangalii capital gains (which is wrong), wengi wao ni speculators, they are purchasing a stock with the sole purpose of selling it at a higher price. Na kwa kweli wapo waliotengeneza fedha nyingi sana kwa mtindo huu wakati soko la DSE inaanza back in 1998. Kama ndugu FADHILIEJ anataka kufuata nyao zao basi ni vyema akasubiri wakati kampuni iko kwenye IPO.

Lakini hapo kwenye red mkuu, nadhani unahitaji kurefresh your memory. Labda nikuulize, unadhani Mtanzania anaruhusiwa kununua HISA nje ya nchi hata kwa zile kampuni ambazo hazijawa CROSS LISTED? Na mbaya zaidi kampuni nyingi za nje hazijawa cross listed DSE, kwani soko letu bado ni changa
 
kwa tz biashara ya hisa haina mpango kwani haina mzunguko wa kutosha (capital market is not active), ni bora ukafanya biashara nyingine nakushauri anza na business ya nafaka kwa tenda maalum,search market then supply) but not stock business.

Uko sahihi mkuu, kweli hisa za hapa Bongo hazina mpango mimi nimenunua share za Precision lakini naona hakuna chochote kinachoendelea ni bora hela zangu ningeziweka kwenye SACCOS kuliko kununua hizi hisa za makampuni ya hapa Bongo
 
Mkuu, upo sahihi, but wawekezaji wengi kwenye stock market hapa Tanzania hawaangalii capital gains (which is wrong), wengi wao ni speculators, they are purchasing a stock with the sole purpose of selling it at a higher price. Na kwa kweli wapo waliotengeneza fedha nyingi sana kwa mtindo huu wakati soko la DSE inaanza back in 1998. Kama ndugu FADHILIEJ anataka kufuata nyao zao basi ni vyema akasubiri wakati kampuni iko kwenye IPO.

Lakini hapo kwenye red mkuu, nadhani unahitaji kurefresh your memory. Labda nikuulize, unadhani Mtanzania anaruhusiwa kununua HISA nje ya nchi hata kwa zile kampuni ambazo hazijawa CROSS LISTED? Na mbaya zaidi kampuni nyingi za nje hazijawa cross listed DSE, kwani soko letu bado ni changa

Enterpreneur,

Thanks for the remarks. Mimi ni mtanzania ambaye ninamiliki hisa nje ya nchi, but the diference is ninaishi nje ya nchi. Pia nimeona jamaa wakinunua hisa online. So nadhani inawezekana kama jinsi inavyowezekana kwa mtanzania kwenda kufungua kiwanda nchi nyingine athough sijajua ina work vipi kwa mtu ambaye hana bank account katika nchi ambayo anaenda kununua hisa.
 
Kaka, njoo huku Selous tufanye biashara ya mbao. Tusafiroshe kwenda Japani na Dubai. Hayo DSE ni chaka, biashara ya ku-hedge finance haiko reliable hapa bongo. Ni wazungu huko kwao wanapiga hela. Kwan unaweza kununua hisa za Microsoft leo za milioni 5 ukauza kesho milioni 7 haaaaa..... Bongo doesnt work!!! Mimi nimesomea hayo mamboooo

Naomba ufafanuzi hiyo biashara unaweza fanya vip,risk zake na naweza anza na kianzio gani.
 
Naomba ufafanuzi hiyo biashara unaweza fanya vip,risk zake na naweza anza na kianzio gani.

Selous ni hifadhi ya Taifa. Kwanza kabisa pata uhakika kwamba biashara ni halali. Kwa mtaji wa sh. mil 5 yule aliyeshauri biashara ya chakula nadhani ndio inafaa zaidi.
 
Kwenye soko la hisa kuna wanunuzi wa aina mbili. Wa muda mfupi wanaotaka kununua hisa zinapokuwa bei chini na kuuza zikipanda. Kama uko kundi hili wakati mzuri wa kununua ni wakati wa IPO, japo ya precision haikua nzuri sana
Na kuna wale wa muda mrefu, yaani ananunua hisa na kuziweka. Kadri value ya hisa inavyopanda na value ya investiment yake inapanda (capital gain), huku kila mwaka anapata dividend japo ndogo, kwa kwetu hapa about 10% hivi.
Kama unataka uwekeze upate ada ya watoto sahau kwa dse. Kama una fedha ya kuweka kwa mda mrefu nunua kuliko kuweka savings account. Utapata dividend sawa kama interest ya bank na capital gain.
Vilevile unaweza kununua dola ukaweka bank kwa muda mrefu utapata shs zaidi.
 
Soko la hisa hali yake inabadilika kila wakati. This is to say, hapa JF huwezi kupata actual and reliable answer.

Unachotakiwa kufanya ni kuresearch market ikoje. Kwa research yangu mimi ninaona hisa za Dar es salaam Community Bank kwa sasa zinalipa kwa malengo ya muda mfupi. Hata hivyo availability yake ndio shida kidogo. Hisa zinapokuwa na capital gain nzuri wamiliki huwa hawataki kuziuza.

Kwa malengo ya muda mrefu hisa za CRDB ni nzuri zaidi kwa sababu wamekuwa kwenye soko muda mrefu na wana historia nzuri financially. Hata hivyo capital gain yao siyo kubwa sana.

Hisa zinazopatikana kirahisi ni kama za Tanzania Oxygen ambazo zimekuwa na zero capital gain kwa muda mrefu. Vilevile, kumbuka kuwa biashara ya hisa siyo rahisi sana kama watu wengi wanavodhani, kama unataka kuhakikisha unatrade kwa faida ni vyema ukatumia muda mwingi kwenye kusoma sheria na taratibu za kufanya biashara hii kabla hujaianza.

NB: Hata kama wewe ni mkazi wa Tanzania siyo lazima ununue hisa za DSE tu, unaweza kuvuka mipaka na kuangalia mambo yakoje kwenye masoko mengine. Sheria inaruhusu na internet inawezesha.

Kila la heri katika uwekezaji.

mkuu tupe link za reliable brokers wa kwenye net. Ukigoogle unawapata lakini reliability yao ndio kazi kuijua.
Je unaweza kuoperate kwa account za kwetu hapa? Najua kununua hakutasumbua, kupata dividend inakuwaje?
 
Angalizo mkuu, kuwa makini unapowekeza, wenzio tuliwekeza visenti vyetu NICOL imekula kwetu, saa hizi najuta bora ningezilia mandazi!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom